Skip to main content

Posts

Showing posts from May 25, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Tanzania Kuandaa Mpango Wa Hatua za Mapema za Kujiandaa Kukabiliana na Ukame - Dkt. Yonazi

Na Mwandishi wetu - Msumbiji TANZANIA inaandaa Mpango wa Kitaifa wa Hatua za Mapema za kujiandaa, kukabiliana na ukame kwa maeneo yanayokabiliwa na janga hilo kwa kushirikiana na Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP), ikiwa ni jitihada za kupunguza athari za janga hilo nchini. Hatua hiyo inaonesha dhamira ya serikali kuachana na utaratibu wa kusubiri madhara yatokee ndipo ichukue hatua, na badala yake kuelekea katika usimamizi wa hatari unaozingatia maandalizi na tahadhari za mapema. Hayo yameelewa na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Dkt. Jim Yonazi, katika ziara ya kubadilishana uzoefu kati ya Tanzania na Msumbiji kuhusu hatua za mapema kabla ya majanga unaoendelea kwa siku tano kuanzia tarehe 25 hadi 29 Mei, 2026 Mjini Maputo Msumbiji. Alisema ukame una madhara makubwa katika kilimo, mifugo, rasilimali za maji, usalama wa chakula, maisha ya wananchi, maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa ujumla. “Kwa sasa Tanzania inaendelea kuandaa Mpango ...

Ruvuma Yapokea Majiko Banifu 7,648 kwa bei ya ruzuku

📍 *Songea , Ruvuma.* Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Mheshimiwa Brigedia Jenerali Ahmed Abbas Ahmed, leo Mei 25, 2026 amepokea rasmi mradi wa uuzaji na usambazaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kupitia kampuni ya Burn Manufacturing Company Limited. Mradi huo unalenga kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa wananchi wa Mkoa wa Ruvuma kupitia usambazaji wa majiko banifu yenye teknolojia ya kisasa kwa gharama nafuu kutokana na ruzuku inayotolewa na Serikali. Akizungumza wakati wa kupokea mradi huo, Mkuu wa Mkoa ameipongeza REA kwa kuendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya nishati safi ya kupikia nchini, akieleza kuwa majiko banifu yana mchango mkubwa katika kuboresha afya za wananchi pamoja na kulinda mazingira. Amesema matumizi ya majiko hayo yatasaidia kupunguza athari zinazotokana na matumizi ya kuni na mkaa usio salama, ikiwemo moshi unaosababisha madhara ya kiafya kwa watumiaji, hususan wanawake na watoto. Mheshimiwa Ahmed Ab...

Dkt. Mwigulu Kumwakilisha Rais Samia Congo Brazaville

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba ameondoka nchini leo (Jumatatu, Mei 25, 2026) kwenda Brazzaville, Jamhuri ya Kongo kumwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye Mkutano wa 61 wa Mwaka wa Bodi ya Magavana wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB). Mkutano huo utafanyika Mei 26 – 27, 2026, katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Kintele jijini Brazzaville, Jamhuri ya Kongo. Mkutano huu ni jukwaa muhimu la majadiliano ya kimkakati kuhusu masuala muhimu ya maendeleo ya dunia, yakihusisha nchi wanachama, taasisi za kikanda na kimataifa ambalo linahusisha kuhamasisha upatikanaji wa rasilimali za fedha ili kuwezesha utekelezaji wa ajenda ya maendeleo ya Afrika na kuimarisha uwezo wa bara kukabiliana na changamoto mbalimbali za kiuchumi na kifedha duniani. Mkutano huo utawakutanisha wajumbe wapatao 3000 ikiwemo Mawaziri wa Fedha na Magavana wa Benki Kuu za Afrika, Watunga Sera, wafanyabiashara, Taasisi za Kifedha, Washirika wa Maendeleo, Wajasiriamali pamoja na Wawekezaji.

Ajali Barabarani zimeua watu 1,066 2025/26

Serikali imesema watu 1,066 walipoteza maisha kutokana na ajali za barabarani kati ya Julai 2025 hadi Aprili 2026, ikilinganishwa na vifo 1,275 vilivyotokea katika kipindi kama hicho mwaka 2024/25. Takwimu hizo zimetolewa Bungeni na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi, wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2026/27. Amesema matukio ya ajali za barabarani yamepungua kutoka 1,322 hadi 1,233 katika kipindi hicho, hali inayoashiria maboresho ya usalama barabarani nchini. Aidha, idadi ya majeruhi imepungua hadi 1,869 kutoka 2,278, sawa na upungufu wa asilimia 18.42. Katambi amesema mafanikio hayo yametokana na juhudi za Jeshi la Polisi katika kuimarisha doria, kusimamia sheria za usalama barabarani na kuchukua hatua kwa wanaokiuka sheria. Serikali itaendelea pia kutoa elimu kwa umma kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii ili kupunguza zaidi ajali za barabarani.

