Skip to main content

Posts

Showing posts from May 28, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Tanroads,Tarura Mara Waahidi Kuvipa Kazi Vikundi Utunzaji Barabara

  Na Shomari Binda-Musoma  WAKALA wa Barabara Vijijini na Mijini( TARURA) na Wakala wa Barabara Nchini( TANROADS) mkoa wa Mara wameahidi kutoa kazi kwa vikundi vitakavyosajiliwa kwaajili ya kutunza na kuhudumia barabara. Kauli hiyo imetolewa na Meneja wa TARURA mkoa wa Mara Mhandisi William Lameck alipokuwa akifunga mafunzo ya siku 14 kwa wanawake,vijana na makundi maalum watakao hudumia barabara. Amesema mafunzo hayo yamekuja wakati muafaka kwa mkoa wa Mara katika kuhakikisha wanashirikiana kutunza na kulinda barabara. Meneja huyo wa TARURA mkoa wa Mara amesema serikali inatumia fedha nyingi kwaajili ya ujenzi wa barabara hivyo ni muhimu kuwa na matunzo shirikishi. Amesema serikali katika bajeti zake kwenye ujenzi wa barabara inawekwa asilimia 30 zaidi ya milioni 300 kwaajili ya vikundi vya kijamii vya kuhudumia barabara. Mhandisi William amesema watu 86 waliopata mafunzo hayo wanapaswa kuchangamkia fursa na kuanzisha vikundi kwa haraka ili waweze kupata kazi na kujipatia kip...

Waendesha Bajaj na Bodaboda Dodoma Kunufaika Na Programu ya Gurudumu la Mama

▪️Vijana kupatiwa fursa ya kupata vifaa vya pikipiki na Bajaj kwa unafuu ▪️Vijana zaidi ya 2000 kunufaika na awamu ya kwanza ya Progamu ▪️RC Senyamule awataka kuzingatia sheria ili kupunguza ajali ▪️Mbunge Mavunde awawezesha kufungua SACCOS Dodoma Wasafirishaji abiria kupitia pikipiki na Bajaj Jijini Dodoma wanategemea kunufaika na programu ya 𝙂𝙪𝙧𝙪𝙙𝙪𝙢𝙪 𝙡𝙖 𝙈𝙖𝙢𝙖 inayoratibiwa na kampuni ya RoadMaster kwa lengo la kusaidi upatikanaji wa matairi mapya kwa Bajaj na Bodaboda katika mfumo rahisi ambao utawawezesha kundi hili kubwa la wasafirishaji kupata vitendea kazi kwa urahisi na kwa muda mfupi. Hayo yamesemwa jana Jijini Dodoma wakati wa uzinduzi wa Programu ya 𝙂𝙪𝙧𝙪𝙙𝙪𝙢𝙪 𝙡𝙖 𝙈𝙖𝙢𝙖 iliyozinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mh. Rosemary Senyamule. Akitoa maelezo ya programu,Mkurugenzi wa RoadMaster na Mratibu wa Progamu hii Ndg. Thuwein Makamba amesema lengo kubwa la programu hii ni kuwawezesha wasafirishaji kuwa na matairi yenye ubora ili kusaidia kupunguza ajali zi...

Waziri Mkuu Majaliwa Akutana na Waziri Mkuu wa Japan

_▪️Asema Japan itaendelea kuimarisha ushirikiano na Serikali ya Tanzania_ _▪️Aagiza tathmini ya barabara za Kibiti-Lindi na Morogoro-Dodoma_ WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amekutana na Waziri Mkuu wa Japan, Ishiba  Shigeru ambaye amemuhakikishia kuwa nchi hiyo itaendelea kuimarisha ushirikiano na Tanzania jambo ambalo linalenga kuchochea ukuaji wa uchumi kutokana na fursa zitakazoendelea kupatikana kupitia mahusiano hayo. Amekutana na kiongozi huyo leo (Alhamisi, Mei 29, 2025) katika ofisi ya Waziri Mkuu Tokyo, Japan, ambapo Mheshimiwa Majaliwa amesema ahadi hiyo inazidi kutoa fursa ya wawekezaji na wafanyabiashara wa Japan pamoja na Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (JICA) kuendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo. Mheshimiwa Majaliwa ametumia fursa hiyo kumueleza Waziri Mkuu huyo kuwa  pamoja na miradi mingine wanayotekeleza nchini, Japan kupitia JICA iangalie uwezekano wa kushirikiana na Serikali ya Tanzania kuzifanyia ukarabati mkubwa barabara za Mo...

Wanachuo Mipango Mwanza wafundwa matumizi sahihi ya mitandao

Kaimu Mratibu wa Polisi Jamii Wilaya ya Magu, Mkaguzi Msaidizi wa Polisi, Magazine Msaidizi wa Polisi Makoye Kitula, ametoa wito kwa wanafunzi wa Chuo cha Mipango kituo cha Mafunzo Mwanza kilichopo Kata ya Kisesa, wilayani Magu kuzingatia matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii na simu za mkononi kwa ajili ya maendeleo yao binafsi na taifa kwa ujumla. Mkaguzi Kitula ametoa wito huo Jana Jumatano Mei 28, 2025 ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa mikakati ya Jeshi la Polisi kupitia dhana Polisi Jamii katika kutoa elimu kwa makundi mbalimbali ili kuzuia na kupambana na vitendo vya uhalifu vinavyohusishwa na matumizi mabaya ya teknolojia. Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Chuo hicho, Dkt Grace Benedict, amelishukuru Jeshi la Polisi kwa kuona umuhimu wa kuwafikia wanafunzi kwa elimu hiyo, akibainisha kuwa ni muda muafaka kwani vijana wengi wamekuwa wakitumia mitandao ya kijamii isivyofaa na kujikuta wakikumbana na matatizo ya kisheria au kijamii.  Ameomba elimu hiyo iwe endelevu ili kusai...

