Skip to main content

Posts

Showing posts from June 4, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Majaliwa: Tbs Hakikisheni Soko la Tanzania Linakuwa na Bidhaa Bora

_▪️Asisitiza Tanzania sio shimo la bidhaa zisizokuwa na ubora_ _▪️Ataka viwanda kuzalisha bidhaa bora zinazouzika ndani na nje ya nchi_   WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameutaka uongozi wa Shirika la Viwango Tanzania kutokuwa na huruma na bidhaa zisizokuwa na ubora kwani Serikali inataka soko la Tanzania liwe na bidhaa bora, salama na zenye kuleta tija kwa mlaji na kwa uchumi. Amewataka wazalishaji wa bidhaa na huduma, wahakikishe wanazingatia taratibu za vipimo, uthibitishaji wa ubora, na uboreshaji wa mifumo ya uzalishaji. “Muhakikishe bidhaa zenu zinakidhi viwango vya kitaifa na kimataifa vilivyowekwa na TBS”. Ametoa maagizo hayo leo (Jumatano, Juni 4, 2025) baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la maabara na ofisi za Shirika la Viwango Tanzania (TBS) katika eneo la Njedengwa jijini Dodoma, ambapo amesisitiza kufuatwa kwa viwango vya ubora. Waziri Mkuu ametoa wito kwa wafanyabiashara na waagizaji wa bidhaa kutoka nje ya nchi, wana wajibu wa kuhakikisha bidhaa wanazoing...

Bil 26.9 Kugharamia Ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji Mwamapuli

📍NIRC:Igunga Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), imeingia mkataba na mkandarasi mzawa kampuni ya Samota limited kujenga mradi wa skimu ya umwagiliaji Mwamapuli, katika kijiji cha Mwanzugi wilayani Igunga mkoani Tabora,  mradi ambao utagharimu zaidi ya shilingi bilioni 26.9. Aidha mradi huo utajengwa kwa zaidi ya siku 720, ukiwa unalenga kuongeza eneo la umwaagiliaji kutoka hekta 630 , hadi kufikia hekta 2397,  huku zaidi ya wakulima 2470 wakitarajiwa kunufaika kutokana na mradi huo Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Paul chacha, amemtaka mkandarasi mzawa kampuni ya Samota LTD, anayetekeleza mradi huo kufanya kazi kwa ufanisi na kwa muda wa makubaliano. Alisema ni muhimu mkandarasi huyo kuheshimu makubaliano na kuzingatia uhitaji wa wananchi  “Serikali ina nia njema lengo ni mradi umalizike kwa wakati ili  uweze kuanza kuwanufaisha wananchi,”alisema.  Akisoma taarifa ya ujenzi wa mradi huo Mhandisi  wa Umwagiliaji Mkoa w...

Kiwanda Cha Kusafisha na Kuongeza Thamani Madini Adimu Kujengwa Kijijini Ngwala,Songwe

▪️Uendelezaji wa Mradi kuanza rasmi    Disemba 2025 ▪️Ni mradi wa Madini Adimu utakaogharimu Bilioni 771 ▪️Waziri Mavunde azindua zoezi la ulipwaji fidia wananchi 192 ▪️Wananchi wamshukuru Rais Samia kwa mazingira ya uwekezaji ▪️Serikali kuvuna mapato ya zaidi ya Trilioni 12  Ngwala,Songwe Kampuni ya Mamba Minerals Ltd inayowekeza kwenye mradi wa Madini adimu imeweka wazi mpango wake wa kujenga kiwanda cha kusafisha na kuongeza thamani madini adimu kijijini,Ngwala Mkoani Songwe badala ya kusafirisha madini hayo yakiwa ghafi. Hayo yamesemwa leo Kijijini Ngwala,Songwe wakati wa uzinduzi wa zoezi la ulipwaji fidia wananchi waguswa wa mradi takribani 192 zoezi ambalo limezunduliwa na Waziri wa Madini Mh. Anthony Mavunde. Akitoa maelezo ya awali,Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Mamba Minerals Ltd Ndg. Ismail Diwani amesema zoezi hilo la fidia litagharimu kiasi cha Tsh 5.3 Bilioni kwa kuhusisha wananchi waguswa wa mradi 192 ambapo mpaka sasa wananchi 116 wamepokea malipo yao tayari....

Majaliwa:Halmashauri Nchini Zatakiwa kuwa na Vituo vya Kuchakata Taka

Na  Mwandishi wetu Jovina Massano. WAZIRI MKUU wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa amezitaka halmashauri zote nchini kuhakikisha  zinaweka vituo vya kuchakata na kutenganisha taka ili zinapozalishwa ziweze kushughulikiwa kwa njia salama na endelevu, kwa lengo la kupunguza mzigo wa taka majalalani na kusambaa ovyo katika makazi ya watu. Ametoa maagizo hayo Juni 03, 2025 wakati akizungumza na vijana katika Jukwaa la Vijana na Mazingira lililofanyika katika Ukumbi wa Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambayo hufanyika Juni 5 kila mwaka ambapo kitaifa yatafanyika Jijini Dodoma. Waziri Mkuu amesema jukwaa hilo la vijana na mazingira linalenga kuwaunganisha vijana kutoka sehemu mbalimbali nchini na kuwajengea uelewa kuhusu masuala ya utunzaji wa mazingira pamoja na kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika kubuni na kutekeleza mikakati ya kutatua changamoto za mazingira nchini. Usafi wa mazingira na udhibi...