Skip to main content

Posts

Showing posts from September 5, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

MAKAMU WA RAIS ASHIRIKI ADHIMISHO LA MISA TAKATIFU YA KUWEKWA WAKFU ASKOFU MSAIDIZI JIMBO KUU LA DAR ES SALAAM

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi ameshiriki Adhimisho la Misa Takatifu ya kuwekwa Wakfu Mhashamu Vincent Mpwaji, kuwa Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, iliyofanyika katika Viwanja vya Msimbazi Center – Dar es Salaam, leo tarehe 05 Septemba 2026. Misa hiyo, imeongozwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam Mhashamu Jude Thaddeus Ruwa’ichi, ambaye ni Askofu kiongozi katika uwekaji Wakfu, akisaidiwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dodoma Mhashamu Beatus Kinyaiya pamoja na Askofu Msaidizi Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam Mhashamu Henry Mchamungu. Pia, Adhimisho hilo limehudhuriwa na Maaskofu kutoka Majimbo Katoliki mbalimbali nchini, Viongozi wa madhehebu mbalimbali ya Kikristo, Viongozi wa Serikali, Viongozi wa Taasisi, Mapadre, Watawa, familia, ndugu, marafiki pamoja na waumini kutoka maeneo mbalimbali.

DKT. MWIGULU AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA JENGO LA OFISI ZA HALMASHAURI YA BAHI

 Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Jumamosi, Septemba 5, 2026, amekagua maendeleo ya ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Bahi na kuweka jiwe la msingi la mradi huo, unaolenga kuboresha mazingira ya utendaji na utoaji wa huduma kwa wananchi. Akiwasilisha taarifa ya mradi huo, Kaimu Mhandisi wa Wilaya ya Bahi, Sassoche Mtenya Maduhu, amesema jengo hilo linatarajiwa kugharimu jumla ya Sh bilioni 4.868 na litajengwa kwa awamu. Amesema hadi kufikia Agosti 30, 2025, Halmashauri ya Wilaya ya Bahi ilikuwa imepokea jumla ya Sh bilioni 1 kutoka Serikali kuu kwa ajili ya kuanza ujenzi wa jengo hilo, ambapo Sh milioni 994.546 zimetumika. Katika fedha hizo, Sh milioni 980.247 zimetumika kumlipa mkandarasi M/s Hamble Ulpan Engineering Company Limited, huku Sh milioni 14.3 zikitumika kwa ununuzi wa vyuma vilivyoagizwa kutoka Kiwanda cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, utekelezaji wa awamu ya kwanza ya mradi umefikia asilimia 100, ukiwa um...