Skip to main content

Posts

Showing posts from August 25, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

MWENYEKITI UVCCM MKOA WA KAGERA ASHIRIKI FAINALI YA BASHUNGWA KARAGWE CUP 2024

  Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Kagera *Ndugu Faris Buruhani,* ameshiriki fainali ya mpira wa Miguu ya BASHUNGWA KARAGWE CUP 2024 ilitofanyika katika uwanja wa mpira wa Bashungwa mjini Kayanga Karagwe. Fainaili hiyo ambayo imefanyika. Agosti 25-2024 imekuwa ya aina yake na kuhudhuriwa na maelfu ya wananchi wa Karagwe na wilaya jirani, sambamba na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali. Ligi hiyo imetamatika kwa timu ya *Nyabiyonza FC kuibuka Mshindi* katika mashindano hayo kwa kunyakua  Kombe, *pesa taslimu 6,000,000/= (milioni sita)* na zawadi nyingine kutoka kwa kamati ya mashindano hayo. Bashungwa Karagwe Cup 2024, ni mwendelezo wa mashindano ya mpira wa miguu yanayoandaliwa na Mbunge wa jimbo la Karagwe *Mh. Innocent Bashungwa* kila mwaka, yenye lengo la kuwaleta vijana pamoja, kuibua vipaji vya vijana na pia kuwainua kiuchumi kupitia vipaji vyao.

TANZANIA YATUMIA KILA MBINU KUMNADI NDUGULILE

  Mwandishi wetu-Brazzaville, Congo Waziri wa Afya, Mhe. Jenista Mhagama, pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo, wameungana na mgombea wa Tanzania kwa nafasi ya Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Dkt. Faustine Ndugulile (MB), katika mazoezi ya ‘Walk the Talk’. Tukio hili la mazoezi ya ‘Walk the Talk’ lililofanyika Agosti 25-2025 Jijini Brazzaville, na kuhudhuriwa na wajumbe mbalimbali waliowasili; lina lenga kuimarisha afya pamoja na kupiga vita magonjwa yasiyoambukiza Wakiwa kwenye mazoezi hayo, Waziri Mhagama na Waziri Kombo walipata fursa ya kusalimiana na mawaziri wenzao na kuwaomba kuunga mkono mgombea wa Tanzania Dkt. Ndugulile katika juhudi zake za kuwania nafasi hii muhimu, huku wakisisitiza umuhimu wa kuwa na maisha yenye afya na kufuata mifumo bora ya kuzuia magonjwa. Wakati wa tukio hilo, viongozi hawa wa Tanzania walikuwa sehemu ya ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ulioa...

Tume ya Taifa ya Uchaguzi Yashauriwa Kutoa Elimu Zaidi Kwa Wananchi

  Na Robinson Wangaso-Musoma.  Wadau wa maendeleo mkoani Mara wameshauri tume huru ya Taifa ya Uchaguzi kutoa elimu kwa wananchi ili kuweza kutofautisha Uchaguzi mkuu utakaofanyika mwakani 2025 na Uchaguzi wa Serikali za mitaa utakaofanyika mwezi Novemba mwaka huu 2024. Akitoa ushauri huo,  Katekista Peter Benard kutoka kanisa LA Roman Catholic amesema elimu ya uboreshaji wa daftari la kudumu inahutajika ili kutofautisha Matumizi daftari hilo katika Uchaguzi mkuu Na ule wa Serikali za mitaa.  Akifungua mkutano wa wadau mkoani Mara Mwenyekiti tume huru ya Taifa ya uchaguzi nchini Jaji Jacobs M. Mwambegele amewaasa wadau kuhamasisha wananchi kujitokeza Kwa wingi kuboresha taarifa zao katika daftari la kudumu la wapiga kura. Jaji Mwambegele ameyasema hayo leo Agosti 25, 2024 katika Mkutano wa Tume huru ya taifa ya Uchaguzi kuhusu uboreshwaji wa daftari la kudumu la wapiga Kura uliyofanyika mkoani Mara katika ukumbi wa uwekezaji katika ofisi za mkuu wa mkoa.  Amesem...

