Skip to main content

Posts

Showing posts from December 7, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Waziri Kombo awasilisha taarifa ya Ufafanuzi kwa Kamati ya CMAG, kufuatia Vurugu za tarehe 29 Okotba 2025.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb) amewasilisha taarifa ya ufafanuzi kwa Kamati ya Mawaziri wa Jumuiya ya Madola Wanaosimamia Utekelezaji wa Tunu za Jumuiya hiyo (Commonwealth Ministerial Action Group-CMAG) kufuatia vurugu zilizotokea nchini tarehe 29 Okotba 2025, katika kikao chake cha dharura kilichofanyika  kwa njia ya mtandao tarehe 05 Desemba 2025. Akiwasilisha taarifa hiyo, Mhe. Kombo amesema matukio yaliyotokea tarehe 29 Oktoba 2025, ambayo hayakutarajiwa kutokea yalisababisha uharibifu mkubwa, ukiwemo wa miundombinu, ofisi za Serikali, mali za raia, kuchomwa moto kwa vituo vya polisi na kusababisha vifo na majeruhi.  Amesema kufuatia vurugu hizo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan aliunda Tume Huru ya Uchunguzi wa Vurugu zilizotokea wakati na baada ya uchaguzi. Tume hiyo imepewa  miezi mitatu kukamilisha jukumu hilo na kuwasilisha taarifa kamili kwa Mhe. Rais. Tume hiy...

Katibu Mkuu Ujenzi Aagiza Tanroads Kupunguza Msongamano Jijini Dar

Katibu Mkuu, Wizara ya Ujenzi, Balozi Mhandisi Aisha Amour, ameuelekeza Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) kufungua kwa muda barabara zote za makutano katika maeneo yanayotekelezwa miradi ya Mabasi Yaendayo Haraka (BRT) ili kupunguza msongamano wakati ujenzi ukiendelea. Akizungumza mara baada ya kukagua maendeleo ya mradi huo jijini Dar es Salaam, Balozi Amour alisema hatua hiyo imelenga kupunguza msongamano wa magari kuelekea kipindi cha Sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya, ambacho kwa kawaida huongeza idadi ya watu na magari jijini humo. “Tumeona njia ya haraka ya kupunguza msongamano katika kipindi hiki ni kufungua barabara za makutano wakati tukisubiri ujenzi wa kudumu wa barabara hizo unaoendelea, ikiwemo ule wa BRT”. Aidha, ameelekeza wakandarasi wote kuhakikisha kuwa barabara za michepuko zinapitika na ziko katika hali nzuri. Amesema kuwa mkandarasi anayejenga kipande cha barabara ya Mwenge–Tegeta ameahidi kuweka lami ya muda katika barabara ya mchepuko ili kurahisisha huduma ...