Skip to main content

Posts

Showing posts from August 7, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Tuhakikishe Vijana Wanapata Mafunzo ya Ufundi Stadi-Majaliwa

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa, ametoa wito kwa wazazi na walezi kote nchini kuhakikisha wanawapeleka vijana wao kupata mafunzo ya ufundi stadi yanayoratibiwa na Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu ili kuwawezesha kupata ujuzi utakaowasaidia kujiajiri na kuchangia maendeleo ya Taifa. Akizungumza mara baada ya kukagua karakana za kujifunzia zilizopo katika Chuo cha VETA wilayani Ruangwa mkoani Lindi, Waziri Mkuu alisisitiza kuwa Serikali imewekeza kwa kiasi kikubwa katika kuimarisha miundombinu ya vyuo vya ufundi stadi pamoja na kuratibu programu za mafunzo ili kuhakikisha vijana wanapata stadi zinazokidhi mahitaji ya soko la ajira la sasa na baadaye. “Serikali inayo dhamira ya dhati ya kuhakikisha vijana wa Kitanzania wanakuwa na ujuzi. Mafunzo ya VETA na yale yanayotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu yanawawezesha vijana wetu kuajiriwa au kujiajiri wenyewe, na hii ni hatua kubwa ya maendeleo kwa familia zao na Taifa kwa ujumla,” alisema Waziri Mkuu. Katika mazungumzo ...

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Aishauri Tume ya Kurekebisha Sheria

  Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Mheshimiwa Mayeka Mayeka, ameishauri Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania kushirikiana na Halmashauri za wilaya wakati wa ukusanyaji wa maoni ya wananchi kuhusu maboresho ya sheria mbalimbali nchini. Akizungumza leo tarehe Agosti 6, 2025 wakati alipotembelea banda la Tume hiyo wakati wa maonesho ya Nanenane yanayoendelea viwanja vya Nzuguni Mkoani Dodoma , Mh. Mayeka alisema ofisi za halmashauri zina mtandao mpana wa kuwafikia wananchi, hivyo zinaweza kusaidia Tume kupata maoni ya watu wengi kutoka makundi mbalimbali ya jamii. “Ni muhimu Tume ikazitumia halmashauri kama daraja la kufikia wananchi wengi, hasa walioko vijijini, ambao mara nyingi wanakosa fursa ya kutoa maoni yao kwenye mchakato huu muhimu wa kisheria,” alisema Mh. Mayeka. Mhe.Mayeka aliongeza kuwa Sheria bora ni zile zinazotokana na ushirikishwaji wa wananchi kwa kiwango kikubwa, kwani zinakuwa zimezingatia changamoto, maoni na mahitaji halisi ya jamii. Kwa upande wake Bi. Vicky Mbunde amb...