Skip to main content

Posts

Showing posts from July 24, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

MZEE OTIENO IGOGO AMLILIA DKT ODEMBA

  Mfanyabiashara Maarufu Nchini, Otieno Olunga Igogo, ameeleza namna alivyoguswa kufuatia kifo cha shemeji yake, Dkt. Alex Seka Odemba, aliyefariki dunia katika Jimbo la Michigan nchini Marekani siku chache zilizopita. Akizungumza kuhusu tukio hilo, Mzee Igogo amesema kuwa familia imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo hicho, akieleza kuwa marehemu alikuwa nguzo muhimu ya familia, mtu mwenye busara, upendo na aliyekuwa mstari wa mbele kuimarisha mshikamano wa ndugu na jamaa. Aidha, Igogo ameeleza kuwa hakuna aliyedhani kuwa Dkt. Odemba angefariki katika kipindi ambacho alikuwa akijiandaa kufunga maisha yake nchini Marekani na kurejea Tanzania kuanza makazi mapya ambapo amesema siku moja kabla ya safari yake, marehemu alianza kujisikia vibaya kutokana na homa ya ghafla na kukimbizwa hospitalini, ambapo baadaye alifariki dunia. Pia, Ameongeza kuwa taarifa za msiba huo ziliishtua familia na marafiki waliokuwa wakiamini kuwa wangempokea Tanzania ndani ya muda mfupi. Badal...

SERIKALI MKOA WA TANGA KUTAFUTA SULUHISHO LA MGOGORO WA SHAMBA LA MANZA-BAY

 Na Mwanamkuu Mwandoro, Mkinga  Serikali imeendelea kuonesha dhamira yake ya kusikiliza maoni ya wananchi katika kutafuta suluhisho la kudumu la mgogoro wa Shamba la Manza-Bay, lililopo Kijiji cha Boma Kichakamiba, Kata ya Boma, Wilaya ya Mkinga, kwa kuahidi kuyafanyia kazi maoni yaliyotolewa kupitia taratibu za Serikali.  Kauli hiyo imetolewa Julai 24, 2026 na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Dkt. Balozi Batilda Burian, wakati wa kikao cha kusikiliza maoni ya wananchi kuhusu mgogoro huo. Amesema Serikali inatambua umuhimu wa kuwashirikisha wananchi katika maamuzi yanayogusa maisha yao na kwamba maoni yote yaliyotolewa yatapewa uzito unaostahili ili kufikia suluhisho la haki na la kudumu lenye kuzingatia maslahi ya wananchi pamoja na mwekezaji.  "Serikali imekuja kuwasikiliza wananchi. Maoni yenu ni sehemu muhimu ya mchakato wa kupata suluhisho la kudumu, na yatafanyiwa kazi kwa kuzingatia sheria, haki na maslahi ya pande zote," amesema Mhe. Dkt. Burian.  Kwa upande ...

MBUNGE DEVOTHA DANIEL: AMANI NI MSINGI WA MAENDELEO

Kagera.  Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kagera, Devotha Daniel, amewataka wananchi kuendelea kudumisha amani, umoja na mshikamano, akisisitiza kuwa utulivu wa nchi ndiyo nguzo inayowezesha Serikali kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo inayolenga kuboresha maisha ya Watanzania. Devotha alisema maendeleo makubwa yanayoonekana nchini, hususan katika sekta ya miundombinu, yamewezekana kutokana na mazingira ya amani na utulivu ambayo yameendelea kudumishwa na wananchi kwa kushirikiana na Serikali. "Tuendelee kuitunza amani ya nchi yetu, kwani maendeleo tunayoyaona leo yanatokana na utulivu uliopo. Bila amani, miradi mikubwa ya maendeleo isingeweza kutekelezwa kwa ufanisi," alisema Devotha. Mbunge huyo alitoa kauli hiyo wakati wa ziara ya Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, aliyefanya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa barabara ya Rusahunga–R...

WAFUGAJI WATAKIWA KUWA NAVIKUNDI VYA ULINZI SHIRIKISHI .

