TFS kuongeza askari, vifaa na kujenga kituo cha walinzi Pohama Na Mwandishi Wetu, Singida Ulinzi wa Msitu wa Hifadhi wa Mgori mkoani Singida unatarajiwa kuimarika baada ya Kamishna wa Uhifadhi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Profesa Dos Santos Silayo, kutangaza mpango wa kuongeza askari, kupeleka vifaa vya kisasa vya ulinzi na kuanzisha ujenzi wa Ranger Post katika kijiji cha Pohama. Profesa Silayo alitoa ahadi hiyo leo Jumanne, Novemba 11, 2025, wakati wa kikao maalum cha Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Singida, kilichofanyika katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Mhe. Godwin Gondwe, kwa lengo la kujadili mikakati ya kuimarisha ulinzi na uhifadhi wa Msitu wa Mgori. Msitu huo, ambao ni miongoni mwa hifadhi muhimu nchini, umekuwa ukikabiliwa na changamoto za uchomaji moto, ukataji miti holela na uvamizi unaoathiri juhudi za Serikali katika kulinda rasilimali za misitu. Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Gondwe alisisitiza umuhimu wa uhifadhi shirikishi, akipendek...
Marato tv - Sauti ya Jamii