Na Shomari Binda-Musoma TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ( TAKUKURU) wa Mara imefanikiwa kuokoa kiasi jumla ya shilingi milioni 70,212,800.00 yakiwemo malipo ya makaburi hewa. Hayo yamesemwa leo mei 27,2025 na Mkuu wa taasisi hiyo Muhamed Shariff alipokuwa akitoa taarifa ya utendaji kazi kwa kipindi cha miezi 3 ya januari hadi machi 2025 kwa Waandishi wa Habari. Amesema katika zoezi la uhamishaji wa makaburi kwa wananchi wanaopisha upanuzi wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti Kata ya Nyatwali Wilaya ya Bunda kiasi cha milioni 49,200,,200 kimeokolewa. Mkuu huyo wa TAKUKURU amesema fedhà hizo iliyokuwa ilipwe kama kifuta machozi kwa wanufaika wa makaburi hewa 123 ambapo kila kaburi lllipaswa kulipwa shilingi 400,000. Amesema walifanikiwa jambo hilo baada ya kufanya uchambuzi wa mchakato mzima uliotumika kuhalalisha ulipaji fidia za makaburi yaliyopswa kuhamishwa. Amedai kuwa uchambuzi ulibaini katika hatua ya uthaminishaji makaburi hayo yalithaminishwa kwa namna yalivyotambulish...
Marato tv - Sauti ya Jamii