Na. Joyce Ndunguru, Morogoro Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi ameelekeza kuendelea kwa matumizi ya teknolojia mbalimbali katika ulinzi wa rasilimali ya wanyamapori. Dkt. Abbasi ameyasema hayo leo Disemba 10, 2024, katika kikao na watumishi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori (TAWA) kilichofanyika katika Makao Makuu ya TAWA Mkoani Morogoro. "Tuendelee kutumia teknolojia za kisasa katika ulinzi wa rasilimali ya wanyamapori ", amesema Dkt. Abbasi. Aidha, Dkt. Abbasi ameipongeza TAWA kwa utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoyatoa katika ziara yake ya kikazi Mkoani Ruvuma mnamo mwezi Septemba ya kununua ndege nyuki kwa ajili kudhibiti wanyama wakali na waharibifu. "Nimefurahi kuona mmeanza kutekeleza maelekezo ya Rais ya kununua ndege nyuki na hapa TAWA nimeona kazi imeanza" ameongeza Dkt. Abbasi Vilevile, Dkt. Abbasi alitoa pongezi kwa TAWA kwa ujenzi wa vizim...