Skip to main content

Posts

Showing posts from December 5, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Makamu wa Rais Asisitiza Umuhimu wa Kulinda Mazingira na Muungano

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewasihi watumishi wa Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira kufanya kazi kwa weledi kwa kuzingatia dhamana kubwa waliyopewa ya kusimamia suala la Mazingira na Muungano hapa nchini. Makamu wa Rais amesema hayo wakati akizungumza na watumishi wa Ofisi ya Makamu wa Rais - Muungano na Mazingira katika kikao kazi kilichofanyika mkoani Dodoma. Amewataka kutambua na kuchukulia kwa uzito suala la uhifadhi na usimamizi wa mazingira kwani linabeba mustakabali wa vizazi vya sasa na baadaye.   Aidha amewataka kuwa na utaratibu wa upimaji wa malengo yaliyowekwa katika Wizara hiyo ikiwemo upandaji wa miti ili kuhakikisha utekelezaji wa mipango na malengo ya uhifadhi mazingira yanakuwa na matokeo mazuri na yenye manufaa. Makamu wa Rais, amesema ni lazima Wizara hiyo kutambua umuhimu wa suala la Muungano kwa kuhakikisha elimu inatolewa vya kutosha kwa wananchi hususani vijana kwa kuhusianisha maendeleo...

Mhandisi Ngh'oma Awataka Wakandarasi Kumaliza Kazi

 Na Mwandishi Wetu Mhandisi wa Mkoani Mwanza Chagu Ngh’oma amekagua utekelezaji wa baadhi ya miradi ya ujenzi wa Miundombinu ya Maji na Barabara inayotekelezwa mkoani humo pamoja na kuzungumza na wakandarasi,maafisa pamoja na wafanyakazi wanaotekeleza miradi hiyo.  Miongoni mwa miradi aliyokagua utekelezaji wake ni pamoja na ujenzi wa Tenki la maji la Sahwa ya chini ambapo amemtaka Mkandarasi kufanya kazi kwa weledi mkubwa pamoja na kuimarisha usimamizi wa vifaa ili kudhibiti upotevu wa vifaa vya ujenzi. Mhandisi Ngh'oma amesisitiza kuwa hatakuwa na huruma na wakandarasi wanaojihusisha na vitendo vya kuiba vifaa vya kazi na kusababisha kusuasua kwa utekelezaji wa miradi husika. ‘’Wizi wa Vifaa vya kazi ni kinyume na maadili na inachangia msimamizi kuonekana anafanya kazi na watu wasio waadilifu,hivyo sitakuwa na Muhali na wanaojihusisha na wizi wa vifaa vya kazi”alisema Mhandisi Ngh’oma wakati wakati wa kikao chake na Mkandarasi pamoja na wafanyakazi wanaojenga Tenki hilo. Kat...

Makamu wa Rais Asisitiza Umuhimu wa Kulinda Mazingira na Muungano

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewasihi watumishi wa Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira kufanya kazi kwa weledi kwa kuzingatia dhamana kubwa waliyopewa ya kusimamia suala la Mazingira na Muungano hapa nchini. Makamu wa Rais amesema hayo wakati akizungumza na watumishi wa Ofisi ya Makamu wa Rais - Muungano na Mazingira katika kikao kazi kilichofanyika mkoani Dodoma. Amewataka kutambua na kuchukulia kwa uzito suala la uhifadhi na usimamizi wa mazingira kwani linabeba mustakabali wa vizazi vya sasa na baadaye.   Aidha amewataka kuwa na utaratibu wa upimaji wa malengo yaliyowekwa katika Wizara hiyo ikiwemo upandaji wa miti ili kuhakikisha utekelezaji wa mipango na malengo ya uhifadhi mazingira yanakuwa na matokeo mazuri na yenye manufaa. Makamu wa Rais, amesema ni lazima Wizara hiyo kutambua umuhimu wa suala la Muungano kwa kuhakikisha elimu inatolewa vya kutosha kwa wananchi hususani vijana kwa kuhusianisha maendeleo...