Skip to main content

Posts

Showing posts from December 30, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Waziri Mavunde asimamisha Uchimbaji Madini kwenye Mto Zila kijiji cha Ifumbo wilayani Chunya-Mbeya

▪️Aelekeza shughuli za uchimbaji madini kusimama kipindi hichi cha Masika kama ilivyoelekezwa na NEMC ▪️ Timu ya Wataalam kufanya tathmini kwa kina na kutoa taarifa ya athari ya Mazingira ▪️Akemea wananchi kuharibu mali za mwekezaji ▪️Asisitiza Sheria na kanuni kufuatwa 📍Chunya,Mbeya Waziri wa Madini, *Mh.Anthony Mavunde (Mb)* amesimamisha shughuli za uchimbaji zilizokuwa zikifanywa na kampuni ya G & I Tech Mining Company Ltd kwa kipindi hichi cha masika na pia mpaka pale tathmini ya kitaalam ya mazingira itapokamilika juu ya shughuli za uchimbaji madini kwenye Mto Zila. Ameyasema hayo Jana tarehe 30 Desemba, 2024 katika kijiji cha Ifumbo, Wilayani Chunya alipotembelea eneo la leseni ya mwekezaji ambalo lilivamiwa na wananchi na kusababisha mgogoro mkubwa na uharibifu wa mali za mwekezaji huyo. "Tumetembelea maeneo yote mawili, na sote tumejionea hali halisi ya mazingira. Ni dhamira na maelekezo ya *Mh Rais Dkt. Samia S. Hassan* kuona shughuli zote za kiuchumi hususan za madi...

Tra yamkosha Askofu Mkuu Ruwa'ichi,atoa ahadi ya Ushirikiano

Askofu Mkuu Mwandamizi wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Jude Thaddeus Ruwa'ichi amesema Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam litaendelea kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuhamasisha watu walipe Kodi kwa kutokana na Kodi kuwa ni suala nyeti kwa maendeleo ya Nchi. Akizungumza na Kamishna Mkuu wa TRA Bw. Yusuph Juma Mwenda alipomtembelea nyumbani kwake Jijini Dar es Salaam ikiwa ni mwendelezo wa kuwashukuru Walipakodi, Askofu Mkuu Ruwa'ichi amesema Suala la kulipa Kodi na kukusanya Kodi ni suala linalohusu maendeleo ya nchi na ni sehemu ya wajibu wa Kiraia. Askofu Mkuu Ruwa'ichi ameeleza kufurahishwa na mfumo wa ukusanyaji wa Kodi unaofanywa katika kipindi cha sasa na ukaribu uliopo baina ya Mamlaka hiyo na Wananchi. "Kwa niaba ya Watanzania wenzangu niwapongeze kwa kazi kubwa mnayoifanya na kuwahakikishie kwamba kadiri ya nafasi na uwezo wetu tutajitahidi kuwahimiza watu wazingatie na waenzi wajibu wa kulipa Kodi kwaajili ya Maendeleo ...

Mbunge Mathayo ampa tano Rais Samia kwa kutoa Bilioni Moja Sekta Ya Uvuvi

Na Shomari Binda-Musoma MBUNGE wa jimbo la Musoma mjini Vedastus Mathayo amesema Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan ameshawafikia wananchi wa Musoma na kuwawezesha kiuchumi. Kauli hiyo ameitoa leo disemba 30 aliposhiriki na kuzungumza kwenye kongamano la jukwaa la uwezeshaji wananchi kiuchumi Wilaya ya Musoma lililofanyika kwenye uwanja wa shule ya msingi Mukendo. Jukwaa hilo ni muendelezo wa matukio ya Mama Samia Musoma Festival ilyoandaliwa na ofisi ya mkuu wa Wilaya ya Musoma. Mathayo amesema kupitia sekta ya uvuvi pekee Rais Samia kwa manispaa ya Musoma ametoa vizimba na chakula cha samaki ikigharimu zaidi ya bilioni 1. Amesema licha ya eneo hilo la uvuvi tayari halmashauri ya manispaa ya Musoma imeanza kutoa mikopo ya asilimia 10 kwa wanawake,vijana na wenye ulemavu. Mbunge guyo amesema hizo zote ni fursa za kuwawezesha wananchi kiuchumi ambazo wanapaswa kuzitumia na kujiinua. Amesema wananchi wanapaswa kuacha uvivu na kujituma kufanya kazi ili fursa zilizotolewa ziweze kuwainua. ...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali amlilia Jaji Werema

 

Rais Dkt.Samia amlilia marehemu mheshimiwa Jaji Mwanaisha Kwariko

  Asema alikuwa alikuwa ni moja ya majaji wa mahakama ya rufani wenye uwezo mkubwa_ WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Desemba 30, 2024 amemwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye mazishi ya Mheshimiwa Mwanaisha Kwariko ambaye alikuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani na Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.  kitoa Salama pole kwa waombolezaji nyumbani kwa marehemu Kondoa, Mkoani Dodoma, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Rais Dkt. Samia ameguswa na kifo cha Mheshimiwa Mwanaisha kwani alikuwa ni moja ya majaji wa mahakama ya rufani wenye uwezo mkubwa katika nafasi zote alizozitumikia.    Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Marehemu Mheshimiwa Mwanaisha alikuwa kiongozi aliyetekeleza wajibu wake kwa weledi na uadilifu “Msiba huu kwetu ni mzito, jukumu letu Wanakondoa, Watanzania, Majaji na wajumbe wa Tume ni kuendelea kumuombea kwa Mwenyezi Mungu” Aidha, Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa kila mmoja kuenzi yote mazuri aliyoyafanya Mheshimiwa Mwanaisha katika kipindi c...