Skip to main content

Posts

Showing posts from May 13, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Majaliwa Ateta Na Waziri Mkuu Wa Côte D'ivoire

_▪️Wakubaliana kuanzishwa kwa Jukwaa la Wafanyabiashara_   WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amekutana na Waziri Mkuu wa Côte d'Ivoire, Robert Beugre Mambe na kujadiliana naye masuala ya kidiplomasia, kiuchumi, teknolojia, kilimo na michezo kwenye kikao kilichofanyika ofisini kwa mwenyeji wake, Boulevard Angoulvant Plateau, jijini Abidjan. Akitoa ufafanuzi mara baada ya kikao hicho jana jioni (Jumanne, Mei 13, 2025), Waziri Mkuu Majaliwa alisema lengo la kikao chao lilikuwa kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia lakini pia kuhimiza haja ya nchi hiyo kushirikiana na Tanzania kwenye masuala mbalimbali ikiwemo utafiti na teknolojia za kisasa kwenye kilimo. “Côte d'Ivoire ina wakazi zaidi ya milioni 31 na inaongoza kwa kilimo cha kakao, korosho na michikichi. Hawa wanalima korosho zaidi kuliko Tanzania, na sisi tunalima korosho kwenye mikoa ya Pwani na kakao kule Mbeya na maeneo mengine. Tunaweza kujifunza kwao na sisi tunaiona hii ni fursa kwetu ya kuongeza uzalishaji kwenye mazao haya.” ...

Waziri Tax yupo nchini Ujerumani kwa ziara ya kikazi

  Mhe. Dkt. Stergomena Lawrence Tax (Mb), Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ametembelea Ubalozi wa Tanzania Berlin, Ujerumani na kupokelewa na Mheshimiwa Hassani Iddi Mwamweta, Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani. Mheshimiwa Waziri Tax yuko Ujerumani kushiriki Mkutano wa Mawaziri wa Ulinzi wa Nchi zinazoshiriki Operesheni za Amani za Umoja wa Mataifa (UNPeacekeeping Ministerial Conference 2025) kuanzia tarehe 13 - 14 Mei 2025 Berlin, Ujerumani.

Wabunge wafungiwa ofisi, vyoo KICC kutokana na malimbikizi ya kodi

 WABUNGE Nchini Kenya Jumanne walifungiwa nje ya afisi zao katika Jumba la Kimataifa la Mikutano la KICC kutokana na malimbikizi ya kodi ambayo sasa ni Sh50 milioni. Pia walioathirika kutokana na utata kati ya KICC na Bunge ni wafanyakazi wa Tume ya Huduma za Bunge (PSC) ambao wana ofisi zao katika jengo hilo. Mnamo Jumanne, Seneti iliwaambia wanachama wake kuhusu tukio hilo huku PSC ikimwaandikia Afisa Mkuu Mtendaji wa KICC, James Mwaura, kuhusu utata wenyewe. Katika barua yake, Seneti iliomba wanachama wake watumie afisi zao ikiahidi kwamba deni hilo litalipwa kabla ya kutamatika kwa mwaka huu wa fedha. “Habari za asubuhi maseneta. Nawafahamisha kuwa kutokana na malimbikizi ya kodi, usimamizi wa KICC umefungia afisi zetu na pia maegesho,” ikasema sehemu ya notisi. “Kodi hiyo hulipwa na bunge na tumefahamishwa kuwa juhudi zinaendelea kushughulikia suala hili. Tunasikitikia usumbufu ambao suala hili umesababishia wafanyakazi,” ikaongeza. PSC katika barua iliyoandikwa Mei 9 iliomba ...

Taasisi ya Nasimama na Mama Yajitambulisha Rasmi Kwa Rc Mtambi

Na Shomari Binda-Musoma  TAASISI ya Nasimama na Mama imejitambulisha dasmi kwa mkuu wa mkoa wa Mara Kanali Evans Mtambi tayari kwa kufanya kazi ya kusemea mazuri yanayofanywa na Rais Dkt.Ssmia Suluhu. Viongozi wa taasisi hiyo wamejitambulisha jana mei 12,2025 ofisini kwa mkuu huyo wa mkoa baada ya kupokelewa na kufanya nae mazungumzo. Akizungumza ofisini hapo,Mwenyekiti wa taasisi hiyo Cde.Ibrahim Assey amesema lengo la kuanzishwa kwa taasisi hiyo licha ya kumsemea Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan ni kuifikia jamii yakiwemo makundi ya vijana,wanawake na makundi maalum na kuelezea fursa mbalimbali za kiuchumi zilizopo mkoa wa Mara. Amesema zipo fursa kwenye sekta ya kilimo,uvuvi,elimu na ujasiliamali kupitia mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri ambapo wananchi wanapaswa kupata uelewa wake. Mwenyekiti huyo amesema ili kufikia malengo ya kuifikia jamii nakufikisha elimu wanahitaji kupata ushirikiano kupitia ofisi mbalimbali. Amesema watahakikisha wanatekeleza majukumu yao pamo...

