Dkt. Rhimo Nyansaho achangia Shilingi Millioni 20 Ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Ring'wani wilayani Serengeti
Na Ghati Msamba; Serengeti MKURUGENZI wa Maendeleo ya Biashara wa Benki ya Azania Tanzania, Dk. Rhimo Nyansaho, ametoa mchango wa Shilingi Milioni 20 kusaidia ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Ring’wani kilichopo katika Kata ya Ring’wani, Wilaya ya Serengeti, Mkoa wa Mara. Dk. Nyansaho alikabidhi mchango huo kupitia Mwakilishi wake, Katibu Tawala wa Wilaya ya Serengeti, Angelina Marco, katika harambee iliyofanyika Desemba 23, 2024, Kijijini Ring’wani. Harambee hiyo ilihusisha wananchi, wadau wa maendeleo, na viongozi wa serikali. Katika harambee hiyo, zaidi ya Shilingi Milioni 84 zilikusanywa, ambapo Dk. Nyansaho alitoa Shilingi Milioni 20 taslimu. Serikali ilitoa ahadi ya Shilingi Milioni 50, na fedha nyingine zilizopatikana ni Shilingi Milioni 6.3 na Shilingi Milioni 8.2 zilizochangwa na Umoja wa Maendeleo wa Ring’wani, na ziliwekwa kwenye akaunti ya ujenzi wa Zahanati hiyo. Katibu Tawala wa Wilaya ya Serengeti Angelina Lubella alieleza kwamba lengo la Serikali ni kuhakikis...