 Wafugaji na Wafanyabiashara wa Mifugo Katika Kijiji na Kata ya Mwimbi, Wilaya ya Kalembo Mkoani Rukwa wametakiwa kuungana na kuunda vikundi vya ulinzi shirikishi ambavyo vitasaidia kulinda mifugo, pamoja na kuwafichua wezi wa Mifugo Kijijini hapo. Akizungumza na Kusikiliza kero za Wafugaji na Wafanyabiashara hao wa Mifugo, leo Julai 24 2026, Kamanda wa Polisi Kikosi cha Kuzuia Wizi wa Mifugo Nchini (STPU) Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Simon Pasua, amesema kuwa wezi wa Mifugo wanatoka katika maeneo yao hivyo ni jukumu lao kuunda vikundi vya ulinzi shirikishi ambavyo vitasaidia kulinda mifugo hiyo, huku akikemea tabia ya kuwaficha wezi wa mifugo baina yao. SACP Pasua amesema kuwa Jeshi la Polisi litawasilisha katika mamlaka husika kero zote zilizoainishwa katika kikao hicho ikiwemo kuwekwa uzio katika eneo la mnada pamoja na uboreshwaji wa miundombinu muhimu, hatimaye kuboresha sekta ya biashara ya mifugo Nchini kwa manufaa yao na Taifa kwa Ujumla. Sambamba na hayo K...

MAKAMU WA RAIS AFUNGUA MKUTANO WA 15 WA MTANDAO WA WATETEZI WA HAKI ZA BINADAMU

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ana dhamira ya dhati ya kuhakikisha Katiba mpya inapatikana, ndio maana suala hilo limewekwa katika Ilani ya Chama Cha Mapinduzi pamoja na kuahidi kulitekeleza. Makamu wa Rais amesema hayo wakati akifungua Mkutano wa 15 wa Wanachama wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) uliyofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City, Jijini Dar es Salaam. Amesema suala hilo limejadiliwa tangu mwaka 1992 mara baada ya kuanza kwa vyama vingi, lakini Serikali ya Awamu ya Sita imeahidi kulitekeleza kwa manufaa ya wananchi. Amewasihi wananchi kuibeba ajenda hiyo kwa uzito mkubwa ili iweze kutekelezwa katika kipindi hiki. Aidha, Makamu wa Rais amesema ni muhimu kuzingatia suala la haki, kwani ndio msingi wa amani katika Taifa lolote lile. Amesema Serikali itaendelea na wajibu wa kuhakikisha wananchi wanaishi kwa usalama bila hofu. Vil...

DC LUBELA APONGEZA UZALENDO WA FORTUNATUS MAGAMBO, ARIDHISHWA NA UJENZI WA MADARASA MATANO SHULE YA MSINGI RING'WANI

 Mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Wakili Angelina Marco Lubela, ameonyesha kuridhishwa kwake na ubora wa ujenzi wa vyumba vitano vya madarasa katika Shule ya Msingi Ring'wani, iliyopo Kijiji cha Nyamatare, Kata ya Nyamatare, huku akimpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Fortunatus Makore Magambo, kwa moyo wake wa kizalendo na kujitolea kuunga mkono maendeleo ya elimu nchini. Mhe. Lubela ametoa pongezi hizo wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya mradi huo, uliofadhiliwa na Magambo kwa lengo la kusaidia Serikali kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia, pamoja na kuondoa changamoto ya uhaba na uchakavu wa vyumba vya madarasa uliokuwa ukiikabili shule hiyo kwa muda mrefu. Akizungumza baada ya ukaguzi, Mkuu huyo wa Wilaya amesema ameridhishwa na kiwango cha ubora wa ujenzi huo, akieleza kuwa madarasa hayo yamejengwa kwa viwango vinavyokidhi mahitaji ya wanafunzi na walimu, na kwamba yatakuwa chachu ya kuinua kiwango cha taalu...

