Skip to main content

Posts

Showing posts from June 8, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Dc Chikoka Apongeza Juhudi za Mbunge Mathayo Kwa Maendeleo ya Elimu Jimboni

Na Shomari Binda-GMTV  MKUU wa Wilaya ya Musoma Juma Chikoka amepongeza maendeleo ya kielimu yanayofanywa na mbunge wa jimbo la Musoma mjini Vedastus Mathayo. Pongezi hizo amezitoa Mara baada ya mbunge huyo kushusha mbao zaidi ya 2000 zitakazoendeleza mradi wa utengenezaji wa madawati,viti na meza kwa ajili ya wanafunzi wa shule za msingi na sekondari kukalia. Akizungumza na GMTV amesema hakuna jambo na urithi ulio bora kama elimu hivyo juhudi za mbunge huyo zinapaswa kupongezwa. Amesema mwanafunzi anapopata sehemu nzuri ya kukaa na kupata elimu uzingatia kinachofundishwa akiwa darasani. Chikoka amesema kama mdau wa maendeleo yakiwemo ya elimu anapongeza juhudi zinazofanywa na mbunge Mathayo. Amesema Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan amewekeza kwenye elimu kwa ujenzi wa shule mpya na kuongeza madarasa ili watoto wapate elimu na mambo ya kumuunga mkono ni kama anavyofanya mbunge Mathayo. " Kwa sasa mzazi achangishwi fedha kwaajili ya ujenzi wa shule na madarasa kazi knafanywa Rais Dkt.S...

Jimbo la Musoma Vijijini Kufunguliwa Shule 2 za "High Schools"za Masomo ya Sayansi

Na Shomari Binda-Musoma  JIMBO la Musoma vijijini mkoani Mara linaratajia kufungua shule mbili mpya za sekondari za kidato cha tano na sita julai 1, 2025 baada ya ujenzi wake kukamilika. Shule hizo zilizojengwa na serikali ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ni pamoha na Suguti itakayoanza na wanafunzi 158 pamoja na Mugango itakayoanza na wanafunzi 62 ambazo usajili wake umekamilika.  Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijni Profesa Sospeter Muhongo imeeleza kuwa kukamilika kwa ujenzi wa miundombinu ya shule hizo kutarahisisha utoaji wa elimu, ufundishaji na ujifunzaji kwa wanafunzi.  Mbunge huyo amesema baada ya muhula wa masomo kuanza atatembelea shule hizo na kugawa vitabu vya masomo ya sayansi kwa lengo la kupanua utoaji wa elimu.  Baadhi ya wadau wa elimu waliopokea taarifa hiyo wakiwemo wananchi wa jimbo la Musoma Vijijini wamemshukuru mbunge huyo kwa jitihada zake za kuinua elimu. Wakizungumza na GMTV wamesema mbunge huyo ni mfano wa ...

Rais Samia kuzindua Daraja la Kigongo - Busisi Juni 19

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuzindua daraja la Kigongo- Busisi (KM 3) juu ya Maji linalounganisha wilaya za Misungwi na Sengerema juni 19 mwaka 2025. Waziri wa Ujenzi mh Abdallah Ulega ametoa taarifa hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika hafla iliyofanyika katikati ya daraja hilo alipokua akielezea kazi zilizotekelezwa ndani ya kipindi cha miaka minne ya uongozi wa serikali ya awamu ya sita. Amebainisha kuwa Serikali chini ya Wizara ya Ujenzi imefanikiwa sana kwenye ujenzi wa madaraja, barabara, vivuko na kurahisisha utoaji wa huduma kwa jamii pamoja na kukuza uchumi wa watanzania. Ulega amesema pamoja na kukamilika kwa daraja hilo lililogharimu Bilioni 716, serikali ya awamu ya sita imejenga madaraja mengine mengi kama Tanzanite (KM 1) juu ya bahari, Wami (Mita 510), Kitengule (140 Mita), Msingi- Singida (Mita 100). Amesema, daraja la Kigongo Busisi limejengwa na kampuni ya CCECC kwa kushirikiana na wataalamu ...

