Skip to main content

Posts

Showing posts from November 14, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Serikali Yadhamiria Ifikapo 2030 Kaya Milioni 15 Zitumie Kilimo Mseto

Fresha Kinasa. Mara. NAIBU Waziri wa Maliasili na Utalii Dunstan Kitandula amesaema kuwa, serikali inalenga ifikapo mwaka 2030 kaya Mil. 15 ziwe zinatumia Kilimo mseto hapa nchini.    Kitandula ameyasema hayo Novemba 14, 2023, wakati akifungua maonesho ya tisa ya Kilimo mseto yanayofanyika katika Kata ya Bweri Manispaa ya Musoma  kuanzia Novemba 14, hadi Novemba 16, 2024. Ambapo yanawaleta pamoja wadau mbalimbali wa Kilimo mseto kutoka serikalini,  sekta binafsi na wananchi kwa ujumla.  Amesaema kuwa,  Wadau wa mazingira na Kilimo mseto wanalojukumu la kushirikiana katika utekelezaji wa mkakati wa kitaifa wa Kilimo mseto uliozinduliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania machi 2024, huko Same Mkoani Kilimanjaro. Ambapo, Wizara ya Maliasili na Utalii ndio msimamizi wa mkakati huo,   unaolenga kuhamasisha Kilimo mseto katika kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi, lishe bora pamoja na kukuza kipato. Huku akiweka wazi kwamba,  ...

Rais Samia amesema Lawrence Mafuru alikuwa Zawadi Kwa Taifa Letu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Waombolezaji kuaga mwili wa aliyekuwa Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Marehemu Lawrence Nyasebwa Mafuru katika Viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaa, leo tarehe 14 Novemba, 2024. Katika salamu zake za pole kwa familia na Watanzania Rais Samia amesema kifo cha Mafuru kimeacha pengo kubwa kwa taifa hasa kutokana na mchango wake mkubwa wa kujitolea kwa taifa lake. Kwa sababu hiyo Mh Rais Dkt Samia amesema Laurence alikuwa zawadi kwa taifa lake na kwamba alikuwa ni mmoja wa mashujaa wa Tanzania. Amesema  ushujaa unaweza kujitokeza  kwa namna mbali ikiwemo kufanya kazi kwa bidii na kujitoa kwa taifa lako bila kuchoka,hivyo Mafuru anastahili sifa  hiyo. Mh Rais Samia amesema Lawrence amekuwa na mchango mkubwa katika sekta binafsi na sekta ya umma na ameacha alama ambayo haitafutika hasa katika mageuzi makubwa ya uendeshaji wa mashirika ya umma aliyofanya akiwa msajili wa hazina. Amesema kutoka...

Rais Samia aongoza Watanzania Kuaga Mwili wa Mafuru leo Novemba 14

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan aongoza Waombolezaji kuaga mwili wa aliyekuwa Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Marehemu Lawrence Nyasebwa Mafuru katika Viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaa, leo tarehe 14 Novemba, 2024.

Mkutano wa Kimataifa Sekta ya Madini Kuomgeza fursa za Uwekezaji Tanzania

*_Rais Samia kuufungua_* *_Kuhudhuriwa na Wageni Zaidi ya 1,500_* *_Kupambwa na Hafla Maalum ya “Usiku wa Madini”_* 📍 Dar es Salaam,  Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde amesema kuwa Mkutano wa Kimataifa wa Uwekezaji katika Sekta ya Madini unatarajiwa kuongeza fursa za uwekezaji katika Sekta ya Madini hapa nchini sambamba na kuweka msingi thabiti wa ushirikiano baina ya wadau, kuimarisha uzalishaji wa madini, na kuhakikisha kuwa rasilimali za madini zinawanufaisha watanzania kiuchumi na kijamii. Amesema hayo leo Novemba 14, 2024 wakati akizungumza katika Mkutano na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam kuhusu maandalizi ya Mkutano wa 6 wa Kimataifa wa Uwekezaji katika Sekta ya Madini nchini Tanzania, unaotarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 19 hadi 21 Novemba 2024 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.  Amesema kuwa, Mkutano huo unaoongozwa na Kaulimbiu ya “Uongezaji Thamani Madini kwa Maendeleo ya Kiuchumi na Kijamii” unatarajiwa ...