OFISI ya Taifa ya Takwimu (NBS) imezindua matokeo ya tafiti mbili muhimu zilizotajwa kuwa miongoni mwa nyenzo zitakazosaidia Taifa kupanga maendeleo kwa kutumia takwimu sahihi kuelekea Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Tafiti hizo ni Utafiti wa Uwezeshwaji Wanawake na Lishe wa Mwaka wa Kilimo 2023/2024 pamoja na Utafiti wa Mazingira na Jinsia wa mwaka 2025, zilizofanywa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wakiwemo Benki ya Dunia, Shirika la Chakula la Umoja wa Mataifa (FAO) na UN Women. Akizindua Tafiti hizo leo Mei 6, 2026 katika Makao Makuu ya ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) jijini Dodoma, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima, amesema Tafiti hizo zimefungua ukurasa mpya wa matumizi ya takwimu katika kuibua suluhisho la changamoto zinazoikabili jamii. “Hizi ni tafiti za kwanza kufanyika Tanzania, na kwa upande wa Afrika, utafiti wa mazingira na jinsia ni wa pili baada ya Senegal. Hii ni fahari kubwa kwa Taifa letu,” amesema Dkt. Gwajim...
Marato tv - Sauti ya Jamii