Na Shomari Binda-Musoma UWEKEZAJI wa ujenzi wa ukumbi mkubwa wa mikutano unaojengwa na Chama cha Mapinduzi ( CCM) mkoa wa Mara umefikia asilimia 65. Hayo yamesemwa na Katibu wa chama hicho mkoa wa Mara Ibrahim Mjanakher alipokuwa akifanya mahojiano maalum na GMTV. Amesema hadi ukumbi huo kufikia hapo ni juhudi za wanachama na wadau mbalimbali wa chama hicho mkoani Mara na nje ya mkoa wa Mara. Mjanakher amesema hadi sasa zaidi ya milioni 700 zimetumika kwenye ujenzi huo unaotarajiwa kuchukua watu zaidi ya 2000 kwa wakati mmoja. Amesema uwekezaji wa ukumbi huo ni maelekezo ya chama ngazi ya Taifa chini ya Mwenyekiti Dkt.Samia Suluhu Hassan ya kutaka chama kuwa na miradi kila ngazi ili kiweze kujiendesha. Katibu huyo amesema ujenzi wa ukumbi huo una simamiwa vixuri chini ya Mwenyekiti wa mkoa wa CCM Patrick Chandi chini ya kamati ya ujenzi inayoongozwa na Mwita Gachuma. " Nashukuru ndugu Mwandishi kwa kutembelea hapa ofisini na kuona maendeleo ya ujenzi wa ukumbi wa mikutano u...
Marato tv - Sauti ya Jamii