Skip to main content

Posts

Showing posts from March 15, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Serikali yawataka vijana kuchangamkia fursa za mikopo

Na Mashaka Mhando, Muheza  SERIKALI imetangaza mkakati wa kuhakikisha fursa za mikopo na zabuni za manunuzi ya umma zinawafikia vijana katika maeneo yote ya nchi ili kuwajengea uwezo wa kiuchumi na kupunguza ukosefu wa ajira. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Maendeleo ya Vijana), Joel Nanauka, ametoa kauli hiyo jana wilayani Muheza wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii ilipotembelea na kukagua shughuli za Kikundi cha Vijana cha ‘Mali Hai’. Nanauka ameiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Muheza kuhakikisha inatenga asilimia 30 ya manunuzi ya umma kwa ajili ya vijana, ikiwa ni pamoja na kuwapatia zabuni za ujenzi kikundi hicho ambacho kimeonesha uaminifu kwa kurejesha mkopo wa Shilingi Milioni 20. “Wizara itahakikisha vijana wanafikiwa kila kona ya nchi ili wanufaike na fursa hizi. Niwaombe vijana kutumia vyema Shilingi Bilioni 200 zilizotolewa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya uwezeshaji wananchi,” amesema Nanauka. Pia Waziri Nanauka amewa...

Serikali kuendelea kuimarisha miundombinu ya elimu

📍 Kamati yaridhishwa na ujenzi Chuo kikuu Mzumbe kampasi ya Tanga Na Mashaka Mhando, Mkinga WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema Serikali itaendelea kuimarisha miundombinu ya elimu ya juu kupitia miradi ya kimkakati ikiwemo ule wa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET), ili kuchochea utafiti na ubunifu utakaosaidia maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Prof. Mkenda ametoa kauli hiyo wilayani Mkinga wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Michezo na Utamaduni ilipotembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Kampasi ya Tanga ya Chuo Kikuu Mzumbe. Alisema serikali itaendelea kuboresha lakini pia alisema kuwa atahakikisha anavuta wawekezaji wengine binafsi kujenga taasisi za elimu katika eneo hilo. Alisema Wizara itahamasisha taasisi nyingine za elimu na sekta binafsi kuwekeza Mkinga ili kukuza dhana ya mji wa kitaaluma. Alibainisha kuwa mkoa wa Tanga utapewa kipaumbele kwa Chuo hicho kufundisha kozi za kimkakati ikiwemo uchumi wa Buluu (Blue Economy) Madini n...

Waziri Mkuu Aweka Jiwe la Msingi Shule ya Sekondari Mgombe Yenye Mkondo wa Amali ya Kihandisi, Katavi

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Machi 15, 2026 ameweka jiwe la msingi la Shule ya Sekondari Mgombe yenye mkondo wa Amali ya Kihandisi iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mlele, mkoani Katavi, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi ya kukagua na kufuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo mkoani humo. Ujenzi wa shule hiyo unatekelezwa kupitia Mradi wa Kuimarisha Ubora wa Elimu ya Sekondari (SEQUIP) kwa gharama ya shilingi bilioni 1.694 na hadi sasa umefikia asilimia 99 ya utekelezaji. Shule hiyo itatoa mafunzo ya amali katika fani mbalimbali zikiwemo ufundi magari, ufundi bomba, mifumo ya umeme wa jua pamoja na ufundi umeme wa magari. Mafunzo hayo yanalenga kuwajengea wanafunzi ujuzi wa vitendo utakaowawezesha kujiajiri, kuajiriwa au kuendelea na masomo ya elimu ya juu.

Waziri Mkuu Aagiza Uchunguzi wa Mfumo wa Upatikanaji wa Dawa Hospitalini

_Akemea watumishi wanaowaelekeza wananchi kununua dawa nje ya hospitali_ _Aonya utapeli wa ardhi za vijiji_ _Akemea wakandarasi wanaolipwa fedha za miradi lakini hawawalipi mafundi_ WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba ameagiza kufanyika kwa uchunguzi kuhusu mfumo wa upatikanaji wa dawa katika hospitali na vituo vya kutolea huduma za afya nchini. Ametoa agizo hilo leo Jumapili (Machi 15, 2026) alipokuwa akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Nsimbo katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Songambele mkoani Katavi, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani humo. Amesema Serikali imekuwa ikipeleka fedha kwa ajili ya ununuzi wa dawa katika hospitali na vituo vya afya, lakini bado baadhi ya wananchi wanapofika kutafuta huduma wanaelekezwa kwenda kununua dawa katika maduka binafsi nje ya hospitali. “Takwimu zinaonesha tuna utoshelevu wa dawa lakini mwananchi akienda hospitalini anaelekezwa mtaani kwenda kununua dawa. Huu mchezo haukubaliki. Duka la mtaani lin...

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa Wa Mara Mhe. Ghati Chomete Ashiriki Ziara ya Kamati ya Bunge Tafico

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mara, Mhe. Ghati Zephania Chomete, ameshiriki ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo iliyofanya ziara ya kutembelea na kukagua miradi ya Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO) inayolenga kuimarisha sekta ya uvuvi nchini. Ziara hiyo ilifanyika jana tarehe 13 Machi 2026 jijini Dar es Salaam, ambapo wajumbe wa kamati walitembelea na kukagua miradi mbalimbali ikiwemo mradi wa meli za uvuvi, ujenzi wa gati, ujenzi wa ghala la kuhifadhia samaki (cold storage), pamoja na mitambo ya kutengeneza barafu inayotumika katika shughuli za uvuvi. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, aliishukuru Kamati ya Bunge kwa kuisimamia sekta ya uvuvi kwa karibu kupitia ushauri na maelekezo kwa Serikali, jambo ambalo limechangia kwa kiasi kikubwa kufufuka kwa shughuli za Shirika la TAFICO. Aidha, Waziri huyo aliwapongeza watendaji wa miradi ya uvuvi kwa juhudi wanazozifanya katika kuhakikish...