Na Dawati la Habari Polisi Mwanza Madereva wa boda boda watakiwa kuvaa kofia ngumu na kufata Sheria za usalama barabarani pindi wanapotumia pikipiki ili kuepukana na ajali ambazo zinaweza wapelekea kupoteza nguvu kazi ya taifa. Hayo yamebainishwa Oktoba 24.2024 na Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Mwanza Mrakibu wa Polisi (SP) Sunday Ibrahim wakati akitoa elimu ya usalama barabarani kwa waendesha boda boda wa vituo vya kata za Nyegezi, Luchelele na Mkolani wilayani Nyamagana mkoani Mwanza. Akizungumza na madereva wa boda boda hao kutoka kanda ya Mwanza kusini,Sunday amesema elimu hiyo imelenga kuwapa uelewa makundi mengine ya watumiaji wa barabara hususan bodaboda ili kuzuia ajali zinazoweza kuepukika. Aidha, SP Sunday amesema, atahakikisha operesheni inayoendelea haimuacha mtu ambapo watakaobaini kutovaa Korea ngumu kinyume cha sheria watachukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kufikishwa mahakamani. " wengi mnasema abiria hataki ...
Marato tv - Sauti ya Jamii