_Apongeza NIRC kwa kuimarisha uwezo kupitia mafunzo ya Usimamizi wa Mikataba, Sheria, Ununuzi na Utafiti wa Miamba_ 📍 NIRC – Iringa Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Mweli, amewataka Wahandisi wa Umwagiliaji nchini kuachana na kufanya kazi kwa mazoea na badala yake kutumia mbinu bunifu na uzoefu wa kitaalamu katika kusimamia miradi ya umwagiliaji, ili kuhakikisha miradi hiyo inaleta tija kwa Taifa. Akifungua mafunzo ya usimamizi wa mikataba, sheria za ununuzi na utafiti wa miamba katika mabwawa mkoani Iringa, Bw. Mweli aliwataka wahandisi kufuta dhana ya kukariri kwa kuwa usimamizi wa wakandarasi unahitaji mbinu za ziada na kubadilishana uzoefu miongoni mwa wataalamu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji na wadau wengine. “Utatuzi wa changamoto za miradi haujawahi kuandikwa wote kwenye makaratasi. Mara nyingine unakutana na mkandarasi mbishi, hapo ndipo unahitaji kuzungumza na mhandisi mwenzako aliyejua jinsi ya kumdhibiti. Msikae kama mnaogopana, kaeni pamoja mbadilishane mbinu z...
Marato tv - Sauti ya Jamii