Skip to main content

Posts

Showing posts from January 26, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mwenyekiti wa Uvccm Mkoa wa Kagera Aongoza Upandaji wa Miti Siku ya Rais Samia

Na Angela Sebastian; Bukoba  Mwenyekiti wa umoja wa Vijana Chama Cha Mapinduzi CCM mkoa wa Kagera (UVCCM) Faris Buruhani amewaongoza  wanafunzi  650 wa shule ya sekondari  ya wasichana ya Omumwani iliyopo Manispaa ya Bukoba mkoani humo kupanda miti 2,000 kama sehemu ya maadhimisho ya siku ya kuzaliwa kwa Rais  Dk.Samia Suluhu Hassani. Akizungumza mara baada ya zoezi hilo, Faris alisema kuwa lengo la tukio hilo ni kuunga mkono jitihada za Rais Samia katika kulinda na kutunza mazingira, akisisitiza kuwa upandaji wa miti ni sehemu muhimu ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. Alisema  kuwa jumuiya hiyo imeamua kuonyesha uzalendo wa vitendo kwa kushiriki katika shughuli zenye manufaa kwa jamii na taifa kwa ujumla ambapo wanafunzi wasichanawa shule hiyo wamekuwa sehemu ya kumbukumbu katika sherehe hiyo ya kuzaliwa kwa mwaka 2026 Alisema  kuwa vijana wa mkoa wa Kagera wanamuunga mkono Rais na wanampongeza kwa kazi nyingi anazofanga ikiwemo kudu...

RC Batilda aiomba Hazina kuzibana taasisi zinazotoa mikopo 'kausha damu'

Na MASHAKA MHANDO, Tanga MKUU wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Balozi Dkt. Batilda Buriani, ameiomba Wizara ya Fedha kuzibana taasisi za fedha zinazotoa mikopo kwa riba kandamizi, huku akitangaza kuanza rasmi kwa utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote mkoani humo ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Rais ndani ya siku 100 za uongozi wake. Akifunga kilele cha Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa katika viwanja vya Usagara Jijini Tanga, Dkt. Batilda alitembelea banda la taasisi ya BRAC na kuelezea kusononeshwa na riba kubwa ya asilimia 3.5 kwa mwezi (wastani wa 40% kwa mwaka) wanayotozwa akina mama.  "Wizara ya Fedha imewaelekeza wakae chini washushe riba hiyo walau ifike asilimia 1.5 ili kuwapunguzia adha akina mama. Tunataka mikopo iwakomboe, siyo iwakandamize," alisema Dkt. Batilda. Katika hatua nyingine, Dkt. Batilda amewatangazia wakazi wa Tanga kuanza kutolewa kwa vifurushi vya Bima ya Afya kwa Wote, jambo ambalo lilikuwa moja ya kipaumbele na ahadi kuu ya Rais ndani ya siku zake 100 za kwanz...

Dkt. Mwigulu Ashiriki Zoezi la Upandaji Miti, Dodoma

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Januari 27, 2026 ameshiriki zoezi la upandaji miti, mbele ya ofisi ya Waziri Mkuu Mlimwa Jijini Dodoma. Zoezi hilo ni sehemu ya hatua ya kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uamuzi wake wa kizalendo wa kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa kwa vitendo vya kulinda mazingira.  Akizungumza baada ya zoezi hilo, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu akiwa ameambatana na mwenza wake Mama Neema Mwigulu, amempongeza Rais Dkt. Samia kwa uongozi wake kwa kuendelea kudhihirisha namna alivyo kiongozi mwenye maono, mbunifu na anayejali maslahi mapana ya Taifa. “Shughuli hii imekuwa na utofauti kwa kusababisha miti ipandwe kila kona ya nchi, kwenye vitabu vyetu vitukufu, kupanda mti ni moja ya ibada kwasababu wanufaika wa miti ni wengi” Kadhalika, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu ametoa wito kwa Watanzania kuadhimisha siku zao za kuzaliwa kwa kupanda miti. “Tunapokuwa na jambo la kukumbuka la aina hii, tufanye kitu ambacho kinaweka alama...

