Na Shomari Binda-Musoma VIONGOZI wa dini mkoa wa Mara kupitia kamati ya amani na maridhiano wamesema wapo tayari kushirikiana na taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ( TAKUKURU) kuelimisha Jamii kuhusu Rushwa hususani Katika Kipindi Cha uchaguzi. Wakizungumza kwa nyakati tofauti kwenye kikao kilichofanyika agosti 13 kwenye ofisi za Takukuru na kuwashirikisha viongozi wa dini,wazee na maafisa wa taasisi hiyo wamesema kikao hicho kimekuja wakati muafaka. Wamesema suala la rushwa linakatazwa hata kwenye vitabu vya dini na wao wapo tayari kuwahubiri waumini juu ya athari za Rushwa. Mwenyekiti wa Kamati ya Amani na Maridhiano ya viongozi wa dini mkoa wa Mara Jacob Rutubija ameishukuru Takukuru mkoa wa Mara,kwa kuwaona viongozi wa dini kuwa wanayo nafasi kubwa kwenye mapambano dhidi ya Rushwa. Shekh wa mkoa wa Mara ambaye ni mjumbe wa kamati hiyo amesema viongozi wa dini wanao watu wengi na ujumbe watawafikishia juu ya athari kwenye uchaguzi. Kiongozi wa itifaki wa kamati ya amani na mar...
Marato tv - Sauti ya Jamii