Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewasihi watumishi wa Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira kufanya kazi kwa weledi kwa kuzingatia dhamana kubwa waliyopewa ya kusimamia suala la Mazingira na Muungano hapa nchini. Makamu wa Rais amesema hayo wakati akizungumza na watumishi wa Ofisi ya Makamu wa Rais - Muungano na Mazingira katika kikao kazi kilichofanyika mkoani Dodoma. Amewataka kutambua na kuchukulia kwa uzito suala la uhifadhi na usimamizi wa mazingira kwani linabeba mustakabali wa vizazi vya sasa na baadaye. Aidha amewataka kuwa na utaratibu wa upimaji wa malengo yaliyowekwa katika Wizara hiyo ikiwemo upandaji wa miti ili kuhakikisha utekelezaji wa mipango na malengo ya uhifadhi mazingira yanakuwa na matokeo mazuri na yenye manufaa. Makamu wa Rais, amesema ni lazima Wizara hiyo kutambua umuhimu wa suala la Muungano kwa kuhakikisha elimu inatolewa vya kutosha kwa wananchi hususani vijana kwa kuhusianisha maendeleo...
Marato tv - Sauti ya Jamii