Skip to main content

Posts

Showing posts from May 2, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Waziri Mchengerwa aweka jiwe la msingi jengo la Jiji la Arusha

  Na John Mapepele  Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa leo  ameweka jiwe la msingi  kwenye jengo la utawala la jiji la Arusha na kushuhudia utiaji wa saini mikataba ya mradi wa Stendi Kuu ya Mkoa wa Arusha, Soko la Mrombo na Bustani ya Mapumziko ya Themi vyote vikiwa  thamani ya takriban shilingi bilioni 40. Akikagua ujenzi wa jengo la utawala la Halmashauri ya jiji la Arusha lenye sakafu tisa ambalo litakapokamilika  litagharimu bilioni 9.8 amemtaka  mkandarasi kukamilisha ujenzi kwa wakati ili kuondokana na adha ya sasa ya watumishi kufanyia kazi  kutokea kwenye ofisi zilizo katika maeneo tofauti hali inayochelewesha utoaji wa huduma kwa wananchi. "Namshukuru Mheshimiwa Rais kwa kuridhia kutoa fedha za ujenzi  wa jengo hili kwa kuwa baada ya kukamilika litakuwa mkombozi kwa watumishi" . Amefafanua Mhe. Mchengerwa  Aidha ameuelekeza uongozi wa Mkoa na Jiji la Arusha kuhakikisha jengo hilo linakamilika mara ...

Wafahamu wabunge Watano wa Kenya waliouawa mitaani Tangu Mwaka 2008

Katika historia ya taifa la Kenya, vifo vya viongozi mashuhuri wa kisiasa vinavyotokea kwa njia ya kutatanisha vimeacha makovu ya kudumu kwenye dhamira ya wananchi. Mauaji haya mara nyingi hutokea nyakati za misukosuko ya kisiasa, yakihusisha siasa za kiimla, uhasama wa uongozi, na migawanyiko ya kitaifa. Matukio haya ya kikatili yaliwafanya wananchi kutokuwa na imani na serikali zilizokuwa madarakani, huku yakiibua majonzi, hasira, na hofu iliyoenea miongoni mwa wananchi. Kila tukio la mauaji halikubaki kama tukio la kipekee bali liliibua athari za kina kuimarisha migawanyiko ya kisiasa, mianya ya usalama na wito wa uwajibikaji hasa katika idara za kijasusi. Wabunge waliopigwa risasi na kuuawa katika mazingira tatanishi baadhi walihusishwa na maono ya mabadiliko au msimamo wa wazi dhidi ya mifumo ya utawala, huku wengine wakionekana kuangukia mikononi mwa wahalifu. Katika taarifa hii tuwaangazia wabunge saba ambao walifariki ghafla baada ya kumiminiwa risasi wakiwa katika shughuli zao...

Mchengerwa amshukuru Raid Samia Kupandisha Mishahara

 *Mhe. Mchengerwa amshukuru Rais kwa kupandisha mishahara, awataka watumishi kuchapa kazi* Na John Mapepele  Siku moja baada ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kutangaza kupandisha kima cha chini cha mshahara wa watumishi wa Serikali kwa 35% Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa amemshukuru na kuwaelekeza watumishi chini ya Wizara yake kuwa wazalendo na wabunifu ili kuinua uchumi wa nchi. Mhe. Mchengerwa ameyasema haya leo Mei 2, 2025 wakati alipokuwa akiongea na watumishi wa Mkoa wa Arusha ambapo amesema Wizara yake inasimamia takribani asilimia 76 ya watumishi wote hivyo njia pekee ya kuunga mkono maono ya Mhe. Rais ni kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi. " Ndugu zangu ili tuweze kutekeleza maelekezo ya Mhe Rais wetu ni muhimu kutembea katika ndoto zake za kutaka kuwaletea watanzania maendeleo". Amesisitiza Mhe. Mchengerwa  Amesema kufuatia Rais kutoa ongezeko hilo la mshahara wa 35% Tanzania inakuwa miongoni mwa nchi pekee ambayo imewapa...

Bunge Lapitisha Kwa Kishindo Bajeti Ya Madini Tsh Bilioni 224.98 Kwa Mwaka 2025/2026

▪️ Maabara ya Kisasa ya Madini kujengwa Dodoma ▪️ Helikopta kununuliwa na kufungwa vifaa maalum kwa ajili ya utafiti ▪️ Wachimbaji Wadogo, Wanawake na Vijana ni sehemu ya Kipaumbele 📍  *Dodoma* Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kauli moja wamepitisha kwa kishindo Bajeti ya Ofisi ya Wizara kwa Mwaka wa Fedha 2025/26 yenye takribani Shilingi bilioni 224.98 kwa ajili ya wizara na taasisi zilizo chini yake kutekeleza majukumu yake. Bajeti hiyo iliyopitishwa kwa uungwaji mkono mkubwa kutoka kwa wabunge, inalenga kuendeleza utekelezaji wa miradi ya kimkakati katika Sekta ya Madini pamoja na kuimarisha utoaji wa huduma na utendaji kazi wa wizara na taasisi zake. Awali, Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde akiwasilisha Hotuba ya Mpango wa Mapato na Matumizi ya Wizara ya Madini kwa Mwaka wa Fedha wa Serikali wa 2025/2026 leo Mei 02, 2025 Bungeni Jijini Dodoma, ameeleza Bunge kuwa kiasi hicho ni kwa ajili ya kuwezesha Wizara ya Madini na taasisi zake kutimiza majukumu...

