Skip to main content

Posts

Showing posts from April 22, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mbunge Mathayo Aendelea Kuwezesha Vijana Mkopo Nafuu wa Pikipiki

Na Shomari Binda-Musoma  MBUNGE wa Jimbo la Musoma mjini Vedastus Mathayo ameendelea kuwezesha vijana mkopo nafuu wa pikipiki. Leo aprili 22,2025 vijana 75 wameingia kwenye utaratibu huo na kupata pikipiki ambazo watarejesha kwa kipindi cha miezi 11 na kuweza kumuliki. Akizungumza mara baada ya kukabidhi pikipiki hizo mbunge huyo amesema lengo lake ni kusaidia vijana waweze kumiliki pikipiki zao na kuiiinua kiuchumi. Amesema amekubaliana na moja ya kampuni zinazouza pikipiki na kijana anayetoa kiasi cha shilingi laki 3 anamuongezea laki 1 na elfu 9 na kuendelea kulipa kidogo kidogo. Mathayo amesema mkopo huo ni nafuu tofauti na mikopo mingine ya gharama kubwa na inayolipwa kwa muda mrefu ambayo itawasaidia vijana. Mbunge huyo amesema hii ni awamu ya pili ya vijana kuwezeshwa kwenye upande wa pikipiki na kudai kuendelea na utaratibu huo kila vijana watapojitokeza. " Hii ni awamu ya pili tunawapatia vijana pikipiki za mkopo nafuu ili baadae waweze kuzimiliki na kufanya shughuli zao ...

Balozi Nchimbi: Tusivurugwe Miezi Michache Kuelekea Uchaguzi Mkuu

_Aelekeza RC, Mawaziri wawili kulipa fidia Nyatwali – Bunda_ Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, amewataka Watanzania kuchukua tahadhari dhidi ya wanasiasa wanaojaribu kuhatarisha haki, amani na utulivu wa nchi, huku Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 ukikaribia kwa miezi mitano tu. Akizungumza na wananchi wa Bunda leo Jumanne, tarehe 22 Aprili 2025, wakati wa ziara yake ya siku tano mkoani Mara, Dkt. Nchimbi alisema kipindi cha uchaguzi huwa na majaribu mengi, ikiwemo uchochezi wa chuki, uhasama na vurugu unaotokana na kauli au matendo ya baadhi ya watu, hasa wanasiasa. “Mwaka huu mtasikia maneno mengi, hata wasiozoea kusema watajaribu kusema ili kuchonganisha na kuamsha vurugu. Watanzania tuwakatae watu wa aina hiyo. Tusikubali amani yetu iliyodumu tangu uhuru ichezewe ndani ya miezi michache kabla ya uchaguzi,” alisema. Balozi Nchimbi aliwasifu wananchi wa Bunda kwa kuwa watu wa kazi na maendeleo, akisema: “Ukija kwa watu wa Bunda na kuzungumzia ma...

TUlinde, Tuenzi Utamaduni Kwa Manufaa Ya Vizazi Vyetu- Majaliwa

▪️Asema tusikumbatie tamaduni zinazokwenda kinyume na maadili na ustaarabu ▪️Prof. Kabudi asema sarakasi ni mchezo unaongoza kuliingizia Taifa fedha za kigeni   WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema Watanzania wana wajibu wa pamoja wa kuhakikisha urithi wa utamaduni wa Taifa unalindwa, unaenziwa na kuendelezwa kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho. Amesema hatuwezi kuwa na Taifa bila kuwa na utamaduni unaolitambulisha na kututofautisha na mataifa mengine. “Utamaduni ni utambulisho wetu halisi kama Taifa. Utamaduni wa Taifa letu ndiyo unatufanya tutambuliwe kuwa sisi ni Watanzania bila kujadili tofauti za makabila, jamii au sehemu tunazotoka.” Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumanne, Aprili 22, 2025) alipofungua Kikao Kazi cha 15 cha Maafisa Utamaduni na Maendeleo ya Michezo kilichofanyika kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam. “Kamwe tusikubali kukumbatia tamaduni zinazokwenda kinyume na maadili na ustaarabu wetu. Tusikubali kuwa watumw...

Mbunge Wanu Ameir Afungua Mafunzo Kuwajengea Uwezo Viongozi Uwt

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kusingi Unguja, Mhe. Wanu Hafidh Ameir amefungua mafunzo elekezi kwa viongozi na watendaji wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kuanzia ngazi ya Matawi, Wadi, Jimbo na Wilaya yaliyofanyika kwenye ukumbi wa TASAF, Zanzibar Wanu amefungua mafunzo hayo tarehe 20 Aprili, 2025 yenye lengo la kuwajengea uwezo viongozi na watendaji wa UWT hasa kutokana na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinapoelekea kushiriki uchaguzi mkuu wa kuchagua Rais, Wabunge, Wawakilishi na Madiwani nchi nzima ifikapo mwezi Oktoba, 2025. Akizungumza katika mafunzo hayo, Mhe. Wanu Ameir amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwawezesha viongozi hao wa UWT ngazi zote kukumbuka wajibu wao hasa CCM inapokuwa kwenye uchaguzi na kupanga mipango ya ushindi Mhe. Wanu Ameir amewasisitiza wanawake kuwa wasisite kujitokeza kuchukua fomu na kugombea nafasi za uongozi wa dola nchini kwani Wanawake wanaweza lakini ni lazima kwanza wathubutu kwa kuonesha nia ya kuwatumikia wananchi Mwisho, Mhe. Wanu Ameir amewaponge...