Na. Joyce Ndunguru, Morogoro. Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), imemuaga rasmi aliyekuwa Kamishna wa Uhifadhi wa TAWA, Mabula Misungwi Nyanda baada ya kumaliza safari yake ya utumishi wa umma. Akizungumza katika hafla hiyo ya Kijeshi iliyofanyika Septemba 19, 2025, katika Ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TAWA, Mej.Jen (Mstaafu) Hamis Semfuko alimpongeza Kamishna Nyanda kwa kuhitimisha safari yake ya utumishi na kuwa Kamishna wa Uhifadhi wa kwanza wa TAWA aliyedumu kwa muda mrefu na kustaafu akiwa kwenye cheo hiko cha juu katika uongozi wa TAWA. “Kwa namna ya kipekee ningependa kukupongeza na kukushukuru Kamishna Mstaafu Nyanda kwa utumishi wako katika tasnia hii ya uhifadhi na hususan ukiwa kama Kamishna wa TAWA,” alisema Mej. Jen (Mstaafu) Semfuko. Sambamba na hilo, Semfuko aliongeza kuwa chini ya uongozi wa Kamishna Mstaafu Nyanda, TAWA imepata mafanikio mengi yakiwemo kuboresha maslahi ya watumishi, ujenzi...
Marato tv - Sauti ya Jamii