Waziri Ndumbaro Awasili Tarime Kufungua Mafunzo ya Elimu ya Kisheria

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amewasili Wilayani Tarime Mkoani Mara Jana tarehe 08 Juni, 2025 ambapo kesho Juni 9, 2025 atafungua mafunzo yenye lengo la kuwajengea uwezo Viongozi wa Kata na Wilaya kuhusu masuala yanayohusu Sheria na utatuzi wa migogoro. Mara baada ya kuwasili Wilayani hapo, Waziri Ndumbaro amepokelewa na Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe. Meja Edward Gowele pamoja na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali. Katika kuendelea kuhakikisha Viongozi wa Kata na Wilaya wanakua na ujuzi na kuzingatia weledi katika utatuzi wa migogoro mbalimbali inayowasilishwa kwenye mamlaka zao, Wizara ya Katiba na Sheria imeendelea kutoa mafunzo ya mara kwa mara kwa makundi hayo ili kuwajengea uwezo wa utatuzi wa migogoro hiyo na kusimamia upatikanaji wa Haki kwa Wananchi.  Mafunzo yatakayotolewa ni pamoja na elimu ya utatuzi wa migogoro kwa njia mbadala, elimu ya uraia na utawala bora pamoja na elimu juu ya ukatili wa kijinsia.

Pinda Aongoza Kikao Cha Bodi ya Taasisi ya Kumbukumbu ya Mwl Nyerere

 Waziri mkuu mstaafu mh Mizengo Peter Pinda ameongoza kikao cha Bodi ya Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kilichofanyika leo juni 08 mwaka 2025 Jijini Dar es Salaam. Katika kikao hicho mh Pinda amezungumzia umuhimu wa kulinda amani ikiwa ni sehemu kumuenzi mwasisi wa Taifa la Tanzania Mwl Julius Kambarage Nyerere, na kuendelea kuyaenzi mazuri yote tulioachiwa na Baba wa Taifa ikiwa ni pamoja na kupinga rushwa hasa katika kipindi hiki tunachoelekea kwenye uchaguzi Mkuu wa Rais,Wabunge na Madiwani.

Msama Awajia Juu Viongozi Wa Dini Wanaotumia Nyumba za Ibada Kuvuruga Amani

Mkurugenzi wa Msama promotion ALEX MSAMA amewataka viongozi wa dini nchini kuacha mara moja vitendo vya kutumia nyumba za ibada kuwa sehemu ya kuhubili siasa kwa baadhi yao nchini. Hayo amebainisha hio leo Juni 08, Mkurugenzi wa Msama Promotion, Alex Msama katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar es salaam ambapo amesema kuwa kitendo cha viongozi hao ni kuikosea serikali na ni kitendo kisichofaa na ni kushindana na agizo la Mungu na kwani kufanya hivyo ni kumkosoa mungu kupitia tabia zisizo za kiungwana za kutoheshimu mamlaka za serikali na miimili yake. Aidha, Msama amesema kuwa yote yanayofanyika na Rais samia Suluhu Hassan ni maerekezo ya Mwenyezi Mungu hivyo ni busara kutii mamlaka ya serikali kwani kile kinachofanyika na Rais ni hitajio la mungu kwa watanzania. Hata hivyo pia Msama ametoa rai kwa watanzania kuacha kutumia lugha za matusi na zisizofaa mitandaoni na katika jamii, kwani kufanya hivyo kunaweza kusababisha mmomonyoko wa maadili huku akilitaka jeshi la...

