Na: Dk. Reubeni Lumbagala Nakumbuka mwalimu wangu wa somo la Uraia (Civics) alipokuwa akitufundisha mada (topic) ya "Haki za "Binadamu" (Human Rights) tulipokuwa Kidato cha Kwanza, alituambia mengi kuhusu haki za binadamu. Miongoni mwa mikazo yake, alituambia hivi: Haki ya kuishi (Right to life) ndiyo haki kubwa kuliko zote maana mtu anapokuwa hai ndipo anakuwa na uwezo wa kupata haki nyingine zote. Nilimwelewa vizuri sana. Kimsingi, uhai ni muhimu katika maisha ya mwanadamu, ndiyo maana inapotokea mtu ameugua, na akawa hana uwezo wa kumudu gharama za matibabu yake, basi familia, ndugu, jamaa na marafiki hushikamana kwa kuchangishana fedha kunusuru uhai wa ndugu yao huyo. Watoto ni kundi ambalo lipo hatarini kukabiliwa na magonjwa mbalimbali. Ni kutokana na msingi huo, serikali inajitahidi sana kutoa chanjo za magonjwa mbalimbali ili kuimarisha na kujenga afya zao ili kuwa na kinga ya kutosha ya kuweza kupambana na magonjwa. Taasisi ya Doris Mollel (DMF) ni wadau muhimu...
Marato tv - Sauti ya Jamii