Oboth Atwaa Uspika wa Bunge la 12 la Uganda kwa Ushindi wa Kishindo

Uganda imeingia rasmi katika ukurasa mpya wa kisiasa baada ya mwanasiasa mkongwe na mwenye ushawishi mkubwa, Jacob Oboth-Oboth, kuchaguliwa kuwa Spika mpya wa Bunge la 12 la Uganda kwa ushindi mkubwa wa kura 441 katika uchaguzi uliofanyika Mei 25,2026 mjini Kampala. Ushindi huo wa kishindo umeonyesha wazi namna alivyofanikiwa kujenga ushawishi mkubwa ndani ya chama tawala cha NRM pamoja na kuungwa mkono na wabunge wengi waliotaka kuona sura mpya ikichukua nafasi ya uongozi uliokuwa ukikabiliwa na misukosuko ya kisiasa na lawama kutoka kwa wananchi. Mara baada ya matokeo kutangazwa, ukumbi wa bunge ulilipuka kwa shangwe, makofi na vifijo huku wabunge kadhaa wakisimama kumpongeza Oboth kwa ushindi huo uliotajwa kuwa mmoja wa ushindi mkubwa zaidi katika historia ya uchaguzi wa uspika nchini Uganda. Katika hotuba yake ya kwanza, Oboth ameahidi kurejesha heshima, nidhamu na mshikamano ndani ya bunge huku akisisitiza kuwa taasisi hiyo lazima iwe sauti ya wananchi wote bila kujali tofauti za ...

Jeshi la Zimamoto na Uokoji Lajipanga Kutoa Elimu Kwa Wananchi

  Na Mwanamkuu Mwandoro, Tanga. Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani Tanga limejipanga kuendelea kutoa elimu Kwa wananchi ili kupunguza majanga na athari zinazoweza kutokea. Hayo yamesemwa na kamanda wa Zimamoto na Uokoaji mkoani Tanga,Mrakibu mwandamizi Katala Issa alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake ameeleza kuwa ni jukumu lao kuhakikisha jamii wanafahamu matumizi sahihi ya nishati safi kama gesi na umeme. Pamoja na hayo pia kamanda Katala pia amewataka wananchi kuoa taarifa mapema kupitia namba Yao ya dharura pindi wanapoona viashiria vya majanga na kutosubiri majanga kuwa makubwa kwani Kuna athari nyinge huzuilika kwani kwasasa jeshi lina mitambo mipya na yakutosha. Sambamba na hayo pia amewataka kutumia vizuri namba hiyo kwani kumekuwa na watu wanaotoa taarifa za uongo na kuzua taharuki na kusababisha usumbufu Kwa jeshi hilo. Jeshi la Zimamoto na uokoji pia limetaka wananchi kutojenga kiholela kwani hii huwapa wakati magumu pindi majanga yanapotokea. "Si...

Ajali Barabarani zimeua watu 1,066 2025/26

Serikali imesema watu 1,066 walipoteza maisha kutokana na ajali za barabarani kati ya Julai 2025 hadi Aprili 2026, ikilinganishwa na vifo 1,275 vilivyotokea katika kipindi kama hicho mwaka 2024/25. Takwimu hizo zimetolewa Bungeni na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi, wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2026/27. Amesema matukio ya ajali za barabarani yamepungua kutoka 1,322 hadi 1,233 katika kipindi hicho, hali inayoashiria maboresho ya usalama barabarani nchini. Aidha, idadi ya majeruhi imepungua hadi 1,869 kutoka 2,278, sawa na upungufu wa asilimia 18.42. Katambi amesema mafanikio hayo yametokana na juhudi za Jeshi la Polisi katika kuimarisha doria, kusimamia sheria za usalama barabarani na kuchukua hatua kwa wanaokiuka sheria. Serikali itaendelea pia kutoa elimu kwa umma kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii ili kupunguza zaidi ajali za barabarani.

