Skip to main content

Posts

Showing posts from May 15, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Waziri Mavunde: Tani 3.7 za Dhahabu Zanunuliwa Bot

▪️ *Tanzania yaipiku Msumbiji, yaingia 10 bora Afrika* ▪️. *Dhahabu kubadilishwa kwa mafuta, fedha za kigeni* 📍 *Dodoma* WAZIRI wa Madini Mhe. Anthony Mavunde aliweka  wazi mafanikio 16 ya Sekta ya Madini katika kipindi cha Miaka Minne ya Rais Samia Suluhu Hassan ikiwemo Benki Kuu ya Tanzania kununua Tani 3.7 kwa gharama ya Shilingi 702.3 Bilioni. Akizungumza na Waandishi wa Habari  Mei 15, 2025, katika ukumbi wa Idara ya habari (MAELEZO), Waziri Mavunde alisema kati ya kiasi kilichonunuliwa takribani, Kilo 2,954 zilisafishwa katika viwanda vya kusafisha dhahabu vilivyoko nchini. Mhe. Mavunde alisema katika Bara la Afrika nchi tano zinazofanya vizuri katika ununuzi wa dhahabu, Tanzania ipo huku nchi ya Algeria ikiongoza. “Miaka mingi nchi yetu iliacha kununua dhahabu kupitia Benki Kuu, lakini mwaka wa fedha 2024/2025 tulifanya marekebisho ya Sheria ya Madini kifungu cha 59 sura ya 123 ambacho kinampa dhamana Waziri wa Madini kujadiliana na wamiliki wa leseni kutenga asilimia ...

Sagini Akamilisha Ujenzi Ofisi Ya Ccm Kitaramanka Awekwa Katika Maombi ya Kila Siku

📍JIMBONI BUTIAMA Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tawi la Kitaramanka wameungana na wananchi wengine kumuweka rasmi Mbunge wa Jimbo la Butiama na Naibu Waziri Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini katika maombi ya kila siku mpaka atakapopitishwa kwenye uchaguzi ujao baada ya kuwakamilishia ujenzi wa Ofisi ya Chama. Wakizungumza katika hafla fupi ya makabidhiano ya bando za bati kutoka kwa Watumishi Ofisi ya Mbunge Afisa Mahusiano Ndg. Japhet Changarawe na Katibu Ndg. Samson Malima wamesema kuwa Mbunge Sagini aliwahidi kuwachangia kiasi katika ujenzi lakini amefanya zaidi kwani amejenga na kukamilisha ofisi hivyo tayari wamemthibitisha kumuombea mema kila siku ili azidi kuendelea kuiongoza Butiama.  "Kwa maendeleo na mambo mema aliyotufanyia Mbunge Sagini Wanachama wote tulikaa kikao cha kumuweka katika maombi ya kila siku ili Mwenyezi Mungu amuongezee pale alipotoa pia amjalie afya njema na katika uchaguzi wa mwaka huu apite kwa kishindo maana tunaimani naye na hatuko tayari...

Rea yaendelea na Uhamasishaji Matumizi Bora ya Nishati ya Umeme, na Uunganishaji Wateja Mkoa wa Morogoro

📌Wananchi wapewa elimu matumizi  bora ya nishati ya umeme 📌Wahimizwa kujiunganisha na huduma ya umeme 📌Wananchi wahamasika na UMEME TAYARI ( Ready Board) Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuhamasisha matumizi sahihi na endelevu ya umeme kwa Watanzania ikiwa pamoja na   kutoa elimu kwa umma kuhusu matumizi bora ya nishati, kuhamasisha kuunganisha umeme, tahadhari za umeme pamoja na utunzaji wa miundombinu ya umeme.  Hayo yamebainishwa na Wataalam wa REA, TANESCO na Mkandarasi waliofika kutoa elimu kwa wananchi kuhusu kutumia fursa ya miradi ya REA inayotekelezwa mkoani Morogoro.  Akizungumza katika mkutano na wananchi, Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka REA, Abdulrazack Mkomi amesema kuwa, lengo na dhamira ya serikali ni kuona mabadiliko yanatokea katika maeneo ya vijijini hasa kwenye nyanja za kiuchumi kama kuongezeka kwa fursa za ajira na viwanda vidogo vidogo, kuboresha sekta ya afya, sekta ya elimu na huduma zote muhimu za kijamii kwa ujumla.  ...

