Na Shomari Binda-Musoma MBUNGE wa jimbo la Musoma mjini Vedastus Mathayo leo agosti 15 amekabidhi ng'ombe, mipira 16 na fedha kiasi cha shilingi laki 2 kwa ajili ya mashindano Mathayo Polisi Jamii Cup 2024. Ng'ombe,mipira na fedha imekabidhiwa kwa mkuu wa polisi wilaya ya Musoma kama sehemu ya zawadi kwenye mashindano hayo yanayoyarajiwa kuanza hivi karibuni kwa kushirikisha timu Kutoka Kata 16 za manispaa ya Musoma. Akikabidhi zawadi hizo kwa niaba ya mbunge huyo Meya wa manispaa ya Musoma Patrick Gumbo amesema huu ni mwaka wa pili ana dhamini mashindano hayo kwa lengo la kuwaweka vijana pamoja na kuinua viwango vyao. Amesema mbunge Mathayo ni mwanamichezo ambaye baada ya kuombwa na Jeshi la polisi wilaya ya Musoma kuwa sehemu ya kufanikisha mashindano hayo hakusita. " Mheshimiwa mbunge ameenda kwenye vikao vya bunge na ameniagiza nikabidhi mipira na ng'ombe kama zawadi kwenye mashindano ya Mathayo Polisi Jamii Cup. Ng'ombe itakuwa zawadi ya bingwa wa mashindano n...
Marato tv - Sauti ya Jamii