Skip to main content

Posts

Showing posts from December 17, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Waziri Mkuu Akagua Athari Kwenye Jengo la Ofisi ya Kituo Cha Forodha Kwa pamoja Kasumulu

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Desemba 18, 2025 amekagua Jengo la Ofisi ya Kituo cha Forodha kwa Pamoja-Kasumulu ambacho kiliathiriwa na vurugu zilizotokea Oktoba 29, 2025.  Mheshimiwa Dkt. Mwigulu yupo mkoani Mbeya kwa ziara ya kikazi ya kukagua miundombinu ya umma na mali za watu binafsi zilizoathiriwa na vurugu zilizotokea Oktoba 29 Mwaka huu nchini.

Waziri Mkuu Akagua Athari Kwenye Majengo ya Mamlaka ya Mji Mdogo Kyela

  WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Desemba 18, 2025 amekagua majengo ya Mamlaka ya Mji mdogo wa Kyela ambayo yaliathiriwa na vurugu zilizotokea Oktoba 29, 2025. Mheshimiwa Dkt. Mwigulu yupo mkoani Mbeya kwa ziara ya kikazi ya kukagua miundombinu ya umma na mali za watu binafsi zilizoathiriwq na vurugu zilizotokea Oktoba 29 Mwaka huu nchini.

Jeshi la Polisi mkoani Mwaanza lawataka wananchi kuachana na mila potofu

Jeshi la Polisi wa Mwanza limewataka wananchi kuachana na imani potofu ikiwa ni pamoja na kuamini katika ushirikina ambao nao mauaji, ukatili na matukio mengine ya jinai katika baadhi ya maeneo, hususan katika Kisiwa cha Ukara, Wilaya ya Ukerewe mkoani Mwanza. Kauli hiyo imetolewa Disemba 17, 2025 na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, DCP Wilbrod Mutafungwa, alipofanya mkutano wa hadhara na wakazi wa Kata ya Bwisya wilayani humo kwa lengo la kutoa elimu ya usalama na kuhimiza usalama wa amani.   Mkutano kwenye mkutano huo uliowakutanisha viongozi wa Serikali, dini na wananchi, DCP Mutafungwa amesema wimbo wa amani ni la kila mmoja, hivyo kila a kuchukua kuchukua kuchukua vitendo vya uvunjifu wa amani vinavyofanywa na watu wanaojiita wataalam wa kusaka wachawi maarufu kama 'Kamchape'. Amebainisha kuwa kundi hilo limekuwa likijihusisha na uporaji wa mali, utapeli kwa kutumia ramli chonganishi na kuingia katika nyumba za watu kwa madai ya kuondoa ushirikina jambo ambalo linajenga ...

Dkt. Mwigulu: Tanroads na Tarura Fanyeni Tathmini ya Miradi Iliyolipwa Fedha za Awali

_Aagiza mikataba ya ujenzi wa miradi iwe na kipengele cha kufungua akaunti za malipo hapa nchini_ WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amewaagiza Watendaji Wakuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kufanya tathmini ya miradi yote ambayo malipo ya awali yameshafanyika na hatua za ujenzi zilizofikiwa katika miradi hiyo. Pia amewaagiza kuangalia kama utekelezaji wa miradi hiyo unaendana na kiwango cha fedha ambacho kimeshatolewa. “Na ikiwa itapatikana miradi ambayo imefanyika chini ya fedha iliyopatikana itakuwa ni hujuma dhidi ya uchumi wa nchi yetu, hawa ni lazima wafike kwenye mkono wa sheria” Ametoa maagizo hayo leo, Jumatano, Desemba 17, 2025 wakati akizungumza na wananchi baada ya kukagua uharibifu wa miundombinu mbalimbali ikiwemo mzani wa. Magari (Mpemba), Mahakama ya Mwanzo Tunduma, soko la Machinga akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Songwe. “Nimefuatilia, yupo mkandarasi ambaye mlimtoa kule Mbinga, asipate kazi nyingine ye...