Serikali yavuna sh Bilioni 726,219 sekta ya madini

  • *Ni kuanzia Julai 2024, hadi Aprili 2025* • *Vibali 9,540 vya usafirishaji madini nje ya nchi vyatolewa* • *Matumizi ya Baruti yaongezeka* WIZARA ya Madini kupitia Tume ya Madini imefanikiwa kukusanya jumla ya Shilingi 726,219,317,398.14 ambapo Shilingi 612,593,046,886.50 ni malipo ya mrabaha na Shilingi 113,626,270,511.64 ni malipo ya ada ya Ukaguzi. Akizungumza Bungeni leo Mei 2, 2025 Waziri wa Madini Mheshimiwa Anthony Mavunde (MB) wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2025/2026 amesema makusanyo hayo ni katika kipindi cha Julai 2024 hadi Machi 2025 ambapo madini yenye thamani ya Shilingi 11,376,270,882,758.50 yalizalishwa na kuiwezesha serikali kupata kiasi hicho cha fedha. *USIMAMIZI, UKAGUZI NA BIASHARA YA MADINI*: Waziri Mhe. Mavunde amesema katika kipindi cha Julai 2024 hadi Machi 2025, vituo vipya saba vya ununuzi wa madini vilianzishwa ambavyo ni Nhungwiza - Geita, Nachingwea, Liwale, Likofia - Lindi, Mugumu, Serengeti – Mara na I...
  ▪️ Wizara yapanga kukusanya maduhuli ya shilingi trilioni 1.1.4l  ▪️ Kuwarasimisha na Kuwaendeleza Wachimbaji Wadogo ili wakue zaidi ▪️ Kuendeleza Mnyororo wa Thamani Katika Madini Muhimu na Madini Mkakati ▪️ Kuimarisha Uendeshaji wa Minada na Maonesho ya Madini ya Vito 📍 *Dodoma* Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde ameainisha vipaumbele vya Wizara ya Madini kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026, ambako imelenga kuimarisha mchango wa Sekta ya Madini katika kukuza uchumi wa taifa, kuongeza ajira, na kuinua ustawi wa jamii kupitia matumizi bora ya rasilimali za madini hapa nchini. Ameyabainisha hayo leo Mei 02, 2025 Bungeni Jijini Dodoma wakati akiwasilisha Hotuba ya Mpango wa Mapato na Matumizi ya Wizara ya Madini kwa Mwaka wa Fedha wa Serikali wa 2025/2026 ambapo kupitia mpango huo, Wizara ya Madini imepanga kukusanya maduhuli ya shilingi 1,405,537,268,755.00 (Trilioni 1.4). Ili kufikia lengo hilo la makusanyo ya maduhuli, Waziri Mavunde amebainisha kuwa, Wizara imeweka mkazo kwen...

Zaidi ya leseni 8,000 za uchimbaji madini zatolewa

  • Maeneo 65 yatengwa TUME ya Madini imetoa leseni 8, 501  katika kipindi cha Julai 2024 hadi Machi 2025 ikilinganishwa na lengo la kutoa leseni 10,294.  Hayo yamesemwa Bungeni jijini Dodoma leo Mei 2, 2025 na Waziri wa Madini Mheshimiwa Anthony Mavunde (MB) akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2025/2026. Akizungumza Mheshimiwa Mavunde amesema leseni za uchimbaji zilizotolewa ni za uchimbaji mkubwa wa madini (SMLs) 1; leseni za uchimbaji wa kati wa madini (MLs) - 25; leseni za utafutaji wa madini (PLs) 396; leseni za uchimbaji mdogo (PMLs) ni 6,227 Aidha, amesema leseni kubwa za biashara (DLs) zilizotolewa ni 548; leseni ndogo za biashara (BLs)  1,290; leseni za uyeyushaji (RFLs) 1; na leseni za uchenjuaji wa madini (PCLs) 13. Waziri Mavunde amesema katika kipindi cha Julai 2024 hadi Machi 2025, leseni 118 za utafutaji wa madini na leseni 41 za uchimbaji wa kati wa madini zilipewa hati za makosa kutokana na kutozingatia masharti ya lesen...