Skip to main content

Posts

Showing posts from February 18, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mzee Wassira Amtembelea Mama Maria Nyerere Msasani

 Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (Bara) Ndg. Stephen Wasira, amemtembelea na kumjulia hali Mama Maria Nyerere, mke wa Hayati Baba wa Taifa na Rais wa kwanza wa Tanzania Mwalimu Julius Kambarage Nyerere nyumbani kwake Msasani jijini Dar es Salaam leo Februari 18, 2026.

Rea Yatoa Elimu ya Umeme Mkoani Tanga

📌 *Wananchi wapewa elimu ya nikonekt* . 📌 *Wananchi waaswa kutunza na kulinda miundombinu ya umeme* . 📍 *PANGANI*  Wakala wa nishati vijijini (REA) umeendelea na zoezi  la uhamasishaji wananchi kujiunga na huduma ya umeme. Uhamasihaji umefanyika wilayani Pangani ambapo maafisa wa REA na TANESCO wametembelea nyumba ambazo zimenufaika na miradi ya umeme pamoja na kufanya mikutano ya hadhara yenye lengo kuu la kuwapa uelewa wananchi juu ya umuhimu wa kujiunga na huduma ya umeme. Akizungumza wakati wa uhamasishaji Afisa maendeleo ya jamii kutoka REA , ndugu Abdulrazack Mkomi amesema,Kwa sasa taratibu za uombaji huduma ya umeme zimeboreshwa zaidi  na hakuna tena mambo ya kutumia fomu kufanya maombi ambapo kwa kutumia tu namba ya Nida mwananchi anaweza kufanya ombi la  umeme moja kwa moja TANESCO kupitia huduma ya NIKONEKT. “Kwa kutumia simu janja, mwananchi atapakua huduma ya Nikonekt na kufanya maombi au kama ni simu ya kawaida atabonyeza *152*00# na kisha kufuata mae...

Rea yatoa elimu ya umeme mkoani Tanga

  📌 *Wananchi wapewa elimu ya nikonekt* . 📌 *Wananchi waaswa kutunza na kulinda ya umeme* . 📍 *PANGANI*  Wakala wa vijijini (REA) umeendelea na zoezi la uhamasishaji kujiunga na huduma ya umeme. Uhamasi umefanyika wilayani Pangani umeme ambapo mamlaka ya REA na TANESCO wametembelea nyumba ambazo zimenufaika na miradi ya umeme pamoja na mikutano ya hadhara yenye lengo kuu la kuwapa uelewa wananchi juu ya umuhimu wa kujiunga na huduma. Akizungumza wakati wa uhamasishaji Afisa maendeleo ya jamii kutoka REA , ndugu Abdulrazack Mkomi amesema, Kwa sasa taratibu za uombaji huduma ya umeme zimeboreshwa zaidi na hakuna tena mambo ya kutumia kufanya maombi ambapo kwa kutumia namba ya Nida mwananchi anaweza kufanya ombi la umeme moja kwa moja TANESCO kupitia huduma ya NIKONEKT. “Kwa kutumia simu janja, mwananchi atapakua huduma ya Nikonekt na kufanya maombi au kama simu ya kawaida atabonyeza *152*00# na kisha kufuata maelekezo ya kufanya ombi, hakuna wakala wanaosajili maombi mtaani t...

Dkt. Mwigulu;Dkt.Samia ni Rais wa Matokeo

_Akagua ujenzi wa Chuo cha VETA Same._ WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema kuwa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ni Rais wa Matokeo na amedhihirisha hayo katika kipindi chake cha uongozi. Amesema hayo leo Februari 18, 2026 alipokagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa Chuo cha  VETA katika Wilaya ya Same, Tarafa ya Chome Suji Kata ya Makanya. Ujenzi wa Chuo hicho utagharimu kiasi cha Shilingi Bilioni 1.4 kutoka Serikali kuu ili kukamilisha ujenzi wa Chuo hicho  kwa awamu ya kwanza na  mpaka sasa kiasi cha Shilingi milioni 542 kimeshapokelewa *Wilayani hapo*  Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alipoingia madarakani *kulikuwa na* wilaya zaidi ya 60 ambazo hazikuwa na mradi wowote wa VETA lakini *alielekeza* wilaya zote ambazo hazina VETA zijengwe ikiwemo na mikoa isiyokuwa na vyuo hivyo”  “Lakini pia alikuta kuna Wilaya zaidi ya 119 hazina hospitali *za* Wilaya, pia alikuta zaidi ya kata 649 hazikuwa na vituo vya afya, ndani y...

Rais Samia amlilia maestro Stephen Hiza aliyetunga Tanzania Nchi ya Furaha 1967

*Na MASHAKA MHANDO, Tanga* RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amepokea kwa majonzi makubwa kifo cha nguli wa muziki wa dansi nchini, Hayati Stephen Hiza (80), aliyetunga na kuimba wimbo wa kitaifa wa uzalendo, *"Tanzania Nchi ya Furaha."* Hayati Mzee Hiza amehifadhiwa leo, Februari 18, 2026, katika nyumba yake ya milele eneo la Mwanzange, jijini Tanga. Akiwa na historia iliyotukuka, Mzee Hiza atakumbukwa kwa utunzi wake uliotikisa Radio Tanzania (RTD) mwaka 1967 akiwa na bendi kongwe ya *Atomic Jazz ya Tanga*, akizalisha vibao vilivyodumu vizazi na vizazi kama *"Leo Nakupasulia"*, *"Hamida Wangu"*, na *"Sitamani Kitu"*. *Alama ya Mwaka 1967 na Uzalendo* Wimbo uliompa heshima ya kipekee na kumfanya atambulike kama "Mzalendo Namba Moja" wa sanaa ni *"Tanzania Nchi ya Furaha"*. Wimbo huu, uliotungwa miaka sita tu baada ya Uhuru, umekuwa utambulisho wa amani na furaha ya Watanzania, jambo ambal...

Agnes Marwa Atoa Tuzo kwa Shule za Sekondari Zilizofanya Vizuri Manispaa ya Musoma

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mara, Agnes Marwa, leo ametoa tuzo na zawadi maalum kwa shule za sekondari zilizofanya vizuri katika Manispaa ya Musoma, ikiwa ni hatua ya kutambua na kuhamasisha ubora wa elimu mkoani humo. Katika hafla hiyo iliyofanyika ndani ya Manispaa ya Musoma, Agnes Marwa amekabidhi tuzo kwa shule zilizopata matokeo bora katika Mtihani wa Kidato cha Nne, sambamba na kuwazawadia walimu wa masomo yaliyopata alama A pamoja na mwanafunzi aliyefanya vizuri zaidi kwa kupata Daraja la Kwanza (Division I.7) Thelesia Obotto anayetokea Shule ya Sekondari Bweri, jambo lililopokelewa kwa shangwe na pongezi kutoka kwa viongozi na wadau wa elimu waliohudhuria hafla hiyo. Mgeni rasmi katika tukio hilo alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Juma Chikoka, ambaye aliambatana na Mstahiki Meya wa Manispaa Mh. Alex Nyabiti, Waheshimiwa Madiwani, Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa, Katibu wa CCM Mkoa wa Mara  pamoja na Katibu wa UWT Mkoa na viongozi wengine wa chama na serikali. Akizungumza wak...