Maafisa Habari Wasioendana na Kasi ya Serikali ya Awamu ya Sita "Kitanzini"....

    Serikali imewataka maafisa habari nchini kutumia teknolojia inayoendana na wakati na mazingira ili kuwafikishia wananchi habari sahihi kwa wakati. Hayo amebainisha mapema hii leo, Disemba 17, 2025, Katibu Mkuu Kiongozi, Dkt. Moses Kusiluka katika ufunguzi wa kikao kazi cha siku mbili cha  kitaifa cha kurugenzi ya mawasiliano ya Rais na maafisa habari wa serikali  kilichoandaliwa na kurugenzi ya mawasiliano ikulu ambapo  pia amewasihi maafisa hao kuepuka kutoa habari za kiongozi badala ya kutoa taarifa za serikali katika sekta husika jambo ambalo si Zuri kwa ujenzi wa taifa. Aidha, Balozi Kusiluka amesema  kuwa ni muhimu kujipanga vizuri katika kukabiliana na matumizi hasi ya teknolojia ya habari katika kuleta maendeleo na ufanisi katika utoaji huduma kwa wananchi. Pia, Bolizi kusiluka amewataka maafisa habari nchini kutokuwa maripota wa matukio badala yake kuwa maafisa wa habari na mawasiliano na kuwa na maudhui yenye kujenga taifa. Kwa upande wake Mkur...

Maafisa Habari Wasioendana na Kasi ya Serikali ya Awamu ya Sita "Kitanzini"....

  Serikali imewataka maafisa habari nchini kutumia teknolojia inayoendana na wakati na mazingira ili kuwafikishia wananchi habari sahihi kwa wakati. Hayo amebainisha mapema hii leo, Disemba 17, 2025, Katibu Mkuu Kiongozi, Dkt. Moses Kusiluka katika ufunguzi wa kikao kazi cha siku mbili cha  kitaifa cha kurugenzi ya mawasiliano ya Rais na maafisa habari wa serikali  kilichoandaliwa na kurugenzi ya mawasiliano ikulu ambapo  pia amewasihi maafisa hao kuepuka kutoa habari za kiongozi badala ya kutoa taarifa za serikali katika sekta husika jambo ambalo si Zuri kwa ujenzi wa taifa. Aidha, Balozi Kusiluka amesema  kuwa ni muhimu kujipanga vizuri katika kukabiliana na matumizi hasi ya teknolojia ya habari katika kuleta maendeleo na ufanisi katika utoaji huduma kwa wananchi. Pia, Bolizi kusiluka amewataka maafisa habari nchini kutokuwa maripota wa matukio badala yake kuwa maafisa wa habari na mawasiliano na kuwa na maudhui yenye kujenga taifa. Kwa upande wake Mkurugenzi ...

Waziri Tamisemi Apongeza Utaratibu wa Usikilizaji Kero Arusha

 *_Aelekeza Mikoa yote nchini kusikiliza kero na kusimamia miradi ya maendeleo_* Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Silas Shemdoe ametoa Pongezi kwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha kwa programu yake ya usikilizaji na utatuzi wa kero za wananchi, akiagiza Mikoa mingine kufanya hivyo kama sehemu ya  utekelezaji wa Maagizo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. Mhe. Prof. Shemdoe amebainisha hayo leo Jumatano Disemba 17, 2025 alipokutana na kuzungumza na Mkuu wa Mkoa wa Arusha CPA Amos Gabriel Makalla, Jijini Arusha, akimpongeza pia kwa namna ambavyo ameendelea kuhakikisha kuwa Arusha inabakia salama na tulivu ili kuruhusu shughuli za kiuchumi na kijamii kuweza kuendelea. "Niwapongeze kwa kazi kubwa na nzuri mnayoifanya. Nimefuatilia na kufarijika na kazi ya juzi ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi na hili ni suala ambalo tunatakiwa tulitekeleze kama alivyoelekeza Mhe. Rais kwamba tujitahidi kusikiliza wana...