Simanzi nzito imetanda nchini India kufuatia ajali mbaya ya ndege ya Air India, iliyokuwa ikielekea London na kubeba watu 242, iliyoanguka Alhamisi, Juni 12, muda mfupi baada ya kuruka kutoka Uwanja wa Ndege wa Ahmedabad, magharibi mwa India. Maafa haya yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 200, na taarifa za awali zikibainisha kuwa miili 204 imepatikana. Kiasi cha waliokuwa ndani ya ndege na waliokuwa chini wakati waanguko ulipotokea bado hakijafahamika, huku uchunguzi ukiendelea kubaini ukubwa kamili wa janga hili. Ndege hiyo ilianguka kwenye makazi yaliyotumiwa na madaktari, na simulizi ya mwanamke mmoja anasema mwanaye alivyonusurika baada ya kuruka kutoka dirishani ghorofa ya pili, baada ya ndege hiyo kuangukia makazi. Katika ndege hiyo walikuwepo raia 169 wa India, Waingereza 53, Wareno saba na Mkanada mmoja. Ajali hii ya kushtua inaongeza kwenye orodha ndefu ya matukio mabaya katika historia ya usafiri wa anga, ikikumbusha ulimwengu juu ya hatari zilizopo licha ya maendeleo makub...