Kairuki: Sekta ya Mawasiliano yapiga hatua kubwa Ndani ya Siku 100 za Uongozi wa Awamu ya Pili ya Rais Samia
KAIRUKI: SEKTA YA MAWASILIANO YAPIGA HATUA KUBWA NDANI YA SIKU 100 ZA UONGOZI WA AWAMU YA PILI YA RAIS SAMIA. Na Mwandishi wetu Dodoma Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mheshimiwa Angela Kairuki, amesema Sekta ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari imeendelea kukua kwa kasi kubwa ndani ya siku 100 za utekelezaji wa kipindi cha pili cha uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, DKT. Samia Suluhu Hassan. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma, Waziri Kairuki alisema mafanikio hayo yametokana na uwekezaji mkubwa unaoendelea kufanywa na Serikali katika ujenzi wa miundombinu ya mawasiliano, ikiwemo minara ya simu na Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano. “Takwimu zinaonesha kuwa laini za simu zilizosajiliwa zimeongezeka kutoka milioni 99.3 mwezi Oktoba 2025 hadi kufikia milioni 106.9 Januari 2026, sawa na ongezeko la asilimia 7.7,” alisema Waziri Kairuki. Aliongeza kuwa idadi ya watumiaji wa intaneti imeongezeka kutoka milioni 56.3 hadi milioni 58.1 kati...