Skip to main content

Posts

Showing posts from December 21, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Dkt Mwigulu: Tuache Tabia ya Kuzoea Matatizo

*Afanya ziara ya kushtukiza Hospitali ya Wilaya Nachingwea WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewaonya watendaji na watumishi wa umma waache tabia ya kuzoea matatizo hasa katika sehemu zinazotoa huduma kwa wananchi. Ametoa onyo hilo jana (Jumapili, Desemba 21, 2025) wakati akizungumza na wagonjwa na watumishi wa Hospitali ya Wilaya ya Nachingwea mkoani Lindi alipofanya ziara ya kushtukiza ili kujionea hali halisi ya utoaji huduma siku za wikiendi katika hospitali hiyo. Waziri Mkuu ambaye alikuwa na ratiba ya kukagua ujenzi wa ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea, mara baada ya kuwasili wilayani humo akitokea Ruangwa, aliamua kuanzia kwanza hospitalini kisha akaenda kwenye ukaguzi wa jengo hilo. Akiwa hospitalini hapo, alienda moja kwa moja kwenye chumba cha daktari wa zamu ili apate utaratibu wa kumhudumia mgonjwa pindi anapofika hospitalini na akaelezwa kwamba ni lazima mgonjwa aanzie mapokezi na kukata cheti ndipo aje kwa daktari. Hata hivyo, Waziri Mkuu alikuta wagonjwa wawil...

Dkt.Mwigulu aagiza ziundwe timu za mikoa za wakaguzi wa miradi

_A watenge gharama ya vifaa vyataka_   WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amemwagiza Waziri wa Nchi (OWM-TAMISEMI) awaandikie barua Wakuu wote wa Mikoa ili waunde timu za majengo na miradi kwenye mikoa yao kama njia ya kuweka na wakandarasi wanaokiuka makadirio ya gharama za ujenzi (BOQ) wa miradi ya Serikali. "Yuko Mhandisi ambaye huwa anakagua miradi wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru. Wakuu wa Mikoa wote wawe na timu za vijana wa aina hiyo, ili wasiuziwe mbuzi kwenye gunia. Iwe ni utamaduni wa Serikali kufanya mtihani wa aina hiyo," amesema Waziri Mkuu.  Ametoa agizo hilo leo (Jumapili, Desemba 21, 2025) wakati.na viongozi na wananchi wa Wilaya Ruangwa na Nachingwea, mkoani Lindi akiwa katika ziara ya siku tatu ya kukagua miradi ya maendeleo mkoani humo.   Akizungumza mara baada ya kukagua ujenzi wa ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea, Waziri Mkuu amesema kuna baadhi ya miradi ambayo wakandarasi wake hawafuati BOQ. "Unakuta BOQ inataka nondo za mm 16 lakini mkan...

Waziri Simbachawene Awaomba Wana Kagera Kuwekeza Nyumbani

 Na Angela Sebastian; Bukoba Waziri wa Mambo ya ndani ya nchi Georgia Simbachawene amewataka wanakagera waishio nje ya Kagera kurudi nyumbai ili kuwekeza ikiwa ni kuasisi tamasha la Ijuka Omuka linalowakutanisha wanakagera wote kwa maslai ya vizazi vilivyopo na vijavyo. Amesema hayo wakati wa kufunga Tamasha la utamaduni la Ijuka Omuka ambapo amewataka wazazi wote nchini kuwafundisha mila,desturi na utamaduni wa wazee wao ili waepuke kujiingiza katika mambo yasiyofaa. Aidha amewashauri wanakagera kufanya uzalishaji wa tija katika zao la ndizi na bidhaa nyingine zitokanazo na zao hilo pia kufanya utafiti wa ndizi zinazofaa kuzalishwa na kuzwpa nje ya nchi na kuingiza uchumi wa mkoa wa Kageta na Taifa letu  Kwa upande wa mkuu wa mkoa wa Kagera Hajat Fatma Mwassa amesema lengo la Tamasha hilo ni kuirudisha Kagera kwenye uhalisia wake,kujadili maendeleo yao,kuibua fursa zilizopo na kutengeneza mikakati ya kutatua changamoto zinazoukabili wa mkoa huo.

Dkt Mwigulu Aagiza Ziundwe Timu za Mikoa za Wakaguzi wa Miradi

*Ataka watenge bajeti ya vifaa vya ukaguzi WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amemwagiza Waziri wa Nchi (OWM-TAMISEMI) awaandikie barua Wakuu wote wa Mikoa ili waunde timu za ukaguzi wa majengo na miradi kwenye mikoa yao kama njia ya kukabiliana na wakandarasi wanaokiuka makadirio ya gharama za ujenzi (BOQ) wa miradi ya Serikali. "Yuko Mhandisi ambaye huwa anakagua miradi wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru. Wakuu wa Mikoa wote wawe na timu za vijana wa aina hiyo, ili wasiuziwe mbuzi kwenye gunia. Iwe ni utamaduni wa Serikali kufanya ukaguzi wa aina hiyo," amesema Waziri Mkuu.  Ametoa agizo hilo leo (Jumapili, Desemba 21, 2025) wakati akizungumza na viongozi na wananchi wa Wilaya za Ruangwa na Nachingwea, mkoani Lindi akiwa katika ziara ya siku tatu ya kukagua miradi ya maendeleo mkoani humo. Akizungumza mara baada ya kukagua ujenzi wa ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea, Waziri Mkuu amesema kuna baadhi ya miradi ambayo wakandarasi wake hawafuati BOQ. "Unakuta BOQ i...

Kongani ya Viwanda Kahama Kuifanya Tanzania Kuwa Kitovu cha Uzalishaji Bidhaa za Mgodini

▪️Ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais.Dkt. Samia Suluhu Hassan. ▪️Zaidi ya Wawekezaji 30 waonesha nia ya kuwekeza kwenye sekta mbalimbali ▪️ Viwanda 15 vya kuzalisha bidhaa za migodini kuanzishwa ▪️Ajira zaidi kwa Vijana kuongezeka *Shinyanga* Kufuatia kuhitimishwa kwa shughuli za uchimbaji katika eneo la Buzwagi, Serikali imeweka mkakati na kutenga eneo hilo kwa ajili ya viwanda hususan vya uzalishaji wa bidhaa na huduma za mgodini na kuiweka Tanzania kuwa kitovu cha uzalishaji wa bidhaa na huduma kusini mwa jangwa la Sahara. Hayo yameelezwa leo Desemba 21, 2025 na Waziri wa Madini, *Mh. Anthony Mavunde* alipotembelea na kukagua eneo hilo la kongani ya viwanda Buzwagi, lililopo Kahama Mkoani Shinyanga. Waziri Mavunde amesema kuwa, Mh. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan* anataka kuona eneo la Buzwagi linabadilishwa na kuwa kitovu cha uchumi wa viwanda nchini. Waziri Mavunde amefafanua kuwa, zaidi ya viwanda 30 vitajengwa katika sekta mbalimbali ikiwamo nishati, Elimu , uzalishaji bidhaa za ...

Waziri Mkuu Dkt.Mwigulu Nchemba akutana na Waziri mkuu Mstaafu Kassim Majaliwa

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amekutana na Waziri Mkuu Mstaafu Kassim Majaliwa nyumbani kwake Nandagala, Ruangwa mkoani Lindi. Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amekutana naye wakati akiwa katika ziara ya siku tatu ya kikazi  mkoani Lindi.