Skip to main content

Posts

Showing posts from November 21, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Jenerali Mstaafu Mabeyo apongeza Kasi ya Ujenzi wa Nyumba Msomera

 -Nyumba 2,500 Zakamilika Msomera,Usambazaji wa Umeme Wafikia asilimia 98,Miundombinu Mingine Mbioni Kukamilika.  Kassim Nyaki, Msomera Tanga. Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro (NCAA) tarehe 21 Novemba, 2024  imefanya ziara ya kikazi kijiji cha Msomera Handeni mkoani Tanga kukagua utekelezaji wa ujenzi wa miundombinu mbalimbali kwa ajili ya wananchi wa Ngorongoro wanaoendelea kuhamia eneo hilo. Akiongoza bodi hiyo Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi NCAA Jenerali Venance Mabeyo (mstaafu) amezipongeza Sekta zote zinazohusika kutekeleza mradi huo kijiji cha Msomera kwa kukamilisha Nyumba 2500, ujenzi wa miundombinu ya Maji, mawasiliano, barabara, minada, majosho, kituo cha kuuzia maziwa, shule, zahanati, shule, kutenga maeneo ya malisho na miundombinu mingine kijijini hapo. "Tumetembelea eneo la Block F ambapo nyumba 1,000 zimekamilishwa katika awamu ya kwanza iliyohusisha ujenzi wa Nyumba 5,000, kitalu hiki pekee kuna matenki matatu ya maji yeny...

Bukombe wanataka Maendeleo na Maendeleo ni Ccm-Dkt.Biteko

*📌 Asema Vyama Vishindane kwa Sera na Utekelezaji wa Ahadi* *📌WanaCCM Bukombe Waaswa Kuimarisha Ushirikiano* *📌 Azindua Kampeni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Bukombe* Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa kwa miaka yote wananchi wa Wilaya ya Bukombe wamekuwa na imani na Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na kiu ya maendeleo. Amesema wananchi hao wana haki ya kuchagua kati ya maneno au maendeleo na  wamekuwa wakitamani maendeleo kwa kuwa na shule, barabara na zahanati. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 21, 2024  wakati akifungua Kampeni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Wilaya ya Bukombe zilizofanyika katika Kata ya Igulwa, Wilaya ya Bukombe Mkoa wa Geita. “ Tunapozindua kampeni zetu tuna wajibu wa kuchagua maneno au maendeleo, tutashindanisha vyama kwa sera na kuonesha tuliyofanya kwa kipindi kilichopita. Tumekuja leo kuwaambia sisi tuko upande wa maendeleo na wengine wako upande wa maneno ...

Wananchi Tarime wameitika,Ujio wa Lissu

 

Waziri Mkuu azindua Kamati Uchunguzi Kuporomoka kwa Jengo Kariakoo

 Novemba 21, 2024 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amezindua Kamati ya Wataalamu ya Uchunguzi wa Jengo lililoporomoka katika eneo la Kariakoo ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuchunguza chanzo cha tukio hilo pamoja na kufahamu ubora na uimara wa majengo yote yaliyoko Kariakoo. Tarehe 16 Novemba, 2024, majira ya saa 3 asubuhi, ilitokea ajali ya kuporomoka kwa jengo la takriban gorofa tatu lililopo mtaa wa Agrey Kata ya Kariakoo, Jijini Dar es Salaam na kusababisha athari kubwa kwa watu na mali katika eneo hilo. Akizungumza na  kamati hiyo, Mheshimiwa Majaliwa ameitaka ihakikishe kuwa inafanya uchunguzi wa kina, uwazi, haki na kwa kuzingatia viwango vya kitaaluma. “Fanyeni kazi hii kwa weledi, Taifa limewatuma nendeni mkaifanye kazi hii na mlete matokeo” Mheshimiwa Majaliwa amezindua kamati hiyo leo (Alhamisi, Novemba 21, 2024) katika ukumbi wa mikutano uliopo kwenye Ofisi Ndogo ya Waziri Mkuu, Magogoni jijini Dar es Salaam, ambapo ameiagiza itekele...

Waziri Mkuu azindua Taarifa ya Tathmini Utekelezaji wa Afya kwa Wote

WAZIRI MKUU Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali  itasimamia na kutekeleza masuala yote yaliyoainishwa kwenye taarifa ya Tathmini ya Utekelezaji wa Afya kwa wote na Utayari wa Kukabiliana na Dharura. Ameyasema hayo leo (Alhamisi, Novemba 21, 2024) alipofungua mkutano wa pamoja na Mawaziri na viongozi wa Juu wa Shirika la Afya Duniani kuhusu hali ya utekelezaji wa afya kwa wote na utayari wa kukabiliana na dharura nchini. Katika Mkutano huo Mheshimiwa Majaliwa alizindua taarifa ya Tathmini ya Utekelezaji wa Afya kwa wote na Utayari wa Kukabiliana na Dharura. Pia amesema Serikali itaweka mikakati madhubuti ya kushughulikia vipaumbele pendekezwa katika eneo la utawala, utendaji na rasilimali fedha. “Sina shaka kila eneo lenye changamoto litapatiwa ufumbuzi hususan kwa kuwa mkutano huu umetoa nafasi kwa waheshimiwa Mawaziri kujadili kwa kina na kwa pamoja masuala mbalimbali kuhusu afya kwa wote na kukabiliana na dharura” Aidha, Mheshimiwa Waziri Mkuu amezitaka Wizara, Idar...