Balozi Yakubu akutana na Katibu Mkuu Kiongozi Comoro

Balozi wa Tanzania nchini Comoro Mhe. Saidi Yakubu amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu Kiongozi wa Comoro Mhe. Nour el Fatih Azali ambapo wamezungumzia masuala kadhaa ya ushirikiano wa Tanzania na Comoro. Balozi Yakubu alitumia fursa hiyo kumuelezea kusudio la ubalozi la kufanya kongamano kubwa la Biashara na Uwekezaji mwezi ujao kwa ushirikiano na Serikali ya Comoro katika maeneo ya Uzalishaji, Ujenzi na Tehama. Aidha, Balozi Yakubu aliwasilisha pia masuala kadhaa ya kufanyiwa kazi na Serikali ya Comoro ambapo Katibu Mkuu Kiongozi Fatih aliyapokea na kuahidi kufanyiwa kazi. Bwana Fatih pia alimueleza Balozi Yakubu kuwa mwaka huu Taifa la Comoro litasherehekea miaka 50 ya uhuru na matukio kadhaa yamepangwa kufanyika na wanatarajia ushiriki wa Taasisi kadhaa za Tanzania. Mkutano huo ulifanyika katika viunga vya Ikulu ya Comoro.

Mfalme Zumaridi Mikononi Jeshi la Polisi

  Jeshi la Polisi mkoani mwanza linamshikilia Diana Bundala kwa tuhuma za kugeuza makazi yake kuwa kanisa,kuendesha shughuli za kidini bila kuwa na usajili pamoja na kuhubiri kwa sauti ya Juu.  Kamanda wa polisi mkoa mwanza Naibu Kamishna wa Polisi Wilbroad Mutafungwa amesema kuwa Bundala Maarufu kwa Jina la Mfalme Zumaridi,Mkazi wa mtaa wa Buguku kata ya Buhongwa Jijini mwanza pia anahojiwa kuhusiana picha Mjongeo inayoendelea kusambaa kwenye mitandao ya kijamii ikimuonyesha akiwaeleza watoto kuwa yeye ndiye mungu wao.  Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda Mutafungwa amesema Polisi inaendelea na uchunguzi wa tuhuma zinazomkabili Mfalme Zumaridi kwa kushirikiana na Taasisi nyingine za serikali.  Aidha ameowaomba wananchi wenye Taarifa mbalimbali zinazoweza kusaidia uchunguzi wa tuhuma dhidi ya Mfalme Zumaridi kuziwasilisha Polisi.  Kwa mujibu wa Kamanda Mutafungwa,Uchunguzi huo utakapokamilika hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya mtuhumiwa.  Hii ...

Rc Mtambi Apokea Tuzo ya Manispaa ya Musoma Kutoa Huduma Bora za Afya Kitaifa

Na Shomari Binda-Musoma  MKUU wa mkoa wa Mara Kanali Evans Mtambi amepokea tuzo 2 za utoaji huduma bora za afya ķitaifa kwa manispaa ya Musoma. Tuzo hizo zimetolewa hivi karibuni na Wizara ya Afya kwa kushirikiana na TAMISEMI kwa manispaa hiyo kuoitia kituo cha afya Nyasho na zahanati ya Kwangwa kwa kufanya vizuri kitaifa. Akipokea tuzo hizo hii leo mei 15,2025 kutoka kwa viongozi wa bituo hivyo na wataalam wa afya amesema tuzo hizo zimeutangaza vyema mkoa wa Mara kitaifa kwa kufanya mambo mazuri. Kanali Mtambi amewapongeza viongozi wa vituo hivyo na wasimamizi wa huduma za afya manuspaa ya Musoma na mkoa wa Mara kwa kazi nzuri.  Amesema vituo hivyo kushinda kufuatia tathmini iliyofanywa na wataalamu wa afya hapa nchini sio jambo dogo na pongezi zinastahili kutolewa. “Kwa niaba ya wananchi wa mkoa wa Mara ninakipongeza Kituo cha Afya Nyasho na Zahanati ya Kwangwa kwa utoaji wa huduma nzuri kwa wananchi na kwa ushindi walioupata kitaifa ambao umetuletea heshima katika mkoa wetu...