Serikali Yaokoa Waathirika 160 Wa Usafirishaji Haramu wa Binadamu, Yakamata Watuhumiwa 57

Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi imeendelea kuongeza nguvu katika mapambano dhidi ya usafirishaji haramu wa binadamu, ambapo katika kipindi cha Julai 2025 hadi Aprili 2026 jumla ya waathirika 160 waliokolewa na kupewa msaada mbalimbali wa kijamii na kisheria. Akiwasilisha bajeti ya wizara hiyo Bungeni jijini Dodoma kwa mwaka wa fedha 2026/2027, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi amesema kati ya waathirika hao, watoto ni 60, wanawake 96 na wanaume 4. Ameeleza kuwa waathirika 126 waliokolewa ndani ya nchi na 34 waliokolewa kutoka mataifa mbalimbali yakiwemo Bahrain, India, Malaysia, Misri, Oman, Syria na Umoja wa Falme za Kiarabu. Katika hatua nyingine, jumla ya watuhumiwa 57 walikamatwa, ambapo 45 kati yao wamefikishwa mahakamani na kesi zao zinaendelea kusikilizwa katika mikoa mbalimbali nchini, huku 12 wakiendelea kuchunguzwa na vyombo vya dola. Aidha, Serikali imeendelea kuimarisha uwezo wa wadau wa haki jinai kupitia mafunzo maalum yaliyotolewa kwa washiriki 314 katik...

NIDA Yasajili Wananchi Milioni 27.1, 668,822 Bado Hawajachukua Vitambulisho

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi amesema Serikali kupitia Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) imeendelea kuimarisha mfumo wa usajili na utambuzi wa wananchi, ambapo hadi Aprili 2026 jumla ya watu 27,186,421 sawa na asilimia 86.4 ya lengo la kitaifa tayari wamesajiliwa na kutambuliwa. Akiwasilisha Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani kwa mwaka wa fedha 2026/2027 bungeni jijini Dodoma leo Mei 25, 2026, Katambi amesema kasi ya usajili imeongezeka ambapo katika kipindi cha Julai 2025 hadi Aprili 2026 pekee, NIDA ilisajili watu 1,145,334 wenye umri wa miaka 18 na kuendelea, ikilinganishwa na 844,994 katika kipindi kama hicho mwaka uliopita. Amesema mafanikio hayo yamechochewa na maboresho ya huduma pamoja na upanuzi wa wigo wa usajili, ikiwa ni sehemu ya kufikia lengo la sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022. Katika huduma kwa Watanzania waishio nje ya nchi, amesema jumla ya wananchi 156 wamesajiliwa kupitia balozi za Tanzania nchini Canada, Marekani, Uingereza na Umoja...

WATANZANIA 17 Waukana Uraia wao

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi amesema Watanzania 17 wameukana rasmi uraia wao baada ya kupata uraia wa mataifa mengine kwa mujibu wa Sheria ya Uraia Sura ya 357 ya mwaka 2023. Akiwasilisha bajeti ya wizara hiyo Bungeni jijini Dodoma leo Mei 25, 2026, Katambi amesema hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa sheria za uraia nchini. Aidha, amesema katika kipindi cha Julai 2025 hadi Aprili 2026, jumla ya wageni 64 walipewa uraia wa Tanzania baada ya kukidhi vigezo na taratibu zilizowekwa. Pia amesema Watanzania 203 wamerejeshwa nchini kutoka mataifa mbalimbali baada ya kukiuka sheria za nchi husika, ikiwemo kuingia au kuishi bila kufuata utaratibu wa kisheria.

KATAMBI:Zaidi ya Wahamiaji Haramu 34,099 Waondoshwa Nchini

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi amesema Serikali imeendelea kuimarisha mapambano dhidi ya uhamiaji haramu kupitia operesheni, misako, doria na ukaguzi unaofanyika katika maeneo mbalimbali Nchini.  Akiwasilisha Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi leo Mei 25, 2026 Bungeni Jijini Dodoma, Katambi amesema hadi kufikia Aprili 2026 jumla ya watuhumiwa 49,469 wa makosa ya kiuhamiaji walikamatwa, huku wahamiaji haramu 34,099 wakiondoshwa nchini baada ya kuchukuliwa hatua za kisheria. Katika kuimarisha usalama wa mipaka, Katambi amesema Idara ya Uhamiaji imeanzisha Kanda Maalum za Uhamiaji katika mikoa ya Kagera na Kigoma kwa kuongeza askari pamoja na vitendea kazi ili kudhibiti wahamiaji haramu. “Tutazidi kufanya misako, doria na kuanzisha kanda nyingine katika maeneo ya kimkakati yenye mwingiliano mkubwa wa wageni ili kuhakikisha wahamiaji haramu wanadhibitiwa ipasavyo,” amesema Katambi. Aidha, amesema kampeni ya “Mjue Jirani Yako” imeendelea kuleta matokeo chanya...