WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji, ametoa onyo kali kwa watu wanaovamia maeneo ya hifadhi nchini, akisisitiza kuwa serikali haitasita kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya wote watakaobainika kuhusika na uharibifu wa maliasili. Waziri Kijaji ameyasema hayo leo Juni 25, 2026 jijini Dodoma Katika Mkutano wa Mwaka wa Wahifadhi Wanyamapori, unaofanyika chini ya kauli mbiu isemayo “Uhifadhi Endelevu kwa Ustawi wa Jamii na Maendeleo ya Taifa katika Utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050.” Akizungumza katika mkutano huo, Waziri Kijaji amesema sekta ya uhifadhi inaendelea kukabiliwa na changamoto kubwa zinazohitaji ushirikiano wa wadau wote ili kuhakikisha rasilimali za taifa zinalindwa kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho. Amesema moja ya changamoto kubwa ni ongezeko la migongano kati ya binadamu na wanyamapori wakali na waharibifu, hali inayosababisha uharibifu wa mashamba, makazi na mifugo, hususan katika maeneo ya vijijini. Ameeleza kuwa hali hiyo inachangiwa zaidi ...
Marato tv - Sauti ya Jamii