Kutoka: Dawati la Habari Polisi Mwanza Koplo Stella Lyimo, mtendaji wa Dawati la Jinsia na Watoto Wilaya ya Nyamagana, Mkoani Mwanza, amemkabidhi Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza tuzo na vyeti alivyoipokea tarehe 25 Aprili 2026, katika hafla iliyofanyika leo, 29 Aprili 2026, katika Bwalo la Polisi Mabatini. Akipokea tuzo na vyeti hivyo, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Wilbrod Mutafungwa, amesema kuwa Jeshi la Polisi litaendelea kuthamini na kutambua mchango wa kila askari anayefanya vizuri katika majukumu yake. Aidha, aliwataka askari wote kuongeza juhudi na nidhamu mahali pa kazi. "Ninawataka askari wengine kuwajibika kikamilifu kwa kuwahudumia wananchi na kulinda raia pamoja na mali zao kama inavyopaswa.Tunalenga kuwa na taasisi inayoheshimika na kupendwa na wananchi," alisema Kamanda Mutafungwa. Katika taarifa iliyosomwa mbele ya Kamanda Mutafungwa, Mkuu wa Polisi Wilaya ya Nyamagana, SSP Virginia Sodoka, alibainisha kuwa Koplo Stella amekuwa akifanya kazi kwa umahiri mk...