Skip to main content

Posts

Showing posts from May 18, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Wanachama 158 Chadema Tanga, wakihama Chama hicho

Na Mashaka Mhando, Tanga Wanachama 158 wa Chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema Mkoani Tanga wamejiondoa kwenye chama hicho kwa madai kwamba chama hicho kimepoteza muelekeo na hivi sasa kimekuwa chama cha matusi,  kudharauliana na kukejeliana kwenye mitandao ya kijamii.  Akizungumza na waandishi wa habari jijini Tanga Mjumbe wa Kamati ya mafunzo kanda ya Kaskazini Zainab Ashraf amesema kwamba wanaondoka katika chama hicho si kwamba wanamfuata aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama hicho Freeman Mbowe bali  sababu zilizowafanya wajiondoe ni kutokana na kupoteza muelekeo wa chama hicho pamoja na kukosekana kwa demokrasia ya kweli.  "Tunajivua rasmi uanachama wa Chadema tutatafuta jukwaa jingine kwasababu wengi wetu hapa ni wanasiasa bado tuna ndoto zetu za kisiasa hazijatimia tutapata jukwaa jengine ambalo tutaliona ni rafiki na sisi kuendeleza harakati hizi za kutafuta demokrasia ya kweli na mapambano ya kweli kuwaokoa watanzania katika jukwaa tutakaloliona ni rafiki, "ali...

Majaliwa: Serikali imejipanga Kudhibiti Magugumaji Ziwa Victoria

_▪️Amshukuru Rais Dkt. Samia ununuzi wa mitambo ya uteketezaji wa magugumaji WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema Serikali imeweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha changamoto ya uwepo wa magugumaji katika ziwa Victoria inapatiwa ufumbuzi ili kuwezesha shughuli za kijamii ziweze kuendelea katika maeneo hayo. ”Ninamshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia kutoa fedha za ununuzi wa mitambo mikubwa ya kuteketeza magugumaji ndani ya ziwa Victoria ili kuwezesha shughuli za uvuvi, usafiri na usafirishaji kuendelea.” Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumatatu, Mei 19, 2025) wakati akizungumza na wananchi alipokagua shughuli ya udhibiti wa magugumaji katika eneo la Kigongo-Busisi akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani Mwanza. Mheshimiwa Majaliwa amesema magugumaji hayo yamekuwa yakiathiri kwa kiwango kikubwa shughuli mbalimbali za kijami na kiuchumi katika ziwa hilo, hivyo ununuzi wa mitambo hiyo utasaidia kuteketezwa kwa magugu hayo. Aidha, Waziri Mkuu amewashukuru wananc...

Katibu Uwt Mara Awapa Ujumbe Wanawake Musoma Mjini Kuelekea Uchaguzi Mkuu

  Na Shomari Binda-Musoma  KATIBU wa Jumuiya ya Wanawake wa CCM ( UWT) mkoa wa Mara Saadan Mwamba amewapa ujumbe wanawake wa Musoma mjini kumsemea Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kutokana na kazi nzuri anayoifanya Ujumbe huo ameutoa leo mei 18,2025 kwenye ukumbi wa CCM mkoa wa Mara alipokuwa akizungumza na viongozi wa jumuiya hiyo wa ngazi ya matawi na Kata pamoja na madiwani wa viti maalum ikiwa ni muendelezo wa ziara kwenye Wilaya. Amesema Rais Dkt.Samia amefanya kazi kubwa katika kuwaletea maendeleo wananchi ambayo wengi walikuwa hawategemei hivyo lazima wazisemee. Katibu huyo ambaye ameambata na wajumbe wa Kamati Tekelezaji ya UWT mkoa wa Mara amesema Rais Samia amegusa sekta zote kuanzia elimu,afya,maji,miundumbinu na masuala ya uchumi na cha kumlipa ni kumchagua kwa kura nyingi kwenye uchaguzi mkuu ujao. Amesema miaka 4 ya uongozi wake hakuna mzazi alichangishwa fedha shuleni shule mpya zikijengwa na kuongezwa kwa madarasa hali inayowafanya wanafunzi kusoma karibu na nyumba...

Serikali ipo Kazini na inaendelea Kufanya kazi-Majaliwa

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amewahakikishia Watanzania kwamba Serikali ipo kazini na inaendelea kufanyakazi ya kuwahudumia na kuwatumikia wananchi katika maeneo yote nchini na bila ya ubaguzi wa aina yoyote. Kadhalika, Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa wananchi waendelea kushirikiana     katika kudumisha amani na utulivu na kwamba wasiwasikilize watu wenye viashiria vya uvunjifu wa amani wanaopita katika maeneo yao. Ameyasema hayo leo (Jumapili, Mei 18, 2025) wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Kwideko, Kata ya Ngudu wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani Mwanza. ”Huu ni wakati ambao watumishi wote wanatakiwa kuwafuata wananchi katika maeneo yao na kuwaeleza miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali kwa ajili ya maendeleo yao, ambapo alitolea mfano mradi wa VETA unaojengwa katika wilaya ya Kwimba kwa gharama ya takribani shilingi bilioni mbili.” Waziri Mkuu amesema wakazi wa wilaya hi...

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa mgeni rasmi kongamano la kusoma Koran Tanga

Na Mashaka Mhando, Tanga BARAZA la Masheikh mkoani Tanga, limeandaa kongamano la kimataifa la kusoma Koran (Tawhid) ambapo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa atakuwa mgeni rasmi. Akizungumza na Waandishi wa habari leo Mei 18, 2025, Sharifu Muhannah Ahmad ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa ushirikiano wa Masheikh mkoani Tanga, alisema kongamano hilo litafanyika Mei 24 mwaka huu kwenye uwanja wa Mkwakwani. Sharifu Muhannah alisema kongamano hilo litakalojuisha wasoma Koran kutoka ndani na nje ya Tanzania,  Alitakuwa na watu 13,000 watakaoshindana Kusoma Tawhid. Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Taasisi ya Kiislamu ya TAMTA Shamsiyah, Mohamed Abduh Dhikiri, alisema kongamano hili litakaloanza saa 8:000 asubuhi hadi saa 6:00 mchana litahushuriwa na wasomaji wa Kimataifa. Naibu Mudir wa taasisi ya Shamsiyah Sheikh Ramani Mabruk alisema umuhimu wa kongamano hilo ni kuwaunganisha watu wawe kitu kimoja kuhakikisha kwamba kitabu cha Koran kimeletwa na Mungu kuwaunganisha pamoja. "Kongamano hilo litakuwa...