Museveni na Mkewe waomba radhi kwa makosa waliyotenda miaka 39 ya uongozi wao

RAIS wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni pamoja na mkewe Janet Museveni,wameomba msamaha kwa wananchi wa Uganda kwa makosa ambayo wametekeleza katika kipindi cha miaka 39 ya uongozi wao. Kwenye Video ambayo ilipakiwa na NTV Uganda, wawili hao walionekana kuwa wanyenyekevu na kuonyesha huruma kwa kuomba msamaha huo, wakiwa kwenye jukwaa.  “Kama viongozi wa juu katika taifa hili, kwa unyenyekevu tunachukua jukumu la kuwajibikia makosa yote yaliofanywa na sisi wenyewe, mawakala wetu na wawakilishi wetu… Tunasimama hapa kutubu na kuwaomba msamaha, hasa watu wa Buganda na wananchi wote,” walisoma kwa pamoja ujumbe wao. Hata hivyo, wachanganuzi hawakukosa kuchambua kwamba huku Museveni akiomba radhi kwa makosa yakijumuisha ukatili kwa wananchi, mwananchi mmoja hasa, mwanasiasa wa Upinzani Kizza Besigye angali anahangaika jela baada ya kukamatwa kikatili akiwa Nairobi na kusafirishwa Uganda. Katika kipindi fulani majuma kadhaa yaliyopita, picha cha kudhoofika kiafya kwa mpinzani huyo ambaye ...

Mwandishi, mwanamageuzi mtajika Ngugi wa Thiong’o aaga dunia

Mwandishi wa Riwaya  mtajika duniani na mwanamageuzi Ngugi wa Thiong’o  ameaga dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu  nchini Marekani, familia yake imethibitisha. Bw Ngugi ambaye anachukuliwa kuwa mwandishi mahiri zaidi wa riwaya Afrika Mashariki amekuwa nchini Marekani kwa miaka mingi na katika miaka ya hivi punde amekuwa akilemewa na maradhi. Ripoti zinasema alikufa kwa mshtuko wa moyo. Mwanawe, Mukoma wa Ngugi, aliandika kwenye safu yake mtandaoni: “Nimejawa na majonzi kusema kwamba babangu, Ngugi wa Thiong’o alikata roho Jumatano, Mei 28, 2025,Ningekuwa mimi nilivyo kama mwanawe, msomi na mwandishi bila yeye. Nampenda. Sijui itakavyokuwa kesho. Hayo tu ndio naweza kusema kwa sasa"

Waziri Ridhiwani Kikwete akutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Ubalozi wa Jamhuri ya Watu wa China ukiongozwa na Balozi wa China Nchini Balozi Chen Mingjian

Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu,Kazi,ajira,Vijana na Wenye ulemavu Ridhiwani Kikwete amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Ubalozi wa Jamhuri ya Watu wa China ukiongozwa na Balozi wa China Nchini Balozi   Chen Mingjian Ofisini, Dodoma. Balozi Mingjian alitumia kikao hicho kujitambulisha na kuendelea kuimarisha mahusiano baina ya nchi ya China na Tanzania. Aidha alikumbusha maeneo muhimu ya ushirikiano haswa katika mafunzo ya kujenga ujuzi na ufundi huku msisitizo mkubwa ukiwa kuwaandaa vijana watakaopambana na mabadiliko makubwa ya kidunia hasa katika mapinduzi ya Teknolojia.  Kwa upande wake, Waziri Kikwete amemuhakikishia Balozi Mingjian na Ujumbe wake kuwa Tanzania itaendelea kuenzi uhusiano uliopo baina yake na China sanjari na kuendeleza uhusiano huo kwa kuimarisha maeneo yote ya mashirikiano hayo.   Pia Waziri Kikwete ameishukuru serikali ya China kwa mabadiliko makubwa ambayo yanaelekea kukuza ujuzi kwa vijana wa Kitanzania na nia yao ya kufany...

Majaliwa Kukutana na Waziri Mkuu na Japan

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Mei 29, 2025 anatarajia kukutana na Waziri Mkuu wa Japan Ishiba Shigeru, kwenye Ofisi ya Waziri Mkuu iliyopo Tokyo nchini Japan. Mazungumzo yao yatalenga kuimarisha uhusiano wa kidiomasia na uchumi kati ya nchi hizo mbili.

Makamu wa Rais ateta na Bosi wa AFDB

 Na Ada Ouko, GMTV. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) anayemaliza muda wake Dkt. Akinumwi Adesina.  Kando ya Mkutano wa Mwaka wa Bodi ya Magavana wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) unaofanyika katika Hoteli ya Sofitel Ivoire Jijini Abidjan nchini Ivory Coast.