Skip to main content

Posts

Showing posts from March 9, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Kata ya Etaro Jimbo la Musoma Vijijini Waendelea na Ujenzi wa Sekondari ya Tatu

  Na Shomari Binda-Musoma  KASI ya ujenzi wa shule mpya za sekondari katika jimbo la Musoma Vijijini umezidi kushika kasi kubwa ili kuongeza idadi ya shule na kutoa fursa ya ukaribu wanafunzi kupata elimu. Kufuatia hilo wananchi wa Kata ya Etaro Kijiji cha Mmahare wameanza ujenzi  wa msingi wa madarasa ya shule mpya ya sekondari ikiwa shule ya tatu kwenye Kata hiyo. Leo machi 10/ 2025 mbunge wa jimbo la Musoma vijijini Profesa Sospeter Muhongo amekabidhi kamati ya ujenzi wa shule hiyo mifuko 50 ya saruji kati ya mifuko 155 aliyoahidi kuendelea na ujenzi na watakabidhiwa mingine kadri wanavyotumia. Hivi karibuni mbunge wa jimbo aligawa saruji mifuko 150 kwa kila kijiji kinachojenga sekondari mpya fedha za saruji hiyo ni zile za mfuko wa jimbo Profesa Muhongo wakati akikabidhi mifuko ya saruji Kijiji cha Mmahare Kata ya Etaro amekipongeza na kukipa hongera kwa kasi nzuri ya ujenzi na tayari kimetumia mifuko yote 150. " Nipongeze kasi kubwa ambayo inafanywa na wananchi wa Ki...

Nyambari Nyangwine Kuibadili Tarime kuwa Kisiwa cha Amani

-Achangisha milioni 45.6 KMT Mangucha, SDA Nyabitoche NA MWANDISHI WETU, Tarime Mfanyabiashara maarufu nchini na mkazi wa Tarime Nyambari Nyangwine ameendesha harambee katika Kanisa la Mennonite Tanzania (KMT) lililopo kijiji cha Mangucha katika kata ya Nyanungu wilayani Tarime na kufanikisha kupatikana kwa shilingi zaidi ya milioni 27. Katika harambee hiyo iliyofanyika kanisani hapo machi 9 mwaka 2025, Nyambari ambaye amewahi kuwa mbunge wa jimbo la Tarime amechangia shilingi milioni 10,huku akisindikizwa na rafiki zake, wakiwemo madiwani kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Tarime Vijijini Diwani wa Kata ya Nyanungu, Tiboche Richard alishiriki katika harambee hiyo ya kuchangia ujenzi wa kanisa hilo. Aidha Nyambari aliahidi kutoa kiasi cha shilingi milioni 12 kwa ajili ya kuchangia makanisa mbalimbali yaliyopo katika kata hiyo kwa lengo la kutaka nyumba hizo za Mungu zitumike kuleta mabadiliko hasa katika kusimamia amani kws maelezo ndio msingi wa Maendeleo. “Mimi ni mzaliwa wa kata hii, n...

Serikali Kutatua Changamoto ya Umeme Kwa Mikoa ya Kaskazini Kwa Kutumia Umeme wa Ethiopia

Na Mwandishi Wetu Serikali imesema kuwa inaendelea na mpango wa kununua umeme kutoka nje ya nchi kwa ajili ya Kanda ya Kaskazini ili kupunguza upotevu mkubwa wa umeme unaosababishwa na usafirishaji wa nishati hiyo kutoka Gridi ya Taifa, hali inayosababisha hasara ya zaidi ya shilingi bilioni 32 kwa mwaka. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Idara ya Habari – MAELEZO na Ofisi ya Msemaji Mkuu wa Serikali, umeme uliopo kwenye Gridi ya Taifa unazalishwa zaidi katika Ukanda wa Kusini Mashariki, hivyo hulazimika kusafirishwa umbali mrefu hadi Kanda ya Kaskazini, jambo linalosababisha upotevu mkubwa wa nishati hiyo. “Kwa sasa, upotevu wa umeme unaosafirishwa kuelekea Kanda ya Kaskazini unasababisha hasara kubwa kwa Taifa, na moja ya njia mbadala ya kutatua changamoto hiyo ni kununua umeme kutoka Ethiopia kupitia Kenya,” imesema taarifa hiyo. Imeelezwa kuwa hatua hiyo itasaidia kupunguza changamoto ya kukatika kwa umeme mara kwa mara katika Kanda ya Kaskazini na kuimarisha upatikanaji wa nish...

WAZIRI MKUU AWASIHI VIONGOZI WA DINI KUKEMEA VITENDO VINAVYOASHIRIA MMOMONYOKO WA MAADILI  

  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewasihi viongozi wa dini nchini waendelee kukemea vikali vitendo vyote ambavyo ni kinyume na maadili ya dini na utamaduni wa Mtanzania. "Ninawaomba viongozi wetu wa dini tuendelee kuliweka suala la kuimarisha malezi na kidhibiti mmomonyoko wa maadili kuwa ajenda ya kudumu. Lazima tuwe na maadili mema ili Taifa liwe endelevu". Ametoa rai hiyo leo (Jumapili Machi 9, 2025) alipomwakilisha Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika ibada ya kuwekwa wakfu na kutawazwa kwa Askofu wa Pili wa kanisa la Anglikana Dayosisi ya Kiteto, Askofu Bethuel Mlula iliyofanyika anisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Mikaeli, Kiteto Mkoani Manyara. Aidha, Waziri Mkuu amesema pamoja na masuala ya kiroho amewaomba viongozi wa dini waendelee kuwahamasisha waumini kuunga mkono ajenda mbalimbali za kitaifa, ikiwemo ya uhifadhi wa mazingira, kampeni ya nishati safi na upandaji miti pamoja na kushiriki katika hatua zote za uchaguzi mkuu wa mwaka 2025. Katika hatua nyingi...

Tundu Lissu afika nyumbani kwa marehemu prof Sarungi

Mhe.Tundu Antpas Lissu, Mwenyekiti CHADEMA Taifa amefika nyumbani kwa Marehemu Prof. Philimon Sarungi kusaini kitabu cha maombolezo na kutoa faraja kwa Mama Maria Sarungi-Tsehai.

Mafanikio ya Rais Samia kuileta Dunia, Tanzania

  -  Ni Uwekezaji baina ya Taasisi za Kitanzania. Na Mwandishi wetu, Arusha Viongozi mbalimbali wamempogeza Mhe. Dkt. Samia SuluhuHassani, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwakuridhia na kuelekeza fedha kwa ujenzi wa kituo cha Mikutano Cha kimataifa cha Mlima wa Kilimanjaro kitakachojengwa jijini Arusha. Kituo hicho cha aina yake Afrika, ambacho kinajengwa kwa ubia baina ya Taasisi ya Kituo cha Mikutano Cha Kimataifa Arusha (AICC ) na Taasisi ya Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) ujenzi wake utakamilika ndani ya miaka miwili. Pongezi hizo zimetolewa Machi 8, 2025 jijini Arusha wakati wahafla ya utaiji saini hati ya makubaliano ya Ujenzi baina ya wabia PSSSF na AICC.  Akizungumza mbele ya waalikwa waliohudhuria Shughuli hiyo , Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Pindi Chana ambaye wizara yake ni mmoja wa mdau muhimu sana katika matumizi ya Kituo hicho, alisema wizara ya Utalii inatoa shukrani na pongezi za dhati kwa Mheshimiwa Rais kwa kuelekeza...