Skip to main content

Posts

Showing posts from May 22, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mbunge Mavunde Akabidhi Matofali 41,000 na Saruji Tani 102 Kuchochea Shughuli Za Maendeleo Dodoma Jiji

▪️Ni kuunga mkono miradi inayoibuliwa na wananchi kwa kata zote 41 ▪️Jiji la Dodoma latenga Bilioni 6 kuunga mkono miradi inayoibuliwa na wananchi ▪️Vifaa kulenga kuboresha sekta ya Afya na Elimu ▪️Rais Samia apongezwa kwa maendeleo makubwa Dodoma Jiji Mwenyekiti wa kamati ya Mfuko wa kuchochea maendeleo ya Jimbo na Mbunge wa Dodoma Mjini Mh. Anthony Mavunde leo amekabidhi matofali 41,000 na Saruji tani 102 kwa kata zote 41 za Dodoma Mjini kwa lengo la kuunga mkono miradi inayoibuliwa na wananchi katika ujenzi wa miundombinu ya Elimu na vituo vya Afya. “Mfuko wa Jimbo hujielekeza katika miradi ya kipaumbele ya Elimu,Afya na uwezeshwaji wananchi kiuchumi. Leo tunakabidhi matofali na saruji kwa kata zote 41 kwa lengo la kuunga mkono miradi inayoibuliwa na wananchi. Kwasasa Jiji la Dodoma limetenga Shilingi Bilioni 6 kuunga mkono miradi yote inayoibuliwa na wananchi ili kuchochea maendeleo zaidi ndani ya Dodoma Jiji. Mh. Rais Dkt. Samia S. Hassan amefanya kazi kubwa sana ya kuiendeleza Do...

Tanroads Mara Yafanikisha Barabara Kupitika Licha Ya Mvua Zinazoendelea Kunyesha"Rc Mtambi"

  Na Shomari Binda-Musoma  WAKALA wa Barabara "TANROADS" mkoa wa Mara imefanikisha kupitika kwa barabara inazozihudumia licha ya mvua zinazoendelea kunyesha. Mkuu wa mkoa wa Mara Kanali Evans Mtambi amesema kufanikisha huko kumetokana na kazi nzuri ya usimamizi unaofanywa na Meneja wa TANROADS mkoa wa Mara mhandisi Vedastus Maribe. Akiwasilisha utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020/2025 kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya mkoa wa Mara leo mei 22,2025.kenyw ukumbi wa chama hicho wa mkoa amesema kupitika kwa barabara hizo kwa kipindi chote kumesaidia kuinua uchumi wa wananchi wa mkoa wa Mara. Amesema TANROADS mkoa wa Mara katika kipindi cha miaka mine ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan imepokea kiasi cha bilioni 240.9 ambazo zimetekeleza miradi mbalimbali. Kanali Mtambi amesema kwenye mtandao wa barabara wa kilometa 893 ni kilometa 11 peke ambazo zina shida kidogo na zinaendelea kushughulikiwa. Amesema mradi wa barabara ya Tarime-Nyamongo hadi Serengeti yenye urefu...

Rc Mtambi Aanika Mafanikio Utekeleza Ilani ya Ccm,Azimio la Kumpongeza Lapitishwa

Na Shomari Binda-Musoma  MKUU wa mkoa wa Mara Kanali Evans Mtambi ameanika mafanikio lukuki ya Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ( CCM) katika kipindi cha mwaka 2020/2025. Mafanikio hayo ni katika sekta ya afya,elimu,maji,umeme,miundombinu na huduma za jamii ambayo imetokana na serikali ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kupeleka fedha nyingi za miradi kwenye mkoa huo. Akisoma taarifa ya utelezaji huo kwa wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Mkoa ya CCM leo mei 22,2025.katika hutuba iliyochukua zaidi ya saa 2 amesema wana CCM wanapaswa kutembea kifua mbele na mafanikio hayo. Amesema serikali  imetoa kiasi cha shilingi tilioni 6.8 ambazo zimetekeleza miradi ambayo imekuwa na manufaa kwa wananchi. Mtambi amesema miradi ya elimu ikiwemo ujenzi wa shule mpya na madarasa yamejengwa pasipo kuwachangiaha wananchi na kuwezesha wanafunzi kusoma maeneo sahihi.  Amesema kwenye eneo hilo la elimu utekelezaji mkubwa umefanywa na kutoa shukrani kwa Rais Dkt.Samia Suluhu Has...