Skip to main content

Posts

Showing posts from June 10, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

MKUU WA JESHI LA MAGEREZA AFUNGUA MAFUNZO YA UTEKELEZAJI WA PROGRAMU ZA UREKEBISHAJI KWA MAAFISA USTAWI WA JAMII

 Na. Ssgt Mawazo Mtondo - Dodoma. Mkuu wa Jeshi la Magereza, CGP Jeremiah Yoram Katungu, leo Juni 10, 2026, amefungua rasmi Mafunzo kwa Maafisa Ustawi wa Jamii kuhusu Mwongozo wa Utekelezaji wa Programu za Urekebishaji katika Ukumbi wa Rugimbana, Msalato, jijini Dodoma. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, CGP Katungu aliishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, kwa namna inavyoendelea kuliwezesha Jeshi la Magereza kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi. Alisema Serikali imekuwa ikitoa rasilimali fedha kwa ajili ya  ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya magereza, makazi ya watumishi, vyombo vya usafiri pamoja na kugharamia mafunzo mbalimbali kwa watumishi wa Jeshi la Magereza. CGP Katungu alibainisha kuwa moja ya majukumu ya msingi ya Jeshi la Magereza ni urekebishaji wa wafungwa kwa kuwapatia elimu, ujuzi na maarifa ili wanapomaliza vifungo vyao warejee katika j...

RAIS DKT. MWINYI: ZANZIBAR NA SINGAPORE KUFUNGUA UKURASA MPYA WA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Zanzibar inakusudia kuimarisha uhusiano na ushirikiano na Jamhuri ya Singapore kwa kuelekeza nguvu zaidi katika diplomasia ya uchumi, biashara na uwekezaji. Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 10 Juni, 2026 Ikulu alipofanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Singapore, Mhe. Tharman Shanmugaratnam, Ikulu Zanzibar ambapo alizikaribisha kampuni na wawekezaji wa Singapore kuwekeza Zanzibar katika sekta za uchumi wa buluu, utalii, nishati, teknolojia na kuongeza thamani ya mazao ya baharini na mwani. Kwa upande wake, Rais Tharman Shanmugaratnam amepongeza hatua kubwa za maendeleo zinazofanywa Zanzibar na kuahidi kuhamasisha wawekezaji wa Singapore kuja kuwekeza Zanzibar. Baada ya mazungumzo hayo, Rais Dkt. Mwinyi, alimwandalia mgeni wake, Rais Tharman dhifa ya chakula cha mchana iliyofanyika Ikulu Zanzibar.

MAGEMBE AELEZA MATARAJIO BAJETI 2026/2027 KATIKA JIMBO LA CHATO KASKAZINI

Mbunge wa Jimbo la Chato Kaskazini, Mhe. Kornel Magembe, amesema ana matarajio makubwa na Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka 2026/27 inayotarajiwa kusomwa Juni 11, 2026, akieleza kuwa bajeti hiyo inapaswa kubeba na kutekeleza maono ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. Akizungumza kuhusu matarajio yake, Magembe amesema miundombinu ya barabara ni miongoni mwa maeneo muhimu yanayohitaji kupewa kipaumbele ili kurahisisha usafiri na kuchochea maendeleo ya wananchi wa Chato Kaskazini. Ametaja baadhi ya miradi ya barabara iliyopangwa kutekelezwa kupitia bajeti hiyo ikiwemo barabara ya Nyamirende–Biharamulo yenye urefu wa kilomita 50, pamoja na barabara ya Katende–Kachwamba–Kasenga inayotarajiwa kujengwa kupitia TARURA. Pia ametaja barabara ya kilomita 1.8 katika Kata ya Mgaza inayopangwa kujengwa kwa kiwango cha lami. Mbunge huyo amesema kutokana na jiografia ya jimbo lake kuwa kandokando ya Ziwa Victoria, wananchi wanahitaji huduma bora za usafiri wa majini ikiwe...

LUTANDULA:BAJETI HII ITAJIBU HITAJI LA MAJI, BARABARA NA AFYA JIMBO CHATO KUSINI

 Mbunge wa Jimbo la Chato Kusini mkoani Geita, Paschal Lutandula, amesema Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka 2026/27 inayotarajiwa kusomwa Juni 11, 2026, imebeba matumaini makubwa kwa wananchi wa jimbo hilo kutokana na miradi mikubwa ya maendeleo inayolenga kuboresha maisha yao. Akizungumza na waandishi wa habari katika Viwanja vya Bunge leo Jun 10,2026 Jijini Dodoma, Mbunge wa Jimbo la chato kisini, Paschal Lutandula amesema moja ya vipaumbele vikubwa ni utekelezaji wa Mradi wa Maji wa Buzilayombo wenye thamani ya zaidi ya Shilingi bilioni 23, pamoja na uchimbaji wa visima zaidi ya vitano vitakavyosaidia kuondoa changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama. "Baada ya mwaka wa fedha 2026/27, changamoto ya maji katika Jimbo la Chato Kusini itakuwa imepungua kwa kiwango kikubwa. Serikali imejipanga kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji karibu na maeneo yao," amesema. Katika sekta ya umeme, amesema Serikali inaendelea kukamilisha usambazaji wa huduma hiyo katika vitongoj...

BAJETI YA TRILION 62.3 YAANZA SAFARI YA DIRA 2050

 Serikali imesema Bajeti ya mwaka wa fedha 2026/27 itaweka msingi imara wa utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, huku ikilenga kuharakisha ukuaji wa uchumi, kuongeza ajira na kuboresha ustawi wa wananchi. Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, amesema bajeti hiyo ni ya kihistoria kwa kuwa ndiyo ya kwanza kutekeleza kwa vitendo Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (2026/27–2030/31) pamoja na Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2025. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma Juni 10, 2026, kabla ya kuwasilisha rasmi bajeti hiyo bungeni, Waziri Omar amesema Serikali inatarajia kutumia Shilingi trilioni 62.3 katika mwaka wa fedha 2026/27, ambapo sehemu kubwa itaelekezwa kwenye miradi ya maendeleo na utoaji wa huduma muhimu za kijamii. “Bajeti hii inakuja katika kipindi muhimu ambapo Taifa limeanza safari ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Dhamira yetu ni kuhakikisha ukuaji wa uchumi unakuwa jumuishi...

NKINGWA ATARAJIA BAJETI KUU YA SERIKALI KUGUSA MAISHA YA WANANCHI

 Mbunge wa Jimbo la Mbogwe Mkoa wa Geita,Mhe Fagason Nkingwa,amesema ana matarajio makubwa kwa Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka 2026/2027 inayotarajiwa kuwasilishwa bungeni Juni 11, 2026, akieleza kuwa anatarajia bajeti hiyo kuleta majibu ya changamoto zinazowakabili wananchi na kuharakisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo nchini. Akizungumza nje ya viwanja vya Bunge jijini Dodoma leo Juni 10, 2026, Nkingwa amesema ana imani na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kutokana na namna ilivyokuwa ikisikiliza maoni ya wananchi na kuyajumuisha katika mipango ya maendeleo. "Imani yangu kwa Serikali inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kubwa. Serikali hii imeendelea kuwa sikivu kwa wananchi wake, na sisi wabunge tumeshiriki kikamilifu kuchangia bajeti za wizara mbalimbali. Ninaamini bajeti itakayowasilishwa kesho itakuja na majibu ya changamoto zinazowagusa wananchi moja kwa moja," amesema Nkingw...