Zaidi ya Wakenya Elfu Moja Wanazuiliwa kwenye Magereza Mbalimbali Ulimwenguni Kwa Makosa ikiwemo ya Ulanguzi wa dawa za Kulevya

 MKUU wa Mawaziri Nchini Kenya Musalia Mudavadi amewaomba wabunge watenge pesa zaidi kwa Wizara ya Kigeni ili serikali iweze kukodi huduma za mawakili kwa Wakenya wanaozuiliwa katika mataifa ya ng’ambo. Hayo yanajiri huku Bw Mudavadi akitoa onyo kali kwa kampuni bandia za kuwasaidia Wakenya kupata ajira ng’ambo zinazowapunja na kupotosha raia hao, hasa vijana. Alisema kuwa wamiliki wa kampuni hizo watanaswa na kushtakiwa kwa mujibu wa sheria. Kuhusu Wakenya wanaozuiliwa katika magereza ya ng’ambo, Bw Mudavadi aliwaambia wabunge kuwa idadi yao ni zaidi ya 1,000. Wamezuiliwa kwa makosa mbalimbali ikiwemo ulanguzi wa dawa za kulevya. Hata hivyo, Mkuu huyo wa Mawaziri ambaye pia ni Waziri wa Masuala ya Kigeni alisema kuwa idadi kubwa ya Wakenya hao wanakosa huduma za mawakili wa kuwatetea, kutokana na uhaba wa mgao wa bajeti. Bw Mudavadi alisema Bunge la Kitaifa halijatengea wizara hiyo fedha za kutosha ili iweze kuchukua hatua ya kukodisha mawakili wa kuwatetea Wakenya walioko magerez...

Machinga Dodoma Wampongeza Rais Samia Kwa Ujenzi Wa Soko la Kisasa

▪️Ni soko kubwa la kipekee la Machinga Complex ▪️Machinga Wanawake Dodoma wazindua Umoja wao ▪️RC Senyamule ataka Jiji kuongeza maeneo ya kufanyia biashara  ▪️Mbunge Mavunde awataka Machinga Dodoma kuchangamkia Mkopo wa Bilioni 7 za Jiji *Dodoma* Umoja wa Wanawake Machinga Dodoma(UWAMADO) wamempongeza Mh. Rais Dkt. Samia S. Hassan kwa ujenzi wa soko la kisasa la Machinga Complex na miundombinu ya kisasa ya soko hilo ambalo ni la kipekee nchini. Hayo yamesemwa jana wakati wa uzinduzi wa chama cha UWAMADO uliofanyika kwenye eneo la soko la Machinga Complex kwa kuzinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mh. Rosemary Senyamule.  Akisoma Risala Katibu wa UWAMADO Bi. Mariam Kajembe amesema umoja huo umelenga kuwaleta wanawake Machinga pamoja ili kujijenga na kujiimarisha uchumi. Aidha pia UWAMADO umempongeza Mh. Rais Dkt. Samia S. Hassan kwa ujenzi wa Soko la Machinga Complex ambalo limesaidia kuwaleta pamoja wafanyabiashara wengi wadogo pamoja ambao awali hawakuwa katika maeneo rasmi na...

Mchango wa Mbunge Waitara Kwenye Bajeti ya Elimu Wapokelewa na Wananchi

Na Shomari Binda-GMTV MCHANGO uliotolewa na mbunge wa jimbo la Tarime Vijijini Mwita Waitara kwenye Bajeti ya Wizara ya Elimu kuhusu umuhimu wa masomo ya Sayansi umepokelewa vyema na wananchi. Wakizungumza na GMTV jana mei 12,2025 wakati wakifatilia michango ya wabunge kwenye bajeti hiyo wamesema kile ambacho kimechangiwa na mbunge Waitara kina umuhimu mkubwa. Mmoja wa wananchi hao aliyekuwa akifatiliàeneo la garden manispaa ya Musoma Juma Kitundu amesema katika soko la ajira la sasa wana sayansi wana nafasi kubwa. Amesema alichokichangia mbunge huyo kina ukweli kuhisu mitaala mipya ya elimu kuzingatia suala la kuwapa uelewa walimu ili wafundishe wanafunzi kwa tija. Juma amesema masomo ya sayansi yana nafasi kubwa kwa sasa lakini zipo nyenzo za ufundishaji zinazohitajika ambazo zinapaswa kuwepo shuleni zikiwemo maabara. " Nimekuwa nikimuelewa sana mbunge Waitara kwenye michango yake anapokuwa bungeni na anapochangia masuala mbalimbali. " Kwenye hili la Wizara ya Elimu Sayansi...