Skip to main content

Posts

Showing posts from December 24, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

TMDA yaimarisha ulinzi dawa zenye asili ya kulevya

* Waganga wafawidhi, wafamasia wapigwa msasa kuzuia uchepushaji Na MASHAKA MHANDO, Tanga MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA), imetoa mafunzo maalum kwa Waganga Wafawidhi, Wafamasia na Wakaguzi wa dawa kutoka wilaya nne za Mkoa wa Tanga, lengo likiwa ni kudhibiti matumizi holela ya dawa za tiba zenye asili ya kulevya (Narcotics & Psychotropics) ili kuzuia uraibu miongoni mwa vijana. Mafunzo hayo yaliyolenga wilaya za Tanga Jiji, Muheza, Pangani na Mkinga, yanakuja kama mkakati wa Serikali kuhakikisha dawa hizo kali ambazo ni muhimu kwa wagonjwa wa upasuaji na saratani, haziingii mitaani kinyume cha sheria. Akizungumza katika mafunzo hayo, Meneja wa TMDA Kanda ya Mashariki, Keddy Manga, alisema kuwa jukumu la msingi la mamlaka hiyo ni kuhakikisha dawa, vifaa tiba na vitendanishi ni bora, salama na vina ufanisi, lakini tahadhari kubwa inahitajika kwenye dawa za maumivu makali. “Kuna dawa zinatumika kwa wagonjwa wenye maumivu makali kama wa saratani au wanaofanyiwa upasuaji. Hata hivy...

Mradi wa Hatifungani ya Kijani wa Bilioni 53.12 Wafikia Asilimia 45

Na MASHAKA MHANDO, Tanga MAMLAKA ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jiji la Tanga (Tanga-UWASA), imetangaza neema ya upatikanaji wa maji kwa miaka 20 ijayo kwa wakazi wa miji ya Tanga, Muheza, Mkinga na Pangani, kufuatia utekelezaji wa mradi wa kihistoria wa Hatifungani ya Kijani (Green Bond). Mradi huo wa Sh. bilioni 53.12, ambao ni wa kwanza wa aina yake nchini na Afrika Mashariki, unatarajiwa kukamilika Machi 2026 na utakuwa mwarobaini wa kudumu wa changamoto ya usambazaji maji kwa asilimia 100 katika wilaya hizo nne. Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira wa Tanga-UWASA, Mhandisi Salum Ngugi, wakati wa ziara ya waandishi wa habari kutembelea chanzo cha maji cha Mabayani na kituo cha kusukuma maji cha Mowe. Mhandisi Ngugi alisema mradi huo ni jibu la changamoto iliyodumu tangu mwaka 2010, ambapo miundombinu iliyosanifiwa kwa miaka 20 tangu mwaka 1978 ilikuwa imezidiwa na kasi ya ongezeko la watu. "Tulitakiwa kufanya maboresho mwaka 2010 lakini...

Helikopta Yaanguka Mlima Kilimanjaro

  Helikopta ya kampuni ya uokoaji Kilimediair Aviation imepata ajali katika Mlima Kilimanjaro nchini Tanzania na kusababisha vifo vya watu wote watano waliokuwemo kwenye helkopta hiyo, wakiwemo raia wa kigeni wawili na rubani. Ajali hiyo imetokea Jumatano ya Desemba 24 saa 11:30 jioni, katika eneo lililopo kati ya kilele cha Kibo na Barafu Camp, moja ya njia zinazotumiwa sana na watalii wapandaji wa mlima huo mrefu barani Afrika. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo, akieleza kuwa helikopta hiyo iliyokuwa imebeba watu hao watano ilikuwa katika zoezi la kuwachukua wagonjwa waliokuwa mlimani. Kwa mujibu wa taarifa rasmi, waliopoteza maisha ni Plos David na Plosova Anna raia wa Jamuhuri ya Czech walipandishwa mlimani kutalii na kampuni ya Mikaya Tours, Jimmy Daniel (daktari), Innocent Mbaga ambaye alikuwa muongoza watalii na rubani Costantine Mazonde raia wa Zimbabwe. Kwa mujibu wa mtandao wa Mwananchi, Maigwa amesema kuwa taarifa z...

Waziri wa Ulinzi na Jkt Azungumza na Wazee wa Mkoa wa Mara

  Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Rhimo Nyansaho akizungumza na wazee wa Mkoa wa Mara katika eneo la Komaswa, Wilaya ya Tarime leo tarehe 24 Disemba, 2025.  Kikao hicho kimehudhuriwa pia na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Chama cha Mapinduzi Mhe. Fadhili Maganya, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi, Mjumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) Mhe. Christopher Gachuma, Mtoto wa Baba wa Taifa, Madaraka Nyerere. Katika kikao hicho kilichohudhuriwa na wazee zaidi ya 160, wazee wameazimia kulinda na kudumisha amani na utulivu katika Mkoa wa Mara na kufanya kikao kama hicho kila mwaka.

Dkt.Mwigulu: Mtendaji Mkuu wa TEMESA na Menejimenti yake wafutwe kazi

_Aagiza uchunguzi ufanyike kubaini sababu za uharibifu wa mara kwa mara wa vivuko_ WAZIRI MKUU Dkt. Dkt. Mwigulu Nchemba ameagiza kufutwa kazi na kufikishwa katika vyombo vya sheria kwa aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) pamoja na Menejimenti ya wakala huo kutokana na ubadhilifu wa zaidi ya shilingi bilioni 2.5. Pia, Waziri Mkuu amemuagiza Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega kufanya uchunguzi wa vivuko vyote ili kubaini vyanzo vya uharibifu kwa sababu kuna taarifa kwamba vivuko hivyo vinaharibiwa kwa makusudi ili wahusika waweze kujipatia fedha kupitia matengenezo. Amesema uamuzi huo unatokana na matokeo ya tume maalumu iliyoundwa ndani ya kuchunguza tuhuma za matumizi mabaya ya fedha za umma katika wakala huo. “Vyombo husika vichukue hatua kwa wahusika, haya mambo ya kutoheshimu fedha za umma, kutokuwa na huruma na Watanzania lazima yafike mwisho.” Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo Jumatano, Desemba 24, 2025 akizungumza na viongozi wa mkoa wa Dar es Sa...