RAIS SAMIA AISHUKURU TAWA NA TANAPA KIZIMKAZI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amezishukuru Taasisi za Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) na Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA ) kwa kuonesha Wanyamapori hai kwenye Tamasha la Kizimkazi lililofanyika Kusini Unguja visiwani Zanzibar. Ameyasema hayo leo Agosti 25,2024 kwenye Kilele cha Tamasha la Kizimkazi lililohitimishwa Makunduchi - Mweha na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali akiwemo Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) na Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi. "Tunawashukuru TAWA,TANAPA, kwa kutuletea wanyama hai katika Maonesho. Ndugu zangu hawa kama walikuwa hawajui fisi basi wamemjua kwenye maonesho" amesisitiza Rais Samia.  Rais Samia alisema kuwa lengo la Tamasha hilo kubwa ni kuchochea Maendeleo ya kiuchumi na kijamii, kuwaleta watu pamoja na kudumisha Mila na desturi.  Tamasha la Kizimkazi la 2024 liliambatana na matukio mbalim...

Wavuvi Musoma Vijijini Waishukuru Serikali

  Na Shomari Binda-Musoma WAVUVI katika jimbo la Musoma vijijini wameishukuru serikali chini ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa mikopo nafuu kwa ajili ya uvuvi wa vizimba. Shukrani hizo zimetolewa na wavuvi was Kitongoji cha Busumi kilichopo Kata ya  Suguti  mara baada ya kufanikiwa kuingiza majini vizimba 4 Kupitia kikundi chao kilichopo chini ya Busumi Fishing Cooperative Society (Chama cha Ushirika cha Wavuvi wa Kitongoji cha Busumi) kimechukua mkopo nafuu usiokuwa na riba kutoka serikalini kwa ajili ya uvuvi wa vizimba ndani ya Ziwa Victoria. Ushirika huo wa wanachama 20 umekopa shilingi milioni 117 kwa ajili ya kupata vizimba vinne (4), vifaranga vya samaki, chakula na bima ya ufugaji wao wa samaki. Mmoja wa wavuvi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mkama Maiga amesema wanaamini baada ya kuwezeshwa na serikali wanakwenda kunufaika kupitia uvuvi. Maiga amesema serikali imewashika mkono nao watahakikisha wana simama imara katika kufanya shughuli zao ili kujiinua kiuchu...

WADAU GEITA WAPONGEZA MIFUMO MIPYA YA MITIHANI YA TAIFA

Mkurugenzi wa Shule ya Msingi Kadama, Mwalimu Leticia Pastory, amesema kuwa mabadiliko ya mfumo wa mitihani ya Taifa kwa shule za msingi yanatarajiwa kuleta manufaa makubwa kwa wanafunzi.  Akizungumza wakati wa mahafali ya kumi na nne ya shule ya Msingi ya Kadama, Mwalimu Leticia alieleza kuwa mfumo mpya utaimarisha ubora wa elimu na kuwaandaa wanafunzi kwa zaidi ya ajira za kawaida, huku pia ukilenga kuwawezesha kujiajiri baada ya kuhitimu masomo yao. Aliongeza kuwa mfumo huo utawajengea wanafunzi uwezo wa kujitegemea, ubunifu, na ujasiriamali, vitu ambavyo ni muhimu sana katika mazingira ya sasa ya kiuchumi.  "Mabadiliko haya ni hatua muhimu katika kuboresha elimu ya msingi, na tunaamini yatasaidia sana kuandaa vijana wenye ujuzi wa maisha," alisema Mwalimu Leticia. Mgeni rasmi kwenye mahafali hayo, Mboje Kisusi, aliwasisitiza wazazi na walezi umuhimu wa kuwafundisha watoto wao maadili mema na kumjua Mungu, akiongeza kuwa elimu bora inapaswa kuendana na malezi ya kiadili. M...