Kutokana na utabiri wa mvua kubwa zinazotarajiwa kunyesha nchini katika kipindi hiki cha mvua za El Niño, Diwani wa Viti Maalum wa Manispaa ya Musoma,Mh Sister Yohana, amewakabidhi waendesha bodaboda wa Kata ya Mwisenge eneo la Mtakuja banda maalum la kujikinga na mvua na jua wanapokuwa wakisubiri abiria. Banda hilo limejengwa katika viwanja vya Shule ya Msingi Mtakuja, Manispaa ya Musoma, ikiwa ni hatua ya kuwawezesha vijana hao kuendelea na shughuli zao za usafirishaji bila kuathiriwa na hali ya hewa, hususan wakati wa mvua. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa banda hilo, Sister Yohana amesema ameamua kutekeleza ujenzi huo kwa kutambua umuhimu wa kuwaunga mkono vijana wanaotegemea shughuli za bodaboda kujipatia kipato na kuendesha maisha yao. “Mimi kama Diwani wa Viti Maalum nimeamua kuwajengea kivuli vijana wa bodaboda wa Mtakuja, ambao ni majirani kabisa na nyumbani kwangu. Nimefanya hivi kwa kutambua juhudi za Serikali chini ya Rais Samia Suluhu Hassan katika kuwajali na kuwawe...
Marato tv - Sauti ya Jamii