Jeshi La Polisi Mkoa wa Kagera Limepokea Magari 14 Kutoka Kwa Rais Samia

Na Angela  Sebastian ;Bukoba Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ametoa magari 14 mapya kwa jeshi la polisi mkoani Kagera kwa kipindi cha mwezi Januari hadi sasa lengo likiwa ni  kuimalisha utendaji kazi na kuhakisha wanafanya kazi kwa weledi na kuwafikia wananchi kwa  wakati popote walipo. Hayo yamebainishwa na Kamanda wa jeshi hilo mkoani humo Blasius Chatanda wakati akikabidhi magari sita kati ya hayo yaliyotolewa kwa  makamanda wa polisi wa  Wilaya za mkoa huo leo mjini Bukoba ambapo, amesema mkoa huo si salama tena kwa waharifu kufanya vitendo viovu maana jeshi hilo limejipanga kukabiliana nao kikamilifu. "Tunaishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Dk. Samia katufanyia makubwa tunayo kila sababu ya kumshukuru ni kwa mara ya kwanza, katika historia polisi mkoa wa Kagera kupata magari 14 kwa kipindi cha miezi mitatu hivyo hii inaashiria usalama mkubwa kwa wananchi mkoani  humu"ameeleza Chatanda Amesema wananchi wanalidai  jeshi...

Sekta ya Madini Yakusanya Zaidi ya Bilioni 902 Kati ya Lengo la Trilioni Moja

*Mchango Wafikia Asilimia 10. 1 katika Pato la Taifa (GDP) kwa mmoja kabla ya lengo*  📍 *Dodoma* Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, amebainisha kuwa Sekta ya Madini nchini imeendelea kupiga hatua kubwa, ambapo maduhuli ya zaidi ya shilingi bilioni 902 sawa na asilimia 90.2 ya lengo la kukusanya Shilingi trilioni moja kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025 kufikia Mei 15, 2025, ikiwa ni kabla ya kumalizika kwa Mwaka wa Fedha, huku zikiwa zimesalia zaidi ya siku 45, jambo linalotoa matumaini makubwa kuwa lengo litafikiwa kwa asilimia 100. Ameyasema hayo leo Mei 15, 2025, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma kuhusu mafanikio makubwa yaliyopatikana katika Kipindi cha Miaka Minne ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. Waziri Mavunde ameeleza kuwa, Sera ya Madini ya Mwaka 2009 na Mpango wa Miaka Mitano wa Maendeleo ya Taifa ulielekeza Sekta ya Madini ikichangia asilimia 10 ya Pato la Taifa ifikapo mwaka 2025. Hata hivyo, tay...

Rasmi, Huduma Sekta ya Madini Kupatikana Makao Makuu ya Wizara Mtumba

*Yatimiza Ahadi yake Kwa Kamati ya Nishati na Madini* *Dodoma* Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde amesema kwamba  kuanzia  Mei 15, 2025 huduma mbalimbali zinazotolewa  na Wizara ya Madini zitaanza kutolewa rasmi katika jengo la Makao Makuu ya Wizara hiyo lililopo eneo la Mtumba, Mji wa Serikali kutokana na kukamilika kwa mradi wa jengo hilo. Hayo yamebainishwa leo Mei 15, 2025 na Mhe. Mavunde wakati akizungumza na Menejimenti  ya Wizara, taasisi zake pamoja  na watumishi wa Wizara. Waziri Mavunde ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiwezesha Wizara kukamilisha jengo ambalo kwa sasa huduma zote zitatolewa hapo. Akielezea kuhusu hali ilivyokuwa ,Waziri Mavunde ameeleza kuwa , awali huduma zilikuwa zinapatikana sehemu tofauti tofauti kutokana na ofisi kuwa mbalimbali lakini na kueleza kwamba sasa  huduma zitatolewa sehemu moja  na hivyo wadau kuondokana na usumbufu....