SERIKALI KUENDELEA KUFUNGUA FURSA ZA UWEKEZAJI SEKTA YA MADINI

 ▪️ Dkt. Mwanga: Changamoto za mitaji na teknolojia zitatatuliwa MWANZA Kamishna wa Madini nchini, Dkt. Abdulrahman Mwanga, amesema Serikali kupitia Wizara ya Madini itaendelea kutatua changamoto zinazoikabili Sekta ya Madini kwa kuweka mazingira rafiki kwa wawekezaji ili kuongeza uzalishaji, mapato ya Serikali kuongezeka na mchango wa sekta hiyo kuendelea kukua katika uchumi wa Taifa. Dkt. Mwanga ameyasema hayo mapema leo Julai 24, 2026, wakati akifunga Jukwaa la Tano la Utekelezaji wa Ushirikishwaji wa Watanzania katika Sekta ya Madini (LCCF 2026), lililofanyika jijini Mwanza kuanzia Julai 22 hadi 24, mwaka huu. Amesema Serikali imeweka mikakati ya kujenga Sekta imara ya Madini kwa kufungua fursa zaidi za uwekezaji na kuendelea kutafuta suluhisho la changamoto za mitaji na teknolojia zinazowakabili wadau, hatua inayolenga kuongeza tija na kuhakikisha Sekta ya Madini inakuwa nguzo muhimu ya uchumi wa nchi. “Sekta ya Madini ni miongoni mwa sekta muhimu zilizopewa kipaumbele katika ...

AFRIKA KUUNGANA KUCHOCHEA MAENDELEO YA VIWANDA

 Na. Mwandishi Wetu ABIDJAN:Naibu Waziri wa Fedha, Mhandisi Mshamu Ali Munde, kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar, ameongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Pamoja wa 9 wa Kamati Maalum ya Mawaziri (STC) ya Umoja wa Afrika inayoshughulikia Fedha, Uchumi, Mipango na Mtangamano, pamoja na Mkutano wa 5 wa Kamati ya Mawaziri wa Biashara, Utalii, Viwanda na Madini. Mkutano huo wa kimkakati ulioanza rasmi tarehe 24 Julai 2026 jijini Abidjan, Côte d’Ivoire, unalenga kuweka misingi imara ya ushirikiano wa kiuchumi barani Afrika. Mkutano huo umejadili kwa kina umuhimu wa nchi za Afrika kuharakisha juhudi za kuendeleza sekta ya viwanda kwa kuongeza thamani ya malighafi za ndani badala ya kusafirishwa zikiwa ghafi, kuimarisha minyororo ya thamani ya kikanda, pamoja na kuweka mazingira bora na wezeshi yatakayovutia uwekezaji wenye tija kiuchumi. Wajumbe wa mkutano huo walibainisha kuwa, kutokana na Bara la Afrika kuwa na rasilimali nyingi za asili, ardhi kubwa yenye rut...

WASIRA AONGEZA KASI YA USIMAMIZI WA UJENZI WA OFISI YA KISASA YA CCM BUNDA

 Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Mzee Stephen Masato Wasira, ameendelea kuonyesha dhamira yake ya kuhakikisha miradi ya maendeleo ya Chama inatekelezwa kwa ufanisi baada ya kufanya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa Ofisi ya Kisasa ya CCM Wilaya ya Bunda, mkoani Mara. Mradi huo ulioanza kutekelezwa mwezi Februari 2026 unagharimu zaidi ya shilingi milioni 700 na hadi sasa umefikia takribani asilimia 90 ya utekelezaji.  Ujenzi huo unasimamiwa na Ofisi ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bunda, huku ukilenga kujenga mazingira bora na ya kisasa yatakayorahisisha utekelezaji wa shughuli za Chama katika wilaya hiyo. Akizungumza baada ya kukagua maendeleo ya mradi huo, Mzee Wasira amesema ameridhishwa na kasi ya ujenzi, lakini amesisitiza kuwa jambo muhimu zaidi ni kuhakikisha kazi zote zinazobaki zinakamilishwa kwa ubora wa hali ya juu na ndani ya muda uliopangwa. "Ninatarajia ifikapo mwezi Agosti 2026...