Skip to main content

Posts

Showing posts from November 12, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Miradi ya CSR Ya Migodi Yawanufaisha Wananchi Simiyu

📍Simiyu Serikali imesema itaendelea kusimamia kwa karibu utekelezaji wa miradi ya Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) inayotekelezwa na kampuni za uchimbaji madini nchini, ili kuhakikisha wananchi wanaoishi jirani na migodi wananufaika moja kwa moja na shughuli za uchimbaji madini. Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Simiyu, Mayigi Makolobela, alisema hayo hivi karibuni alipokagua utekelezaji wa miradi ya CSR inayofanywa na kampuni za uchimbaji madini katika mkoa huo, akibainisha kuwa miradi hiyo imechangia kwa kiasi kikubwa kuboresha huduma za kijamii ikiwemo elimu, afya na miundombinu ya umeme. “Serikali inatambua mchango mkubwa wa sekta ya madini katika kukuza uchumi wa nchi na kuboresha maisha ya wananchi. Ndiyo maana tunasisitiza kampuni zote za uchimbaji, zikiwemo zinazomilikiwa na wachimbaji wadogo, kutekeleza wajibu wao wa kijamii kupitia miradi ya CSR ili jamii inayoishi jirani na migodi inufaike moja kwa moja na rasilimali hizo,” alisema Makolobela. Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kampuni ...

Mbunge Mavunde Aanzisha Ujenzi wa Zahanati Mtaa wa Maseya-Hombolo Makulu

▪️Wananchi wampongeza kwa kuanza kutimiza ahadi yake ▪️Aapa kukamilisha ujenzi kwa wakati ▪️Wananchi wamshukuru Rais Samia kwa visima vya umwagiliaji na Umeme Mbunge wa Jimbo la Mtumba Mh. Anthony Mavunde leo ameshiriki na mamia ya wananchi wa Mtaa wa Maseya-Kata ya Hombolo Makulu kuanzisha ujenzi wa Zahanati katika mtaa huo ikiwa ni utekelezaji wa ahadi aliyoitoa wakati wa Uchaguzi Mkuu 2025. “Nawashukuru wananchi wa Maseya kwa kumchagua Rais Samia,mimi na Diwani wa kata yetu kwa kura nyingi sana kwenye uchaguzi mkuu uliomalizika. Kazi yetu sasa ni kufanya kazi na kutatua changamoto za wananchi,nawapongeza kwa kuitikia wito wa ujenzi wa zahanati yetu ambayo itasaidia kusogeza karibu huduma ya Afya kwa wananchi wetu. Nitakabidhi matofali 2000 na saruji mifuko 100 ili kulifikisha juu jengo letu mpaka hatua ya upauaji,ni imani yangu kwamba serikali yetu sikivu itatuunga mkono ukamilishaji wa zahanati hii”Alisema Mavunde Akitoa salamu za wananchi,Mwenyekiti wa Mtaa wa Maseya Ndg. Alexande...

ZAIDI YA WANANCHI 1,5000 KUNUFAIKA NA MRADI WA MAJIKO BANIFU WILAYANI BABATI

📌 *Majiko banifu 1,582 kusambazwa na kuuzwa kwa bei ya ruzuku* .   📌 *Jiko moja kuuzwa kwa bei ya ruzuku ya TZS 11,200* . 📍 *BABATI*  Mkuu wa Wilaya ya wa Babati, Mheshimiwa Emmanuela Kaganda, leo Novemba 12, 2025 kwa niaba ya wakazi wa wilaya ya babati amezindua mradi wa uuzaji na usambazaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku.   Uzinduzi huu ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya mkuu wa mkoa wa Manyara, Mheshimiwa Queen Sendiga akiwataka wakuu wa wilaya wote wa mkoa wa manyara kuzindua na kusimamia kikamilifu utekelezaji wa mradi wa usambazaji na uuzaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku katika wilaya zao. Uzinduzi umefanyika katika kata ya Magugu wilayani babati, ambapo jumla ya majiko banifu  1,582 yatauzwa na kusambazwa kwa bei ya ruzuku ya TZS 11,200 ambayo ni sawa na aslimia 80 ya ruzuku ya TZS 56,000 ambayo ni bei ya awali ya jiko. Akizungumza wakati wa uzinduzi, Mheshimiwa Kaganda amesema mpango huo umelenga kuhakikisha wananchi wote, hususani wa k...

Wachimbaji Wadogo wa Madini Simiyu Wapaza Sauti: “Tunaweza Tukipewa Umeme na Mikopo

Simiyu WACHIMBAJI Wadogo wa Madini wa Mkoa wa Simiyu wameiomba Serikali pamoja na taasisi za kifedha kuwaunga mkono kwa kuwapatia umeme wa kudumu na mikopo yenye masharti nafuu, wakisema changamoto hizo zimekuwa kikwazo kikubwa katika kuongeza uzalishaji wa madini, hususan dhahabu. Mmoja wa wachimbaji wanawake kupitia Chama cha Wachimba Madini Wanawake Tanzania (TAWOMA) mkoani humo, Anisia Japhet, amesema wamekuwa wakitumia gharama kubwa kuendesha mitambo kutokana na kutegemea nishati ya dizeli. “Tunatumia dizeli ambayo ni ghali. Lita 80 zinamalizika ndani ya saa 24. Tungepata umeme wa kudumu, tungepunguza gharama na kuongeza tija,” amesema Anisia. Ameongeza kuwa uchimbaji si kazi ya wanaume pekee bali ni fursa yenye manufaa makubwa kwa wanawake wanaojituma. “Nikiwa mwanamke, nimefanikiwa kusomesha watoto na kuendesha maisha yangu kupitia uchimbaji. Kila mwezi tunapata wastani wa viroba 100 vya mawe, na kila kiroba kinaweza kutoa gramu moja au zaidi za dhahabu,” ameongeza. Kwa upande w...