Mbunge Ghati Chomete Ampongeza Rc Mtambi Kwa Maonyesho Bora ya Madini

  Na Shomari Binda-Musoma  MBUNGE wa Viti maalum mkoa wa Mara Ghati Chomete amempongeza mkuu wa mkoa wa Mara Kanali Evans Mtambi kwa kuandaa kongamano la maonyesho ya madini mkoa wa Mara. Akizungumza na GMTV leo juni 8,2025 amesema maonyesho hayo ambayo yamefanyika kwa mara ya kwanza mkoani Mara yamekuwa na ubora wa hali ya juu na yameutangaza vyema mkoa. Amesema kwa mwana Mara na Mtanzania yetote ambaye amefuatilia kwa karibu maonesho ya madini yaliyofanyika mkoani Mara kuanzia tarehe 3 hadi 6 juni,2025 atakuwa ameridhishwa na ubunifu huo uliofanywa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara chini ya Mkuu wa Mkoa Kanali Evans Alfred Mtambi.  Mbunge huyo amesema maonesho hayo ambayo yalilenga kutambua fursa mbalimbali za madini katika mkoa wa Mara, kusikiliza kero na changamoto za wachimbaji na kuzipatia ufumbuzi pamoja na kuhamasisha wana Mara na Watanzania kwa ujumla kuchangamkia fursa za madini hususani katika mkoa wa Mara.  Amesema maonesho hayo pia yamechangia kuongezeka ...

Dkt. Biteko Aeleza Mapinduzi Yaliyofanywa na Serikali Sekta ya Elimu

📌 Ataka CWT wasigawanyike, ahimiza amani, upendo na mshikamano* 📌 Serikali kuendelea kuajiri walimu kila mwaka 📌 Serikali ya Awamu ya Sita yajenga madarasa 62,685 ya shule za msingi na sekondari, shule mpya za msingi na sekondari 2,611 na nyumba za walimu 1,792 📌 Serikali kufanyia tathmini ombi la kuwa na chombo kimoja cha kusimamia walimu nchini 📌 CWT yaipongeza Serikali kwa kuendelea kulipa stahiki za walimu Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Serikali imeendelea kutambua mchango wa walimu katika maendeleo ya sekta ya elimu kwani ni wazalishaji wa watalaamu mbalimbali waliopo katika sekta zote ikiwemo afya, nishati, sayansi na teknolojia. Sambamba na kufanya maboresho yatakayowaongezea walimu ari ya kufanya kazi kwa bidii, weledi, uadilifu na kutanguliza mbele maslahi ya Taifa. Mafanikio yaliyopatikana katika sekta hiyo yanachangiwa moja kwa moja na walimu. Hivyo, Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kina mchango mkubwa kwa jamii na kwa Taifa kwa ujumla kwa kuwa pamoja...

CRJE yakabidhi majengo mawili ya hosteli za wanafunzi kwa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji

"Wakati wa mradi wa ujenzi zaidi ya wafanyakazi na mafundi 200 wa kitanzania waliajiriwa na kampuni ya CRJE (East Africa) Limited katika kuimarisha ushirikiano kati ya China na Tanzania," Meneja mradi wa majengo hayo kutoka CRJE (East Africa) Limited Dai Yanwei alisema wakati wa hafla ya kukabidhi majengo hayo. Na Mwandishi Wetu KAMPUNI ya ujenzi ya kutoka nchini China, ya CRJE (East Africa) Limited imekabidhi rasmi majengo mawili ya hosteli ya wanafunzi ambayo yamekamilika kwa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT). Kukamilika kwa majengo haya kunaashiria hatua kubwa katika maendeleo ya miundombinu inayoendelea katika taasisi hiyo.  Hosteli hizo mbili ni sehemu ya mradi wa ujenzi ambao  umefadhiliwa na Benki ya Dunia chini ya Mradi wa Ujuzi wa Afrika Mashariki wa Mabadiliko na Ushirikiano wa Kikanda (EASTRIP). Mpango huu unalenga kuimarisha mazingira ya kujifunzia na kuboresha vifaa vya malazi kwa wanafunzi. Kukamilika kwa majengo hayo kunaonyesha ushirikiano mkubwa kati ya N...