Skip to main content

Posts

Showing posts from February 1, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Naibu Katibu Mkuu Aagiza Ujenzi Wa Barabara Za Tactics Jijini Arusha Ukamilike

Arusha NAIBU Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tamisemi anayeshughulikia Miundombinu Mhandisi Rogatus Mativila ameagiza wakandarasi wanaojenga barabara za Engosheraton, Olasiti na Oljoro patakapojengwa stendi mpya ya mabasi kwa Jiji la Arusha zikamilike kwa wakati. Agizo hilo lilitolewa Jijini hapa na Mhandisi Mativila wakati alipotembelea barabara hizo tatu zenye urefu wa kilomita 12.1 kupitia Mradi wa Kuboresha Miji (TACTIC) uliopo chini ya TARURA. Alisema barabara hizo tatu za Engosheraton, Olasiti na Oljoro zenye thamani ya shilingi bilioni 15.4 zinajengwa kwa kiwango cha lami lakini bado ukamilishwaji wake upo nje ya muda. Akizungumza mara baada ya kutembelea barabara hizo Mhandisi Mativila alisema ziara hiyo ni ya kawaida katika kuangalia maendeleo ya kazi zinazofanywa katika ujenzi wa barabara hizo. “Ujenzi wa barabara ya Oljoro bado upo nyuma kwa asilimia 35 kutokana na kubadilishwa kwa mchoro(dizaini) kutokana na kiwango chake cha usanifu na kuwa barabara ya Mkoa kutokana na ujenzi...

Wanafunzi waliopata Division One St Mary’s wapewa tuzo

Na Mwandishi Wetu WANAFUNZI 30 wa shule ya St Mary’s Mbezi waliopata daraja la kwanza kwenye matokeo ya kidato cha nne  mwaka huu wamepewa zawadi mbalimbali zikiwemo fedha taslim na kwenda kutalii Mbuga ya Mikumi. Hafla ya kuwapa zawadi wanafunzi hao ilifanyika mwishoni mwa wiki shuleni hapo na kushuhudiwa na wazazi wa wanafunzi hao walimu na uongozi wa shule za St Mary’s. Akizungumza kwenye hafla hiyo, Mkuu wa shule ya sekondari Mbezi, Reca Ntipoo alisema kwenye mtihani wa kidato cha nne wanafunzi 30 wa shule hiyo walipata daraja la kwanza, wanafunzi 66 daraja la pili na wanafunzi 42 walipata daraja la tatu. “Tofauti yetu na shule zingine ni kwamba sisi  hatuchukui wanafunzi wenye uwezo mkubwa sana tunachukua wanafunzi bila kubagua uwezo wao darasani tunawafundisha mpaka wanapata daraja la kwanza au la pili,” alisema “Kwa hiyo tuliposajili wanafunzi wengi baadhi ya viongozi waliogopa lakini tuliwaambia msiwe na wasiwasi walimu wetu wako vizuri sana watafaulu na leo hii najisi...

Rais Samia Apewa Tuzo Maalum Kutokana na Mchango Wake Katika Sekta ya Elimu Nchini

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea tuzo Maalum kuhusu maono na mchango wake kwenye sekta ya Elimu kutoka kwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Adolph Mkenda wakati wa hafla ya uzinduzi wa Sera ya Elimu na Mafunzo kwa mwaka 2014, toleo la 2023 katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma tarehe 01 Februari, 2025. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikagua mabanda ya maonesho kuhusu masuala mbalimbali ya Elimu kabla ya kuzindua Sera ya Elimu na Mafunzo kwa mwaka 2014, toleo la 2023 katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma tarehe 01 Februari, 2025. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisaini bango maalum lenye ujumbe kuhusu Elimu mara baada ya kukagua mabanda ya maonesho ya masuala ya Elimu katika viwanja vya ukumbi wa mikutano ya Jakaya Kikwete Jijini Dodoma tarehe 01 Februari, 2025. Matukio mbalimbali wakati wa hafla ya uzinduzi...

Uboreshaji Wa Miundombinu Wachagiza Ongezeko la Wageni Saadani

Na. Edmund Salaho - Saadani. Kamishna wa Uhifadhi TANAPA, Musa Nassoro Kuji leo tarehe 01, Februari 2025 ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kuboresha miundombinu ikiwemo Barabara ambazo kwa kiasi kikubwa zimechangia ongezeko la wageni katika Hifadhi ya Taifa Saadani. Kamishna Kuji ameyasema hayo wakati wa Kikao kazi kilichofanyika katika Hifadhi ya Taifa Saadani lengo likiwa ni kuboresha utendaji kazi wa Maafisa na Askari wa Hifadhi hiyo katika utekelezaji wa  majukumu yao ya kila siku. “Nimepokea Taarifa ya Saadani kuna ongezeko la watalii zaidi ya asilimia kumi na saba mafanikio haya yamepelekea kuongezeka kwa mapato kufikia billioni 1.7 ikiwa ni makusanyo ya miezi saba huku makadirio yakiwa ni billioni mbili kwa mwaka katika Hifadhi hii ni jambo la kupongeza sana kila mmoja wetu Afisa kwa Askari amechangia mafanikio haya na TANAPA tumejipanga kutoka kwenye kukusanya billioni na kwa sasa tunaenda kwenye Trillioni” “Mafanikio haya ya TANAPA ni matokeo y...