WASHINGTON, MAREKANI KATIKA tukio nadra sana, Rais wa Marekani Donald Trump amemsifia kiongozi wa Afrika kwa kuzungumza Kiingereza kwa ufasaha. Trump mnamo Jumatano alikutana na kundi la marais kutoka Afrika ambao wanazungumza lugha mbalimbali. Walitumia nafasi hiyo kutoa wito wa kukuzwa kwa uhusiano wa kibiashara kati ya Marekani na nchi zao. Hata hivyo, kilichomteka makini Trump ni jinsi Rais wa Liberia Joseph Boakai alivyozungumza Kingereza kwa ufasaha akipigia debe kuimarishwa kwa uhusiano kati ya taifa lake na Marekani. “Liberia ni rafiki mkubwa wa Amerika na tunaamini katika sera yako ya kufanya Marekani iwe bora tena (MAGA),” akasema Rais Boakai kwenye Ikulu ya White House wakati wa mkutano huo wa uwekezaji na marais wa Guinea Bissau, Senegal, Mauritania, Gabon na Liberia. “Tunataka kukushukuru sana kwa nafasi hii tukizi ya kukutana nasi,” akaongeza. Trump alifurahishwa na ufasaha wa Boakai hata akauliza mahali ambapo kiongozi huyo alisomea lugha. “Kingereza kizuri na bora zaidi...
Marato tv - Sauti ya Jamii