Skip to main content

Posts

Showing posts from February 17, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mtambi Amtaka Mkandarasi Kukamilisha Mradi Kwa Wakati

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi, Februari 17 Mwaka huu ameshuhudia makabidhiano ya mradi wa uchimbaji wa visima saba vya kilimo cha umwagiliaji katika Mkoa wa Mara na kumtaka mkandarasi wa mradi huo kukamilisha mradi huo kwa wakati.  Mhe. Mtambi ametoa maagizo hayo katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika kijiji cha Kwikuba, Kata ya Busambara Halmashauri ya Wilaya ya Musoma na kumtaka mkandarasi huyo na wengine wote ndani ya Mkoa wa Mara kutekeleza miradi yao kwa wakati.  “Serikali imekupatia zabuni hii baada ya kujiridhisha na uwezo wa kampuni yenu, sasa Mkoa wa Mara hatutaki visingizio katika utekelezaji wa mradi huu kama kuna changamoto tutaarifiwe mapema ili kuweza kuitatua” amesema Mhe. Mtambi.  Mhe. Mtambi anasema miradi ya maendeleo inalenga kutatua changamoto za wananchi na kuwataka wakandarasi wote wa Mkoa wa Mara kujitahidi kukamilisha miradai yao kwa wakati ili iweze kutumika na kutatua kero za wananchi wa Mkoa wa Mara.  Kanal...

Mtambi Akemea Uvuvi Haramu Mara

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 17 Februari, 2025 amefanya mkutano wa hadhara na wananchi wa Kijiji cha Kwikuba, Kata ya Busambara, Halmashauri ya Wilaya ya Musoma na kuwakemea watu wote wanaojihusisha na uvuvi haramu katika Ziwa Victoria.  Mhe. Mtambi pia amewataka wananchi wote wa Mkoa wa Mara kuungana na kukemea uvuvi haramu na kutoa taarifa zinatazowezesha kuwakamata wanaojihusisha na uvuvi haramu katika ziwa Victoria ili waweze kuchukuliwa hatua za kisheria.  “Wanachokifanya ni kuhujumu misingi ya kiuchumi ya wananchi wote wanaotegemea Ziwa Victoria na mwisho wake tunajitengenezea umaskini na Serikali ya Mkoa wa Mara haitakubali hilo litokee” amesema Mhe. Mtambi.  Mhe. Mtambi amesema Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mara inajiandaa kufanya operesheni maalum ya kudhibiti uvuvi haramu katika Ziwa Victoria hivi karibuni na itawachukulia hatua za kisheria watu wote wanakaojihusisha na uvuvi haramu watakaokamatwa katika operesheni hiyo.  M...

Wakuu Wa Wilaya Musoma/ Rorya Tokeni Ofisini

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 17 Februari, 2025 ameitembelea kambi ya wagonjwa wa kuharisha na kutapika katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma na kuwaagiza wakuu wa Wilaya za Musoma na Rorya pamoja na wataalamu wa Halmashauri kutoka ofisini na kushughulikia chanzo cha ugonjwa huo.  Mhe. Mtambi ametoa maagizo hayo katika Zahanati ya Bwai ambayo kwa sasa inatumika kama Kituo cha Halmashauri ya Musoma kwa ajili ya kutibu wagonjwa wa kuharisha na kutapika katika eneo hilo na kujionea hali halisi ya kituo hicho na kuzungumza na viongozi, wataalamu na wananchi waliokuwepo eneo hilo.  “Ninawataka Wakuu wa Wilaya na Wataalamu wa Halmashauri za Wilaya ya Musoma na Rorya kutoka ofisini na kufanya kampeni maalum ya ujenzi wa vyoo katika maeneo ambayo yamekumbwa na tatizo hilo na kushughulikia chongamoto zozote zinazoweza kuendeleza changamoto hizi katika maeneo yao” amesema Mhe. Mtambi.  Mhe. Mtambi amezitaka Wilaya hizo kuanzisha operesheni maalum ...

