Na NIRC,Namtumbo Waziri wa Kilimo Mhe Hussein Bashe ameleta kicheko kwa wananchi wa kijiji cha Lwinga Wilayani Namtumbo Mkoani Ruvuma baada ya kurejesha zaidi ya hekta 3,000 kati ya hekta 6,580 za shamba la serikali kwa wakulima. Waziri Bashe, amesema anatambua kuwa shamba hilo lina siasa nyingi lakini ni lazima kufanya maamuzi magumu kwa maslahi ya wananchi ambao wana haki ya kumiliki shamba hilo. Akizungumza wilayani humo katika muendelezo wa ziara yake,Waziri Bashe amesema, wananchi wa kijiji cha Lwinga wilayani Namtumbo wana haki ya kumiliki shamba hilo. “Iwapo kuna mwenye hoja awasiliane na mimi haiwezekani wananchi hawa wakose maeneo na wachache watake kujimilikisha wanavyotaka wao"alisema Waziri Bashe na kuongeza kuwa “Shamba hili lilikuwa la wananchi wakalitoa kwa serikali chini ya NAFCO ambao walilitumia kwa miaka nane kisha kulitelekeza na baadaye kurudishwa wizara ya Kilimo na Kilimo tumelitoa kwa Wakala wa mbegu ASA,limekuwa katika mgogoro kwa zaidi y...
Marato tv - Sauti ya Jamii