Skip to main content

Posts

Showing posts from April 30, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Serikali kutambulisha Leseni mpya maalum ya uzalishaji chumvi

  ▪️Waziri Mavunde aelekeza mchakato wa mabadiliko ya sheria kuanza. ▪️Aelekeza kanuni kubadilishwa kupunguza tozo kwa hekta kufikia 20,000. ▪️Wazalishaji Chumvi wampongeza Rais Dkt. Samia S. Hassan kwa ujenzi wa kiwanda cha Chumvi Mkoani Lindi ▪️Serikali kuwezesha wazalishaji chumvi kumiliki viwanda vya kuchakata chumvi *Dodoma* Serikali ipo mbioni kutambulisha Leseni mpya ya uzalishaji wa chumvi ili kuiondoa chumvi katika kundi la madini mengine na hivyo kuchochea ukuaji wa tasnia ya uzalishaji chumvi nchini Tanzania. Hayo yamesemwa leo Jijini Dodoma wakati wa Kikao cha Waziri wa Madini Mh. Anthony Mavunde na Uongozi wa Chama cha Wazalisha Chumvi Tanzania(TASPA),kikao ambacho kimelenga kuboresha sekta ya madini kupitia tasnia ya chumvi. “ Mh. Rais Dkt. Samia S. Hassan ametupa maelekezo mahsusi kuwezesha wachimbaji wa madini na wazalishaji wa madini chumvi nchini ili kuchochea ukuaji wa sekta ya madini. Serikali imesikia kilio chenu cha muda mrefu cha uwepo wa Leseni moja ya uzali...

Ahsante Dk. Doto Biteko kwa kutukumbusha umuhimu wa watu maishani

  Dk. Reubeni Lumbagala  Katika haya maisha, binafsi yangu nimeamua kujifunza kwa yeyote bila kujali dini, itikadi ya kisiasa, kabila, umri, jinsi ili mradi analo funzo la kunisaidia. Ndiyo, nimeamua hivyo kwani nimegundua kujifunza ni suala endelevu na kila siku kunahitajika kujifunza mambo mapya kutoka kwa watu mbalimbali.  Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko, ni moja ya walimu wazuri wa falsafa za maisha na siasa, na binafsi nimejifunza mengi kutoka kwake na naendelea kujifunza. Mara kadhaa nimeandika makala kumuhusu yeye kutokana na hotuba nzuri anazozitoa kwa viongozi na wananchi kwa ujumla. Moja ya hotuba yake nzuri aliyoitoa hivi karibuni ni ile yenye kichwa cha habari "Watu Ni Walewale." Ndugu msomaji wangu, kama umeisikiliza vyema hotuba hiyo, basi utakuwa umeelimika vya kutosha, lakini funzo kubwa ni kuhusu kuheshimu na kuthamini watu kwani katika maisha tunahitajiana ili kukamilishana, na kufanya maisha yaende vizuri.  Kimsingi, hakuna ...

Kikwete atoa taarifa kwa Waziri Mkuu maandalizi Mei Mosi yamekamilika 100%Rais Samia mgeni rasmi

  Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu -Ridhiwani Kikwete ametoa taarifa kwa Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa ya ukamilifu na utayari wa kilele cha Sherehe za Mei Mosi zinazotarajiwa kufanyika kesho Mei Mosi katika Viwanja vya Bombadier, Manispaa ya Singida. Akizungumza baada ya ukaguzi na kupokea taarifa, Waziri Mkuu ameeleza kuridhishwa na maandalizi na kupongeza maandalizi yaliyofanyika ambapo ameeleza kuwa na viwango vikubwa sana kuliko kupata kutokea. Wafanyakazi wote wanakaribishwa wananchi wote kuja kusherehekea mafanikio ya miaka minne ya Rais Samia Suluhu Hassan, ambapo pia Rais Samia anatarajiwa kuwa Mgeni rasmi.

Rc Mtambi aipongeza Azania Benk ikitoa mchango wa meza na viti 300 kwa shule za sekondari Musoma mjini j

  Na Shomari Binda-Musoma MKUU wa mkoa wa Mara Kanali Evans Mtambi  ameipongeza Benki ya Azania kwa kutoa meza na viti 300 kwa shule za sekondari katika jimbo la Musoma mjini. Meza na viti hivyo vimetolewa na benki hiyo leo aprili 30 2025 kwenye uwanja wa shule ya msingi Mukendo katika kuunga mkono juhudi za serikali na kutimiza ombi la mbunge wa Jimbo la Musoma mjini Vedastus Mathayo. Mkuu huyo wa mkoa amesema mchango wa benki hiyo kwenye sekta ya elimu ni jambo muhimu ambalo linapaswa kuungwa mkono na wadau wengine. Licha ya kuipongeza na kuishukuru benki hiyo ameishukuru pia taasisi ya Nyansaho Foundation ambao pia wameahidi kuchangia upatikanaji wa madawati, meza na viti kwaajili ya shule za jimbo la Musoma mjini. Amesema taasisi hiyo imekuwa mstari wa mbele kuchangia maendeleo na sio kwa jimbo la Musoma mjini pekee bali mkoa mzima wa Mara. " Hapa nimepokea madawati,viti na meza jumla ya 600 kutoka kwa mbunge Mathayo,Azania benki napenda kuwapongeza sana na kuwashukuru. "...

Wafungwa na Mahabusu kusikiliza kesi kwa Mahakama Mtandao ni sababu za kiusalama - Bashungwa

  📌Atoa maelekezo kufuatia matamko ya CHADEMA.  📌Asema hakuna ‘VIP treatment’ kwa wanaotaka kuwaona Wafungwa na Mahabusu. 📌Aagiza Jeshi la Polisi kudhibiti maandamano na matishio ya kiusalama. Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amesema kuwa Jeshi la Magereza kwa kushirikiana na Mahakama ya Tanzania litaendelea kuwawezesha Wafungwa na Mahabusu kusikiliza mashauri yao wakiwa magerezani kupitia Mahakama Mtandao, hasa kunapokuwepo na viashiria vya matishio ya kiusalama, ili kudumisha amani na kulinda usalama wa raia na mali zao. Ameeleza kuwa mojawapo ya sababu ya kuendelea kutumia Mahakama Mtandao ni masuala ya kiusalama, ambapo hivi karibuni baadhi ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wametoa matamko yanayoashiria uvunjifu wa amani na usalama, hali iliyosababisha baadhi ya Wafungwa na Mahabusu kusikiliza mashauri yao kwa njia ya mtandao. Bashungwa ameyasema hayo leo, tarehe 30 Aprili 2025 jijini Dodoma, alipoambata na Kamati ya Bunge ya...