Afungwa Miaka Mitatu Jela Kwa Kung'ata Watu Wawili

Mahakama ya Wilaya Sengerema mkoani Mwanza imemhukumu kwenda jela miaka mitatu Mkazi wa Kijiji cha Soswa wilayani humo, Amos John Malaki  (30) baada ya kukutwa na hatia ya kuwajeruhi watu wawili kwa kuwang'ata. Mshtakiwa amefikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza leo 17.02.2025 na kusomewa mashtaka hayo katika kesi hiyo ya Jinai namba 4079/2025 na kwa hiari yake bila kuisumbua mahakama amekiri kutenda makosa ya kuwajeruhi watu hao wawili. Awali akisoma mashtaka Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Nyamhanga Tissoro aliieleza mahakama kuwa mshtakiwa alitenda makosa hayo Januari 08, 2025, Saa 5: 57 usiku kwa kumng'ata  Regina Thomas kwenye jicho.  Katika tukio lingine lililotokea Januari 09,2025 Saa 6:01 usiku, mshtakiwa alimng'ata kidole gumba cha mkono wa kulia, Mashaka Idd Daudi aliyefika kuamua ugomvi na akakiondoa kabisa kinyume na vifungu vya 225 cha sheria ya kanuni ya Adhabu sura ya 16 marejeo ya mwaka 2022. Amos Malaki ametiwa hatiani na mahakama hiyo baada ya kupitia vi...

Tasaf Yamfikisha Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam Theresia

  Mwanafunzi wa mwaka wa pili Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Shule ya elimu (DUCE), Theresia Noel ambaye ni mlemavu wa viungo, akiwa kwenye maktaba ya Chuo hicho aeleza jinsi TASAF ilivyochangia kufanikisha ndoto zake pia amemshukuru Rais Samia na kumuomba kuendelea kutunisha mfuko huo.  Bibi Angelina ...mnufaika wa mfuko TASAF, akizungumza na waandishi wa habari namna alivyoanza kumlea mjukuu wake Theresia Noel ambaye ni mlemavu baada ya kutelekezwa na mama yake akiwa na miezi sita

Mkuu Wa Mkoa Wa Mwanza Apongeza Ofisi Ya Mwanasheria Mkuu Wa Serikali

  -kwa uamzi wake wa kuwafuata wananchi pale walipo.  Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhe. Saidi Mtanda amezindua Kamati ya Ushauri wa Kisheria ya Mkoa wa Mwanza tarehe 17 Februari 2025 na kufuatiwa na Kliniki ya Sheria bila malipo kwa wananchi wa Mkoa wa Mwanza inayoanza Februari 17 hadi 23, 2025 katika Viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kliniki ya Sheria bila malipo kwa Wananchi wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Mtanda amempongeza Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza Johari pamoja na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa Ujumla kwa kuuchagua Mkoa wa Mwanza na kufanya Kliniki hiyo. *“Nimpongeze Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Ofisi yake kwa ujumla kwa kuuchagua mkoa wetu wa Mwanza na kuja kufanya Kliniki hii ambayo itasaidia kutatua masuala mbalimbali yanayohusu sheria”.* Aidha, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, ameeleza kuwa Kliniki hiyo ni sehemu ya juhudi za Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kusogeza huduma karibu na wananchi kwa kuwafikia kwenye ...

Waziri Mavunde Apiga Marufuku Wageni Kuingia Kwenye Leseni Za Uchimbaji Mdogo

▪️Awataka wenye Leseni kufuata taratibu za kisheria za msaada wa kiufundi ▪️Serikali kutunga kanuni za kuratibu wageni kwenye Leseni ndogo ▪️Awataka RMO kufanya ukaguzi katika maeneo yao ▪️Awaonya wachimbaji wanaoingiza wageni kinyemela *📍Morogoro* Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde amepiga marufuku raia wa  kigeni kuingia na kufanya shughuli kwenye leseni za uchimbaji mdogo; hii ni kufuatia changamoto zilizobainika katika uingiaji mikataba ya utoaji wa misaada ya kiufundi kati ya wamiliki wa leseni ndogo za uchimbaji madini na raia wa kigeni.  Amesema hayo leo Februari 17, 2025 wakati akifungua Kikao Kazi cha kupokea maoni kutoka kwa wadau kuhusu mapendekezo ya kuandaa Rasimu ya Kanuni za Madini za Utoaji Msaada wa Kiufundi kwa Wamiliki wa Leseni Ndogo za Uchimbaji Madini za Mwaka 2025 kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Edema Hoteli Mkoani Morogoro. Aidha, Waziri Mavunde ametoa wito kwa washiriki wote wa Kikao Kazi hicho kutoa maoni yao kwa uhuru na uwazi ili kus...