Siku Mia Moja za Rais Samia Zawezesha Upatikanaji wa Mtambo wa Kusafisha Chumvi Wilayani Kilwa

  DODOMA. Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ndani ya siku 100, Wizara ya Madini kupitia Shirika la Madini la Taifa(STAMICO) ipo katika hatua za mwishoni za usimikaji wa mtambo wa kusafisha chumvi katika eneo la Llingaula Wilayani Kilwa Mkoani Lindi. Hayo yamebainishwa Leo January 26,2027Jijini Dodoma na Waziri wa Madini Anthony Mavunde wakati akieleza ahadi za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan Katika kipindi Cha siku 100 alizowaahidi Watanzania kipindi Cha uchaguzi Mkuu. Amesema hatua hizo za mwishoni za usimikaji wa mtambo wa kusafisha chumvi ni mojawapo ya uongezaji thamani madini ya chumvi. "Gharama za ujenzi zinakadiriwa kuwa Shilingi Bilioni 4 na uwezo wake utakuwa ni wastani wa tani 2,040 kwa mwezi ambapo ni sawa na tani 24,480 kwa mwaka". Amesema "Wavunaji wa Chunvi kutoka Mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Lindi na Mtwara watanufaika na huduma zitakazotolewa na Mtambo huo unatarajiwa kuanza kazi Februari, 2026". Ameongeza A...

Nafasi za Kujiunga na Jkt Kwa Kujitolea Haziuzwi - Meja Jenerali Rajabu Mabele

Mkuu wa  JKT Meja  Jenerali Rajabu Mabele amesema nafasi za kujiunga na Mafunzo ya JKT kwa kujitolea Haziuzwi, zinatolewa bure  kwa kila kijana wa kitanzania mwenye sifa zilizoainishwa na JKT. Meja Jenerali Mabele  ameyasema hayo ofisini kwake Makao Makuu ya JKT Chamwino Dodoma, wakati walipokuwa akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari waliotaka kufahamu zaidi namna JKT linavyotekeleza jukumu la Malezi ya Vijana na umuhimu wake kwa Taifa. Amefafanua kuwa nafasi zote zimepelekwa katika Mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani, hivyo amewataka wananchi kuepuka matapeli watakaotaka kiasi chochote cha fedha ili kuwapatia vijana wao nafasi hizo.

Watendaji wa Uchaguzi Watakiwa Kutekeleza Majukumu Kwa Weledi

Na. Mwandishi Wetu, Iringa  Watendaji wa uchaguzi wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na weledi ili kufanikisha uchaguzi mdogo wa ubunge katika Jimbo la Peramiho na udiwani katika Kata ya Shiwinga unaotarajiwa kufanyika tarehe 26 Februari, 2026. Wito huo umetolewa na Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa (Mst) Mbarouk Salim Mbarouk Mkoani Iringa leo tarehe 26 Januari, 2026 wakati akifunga mafunzo ya watendaji wa uchaguzi yaliyofanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 24 Januari, 2026.  “Ni matazamio ya Tume kwamba, baada ya kupatiwa mafunzo haya, mtatekeleza majukumu yenu kwa ufanisi na weledi mkizingatia ratiba ya utekelezaji ili kufanikisha uchaguzi mdogo wa ubunge katika Jimbo la Peramiho na Udiwani katika Kata ya Shiwinga unaotarajiwa kufanyika tarehe 26 Februari, 2026,” amesema Jaji Mbarouk. Amesisitiza kuwa ili ufanisi uwepo ni muhimu watendaji hao wazingatie sifa na uwezo wakati wa kuteua na kuajiri watendaji wa vituo...

Twiga, Tanga Cement Wapewa Saa 48 Kujisalimisha

•Watakiwa kusimamia bei elekezi • Wachimbaji wadogo watakiwa kutulia DODOMA | Januari 26, 2026 SERIKALI kupitia Wizara ya Madini imezipa Kampuni za Twiga Cement na Tanga Cement saa 48 kufika mbele ya mamlaka husika na kujibu hoja zinazowakabili, ikiwemo madai ya kukiuka bei elekezi za madini zinazotolewa na Serikali na kukosa mikataba kwa wauzaji wa malighafi viwandani. Akizungumza leo katika kikao cha wachimbaji wadogo wa madini ya Jasi (gypsum) kutoka Same mkoani Kilimanjaro kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Gold, Ofisi za Tume ya Madini jijini Dodoma, Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Dkt. Steven Kiruswa, amesema kampuni hizo zikikaidi wito huo, Serikali itachukua hatua kali ikiwemo kusimamisha shughuli zao. “Kitendo cha kukaidi wito wa Serikali ni kuidharau mamlaka. Wasipofika ndani ya saa 48, tutamshauri Waziri kufuta leseni zao,” amesema Mhe. Dkt. Kiruswa. Amesisitiza kuwa kampuni hizo zinapaswa kulipa wasambazaji wa madini ya jasi kwa kuzingatia bei elekezi iliyowekwa na Serikali, kuto...